Tuwasaidie wepi, Yanga? Ndiyo imeshapangwa hiyo hakuna jinsi. Wajue tu kwamba njia ya Jehanamu imejaa tele njia njema. Simba? Wakubali yameisha wajipange vizuri kwa msimu ujao ili wasiendekeze wala isilazimike kubebwa. Azam? Nao wajipange wasilazimishe vitu vinavyochangia kuwa gaming wenyewe, Kama ni ubeleko unakuwa una upupu (mbegu fulani za porini zinazowasha sana). Nasikia wana akademi ya maana. Hiyo ndiyo ipeleke timu kwenye 'Ndondo Cup' za kimataifa. TFF? Wajue ukitaka kuwaridhisha wote hutamridhisha hata mmoja. Wajue kwamba timu si Azam, Simba na Yanga peke yao.
Wakati hayo ya Yanga na Ndanda yakionekana ni kituko cha kihistoria kwenye soka club za Atletico na Real Madrid wamekubaliana kucheza mechi katika jiji la Madrid hivyo wameiomba Uefa kuhamisha mechi kutoka kwa Muitaliano.
Mbona hizi Timu zenyewe sioni zikifanya vizuri katika mashindano ya kimataifa..
Pia watangazaji na mashabiki Kuna kitu wanajisahau kuzani Simba, Yanga.. Kuzani matokeo yanayostahili ni Ushindi TU.. Vilabu vingine havistahili Ushindi