Augustine Lyatonga Mrema: Mpiganaji!


Mkuu uwezo wako wa kupambana na propaganda ni mkubwa,yote uliyoyasema ni kweli tupu!Mrema si tu kuwa ni mpiganaji,bali mpiganaji halisi,na CCM naona bado wakimfikiria hawapati usingizi,tumepata fagio jipya ila la zamani kamwe hatutalitupa maana linajua kona zote za nyuma...Long live Lyatonga mzee wa inji hii...!Na muencourage kuwa mapambano yanaendeleaa!
 
Tunatakiwa kuwa na kiongozi mwenye vision, mwenye akili, mwenye uwezo wa kuongoza , kupenda maendeleo, kutoa leadership na mwenye uwezo wa kumanage. Si lazima kila hii quality ipatikane kutokana na elimu. Unaweza kusoma kama baadhi ya viongozi wetu wa sasa lakini usiwe na hivyo, unaweza usisome lakini ukawa na uwezo mkubwa wa ku-manage.

Kiti cha urais, uwaziri, ubunge na uongozi mwingine hauhitaji kufanya kazi kwa kubahatisha au kutegemea tu ushauri wa watu. So Mrema kwa maoni yangu alikuwa very patriotic kwa kuwa aliipigania sana Tanzania, lakini hakuwa na uwezo wa kuwa rais kwa kuwa sera yake kubwa ilikuwa ni kuwiangiza magereza wezi na vigogo wa wakati ule. Hakuwa na mapendekezo yoyote ya sera ambayo ingemsaidia mtanzania.
Angefanya alilotaka kwa mwezi au miezi miwili kuwa rais kunakuhitaji ufanye kazi kwa at least miaka 5, yeye angefanya nini?
 
 

Vigogo na majambazi wa wakati ule ni tofauti na hawa wa sasa? Si ni wale wale? Toauti ni msamiati tu kwani wakati ule waliitwa simply vigogo na sasa ni mafisadi,majambazi ni wale wale ushahidi upo....Inawezekana sisi watanzania tunachukua muda mrefu kutambua....Kumbuka kuwa failure to understand back then is what costs us this time. Matatizo yote aliyokuwa akiyafanyia kazi na kukatishwa tamaa na watu kama nyie ndiyo yamesamiri na kukubuhu hivi sasa na hata kuwaumiza vichwa wapiganaji wengi.
Sasa wezi na vigogo wa wakati ule si ndio hawa wanaotucost wakati huu? Ebu nieleze,hao kina Mramba si ndio aliokuwa akipambana nao?Kina Mkapa? Halafu na hao majambazi unaodai wa wakati ule si ndio hao hao waliomfanya JK aigawe Dar kikanda kwenye idara ya polisi?
Mkuu tumia muda kidogo kufikiri kabla hujaposti,itasaidia sana kwani mnategemewa na wananchi. Say what you think is right bila kujali nani atafikiri nini hapa jamvini.
 

1. Mrema hana sera , sera ni za chama
2. Aliwaza na kufanya hayo akiwa waziri wa mambo ya ndani, unajua angefanya nini kama angeshika wizara ya nishati?
3. Viongozi unaowaona wewe wana uwezo wa kuongoza miaka 5 ni akina nani, na wamefanya nini?
4.Huoni kuwa unaongea falsafa kuwaza kuwa YEYE ANGEFANYA NINI?

NI rais gani aliyeingia madarakani ambaye ulipata hakika tangu mwanzo kuwa akiingia,atafanya kitu fulani na fulani kwa miaka mitano?
 
 

Mkuu i think i am right as you may think am wrong and as i may think that you are wrong. Mrema ni mpiganaji, ni mzalendo, na mwenye uchungu na nchi, as well as my hero. My point is to be a president is much more than that. It is far more difficult job than to be a minister of home affairs or deputy prime minister for that matter. Leading a ministry as not the same as leading or ruling the country, you do not have to be emotional, unreasonable and you need to have a personality for that office. Mream lacked almost in all. I may be wrong on this, but it is why i did not vote for Mrema. I never liked Ben Mkapa, but i knew he would make a better president that Lyatonga, and voted for him. Mbunge nilimpigia wa upinzani.
 
Mkuu FM
Kati ya wanajamvi wanaonivutia kwa hoja zilizo simama wewe ni mmoja wapo.
Bilashaka kuna jamaa kaiba password yako,umekuwa chini ya viwango katika hii hoja kwa kiwango cha kutisha.

- Kwa kawaida huwa unaanza na hoja, halafu nikukubana mbavu then huwa unabadilika kama kinyonga na kuanza maneno ya low kama haya ambayo hayana anything na kuwasadia wananchi wala taifa, naona nikuachie ubaki nayo, maana I am too big for this lows.

- Ndio maana nilisema kwamba I am looking forward for the day nitajadili siasa na wewe bila nonsense za personal's speculations.

Respect.

Kamanda FMEs!
 

- Unajua Mungu anasema watu wangu wanakwisha kutokana na kutokuwa na hekima, bila kutumia hekima huwezi kuelewa madhara ya kutokwua na elimu kwa kiongozi wa juu, saafi sana Bongolander maneno mazito sana haya.

Respect.

FMEs!
 

So unataka kuniambia kuna sera yoyote ya kulinda ufisadi inayotekelezwa sasa na serikali, kwenye ilani ya CCM? Hii ni sera inayitekelezwa lakini haipo kwenye manifesto. Sera za chama zinatengenezwa na nani, na wanachama au zinajitengeneza zenyewe?
Kwa hiyo kiongozi anaweza kuja na policy suggestion ambayo inaweza kuja kuwa sera, au akatawala kwa decree, kama mrema alivyokuwa antoa siku saba kwa watendaji wa serikali. Angekuwa rais angekuwa mtawala wa kiimla na sio wa sheria au anayeongozwa na sera.

Kama kazi yake ilikuwa kukamata wezi angeenda wizara ya nishati angeshindwa, kwa sababu nishati hawakamati wezi, isipokuwa wanashughulikia mambo ya nishati, ku explore vyanzo vipya vya nishati, kunahitaji innovation capabities and alike.
Nilikuwa na uhakika kuwa Ben Mkapa akiingia madarakani ataweza kustabilize uchumi na kupunguza inflation, which he did. Nilidhani kuwa atapigana na rushwa i was wrong.
Kwa hiyo inawezekana kabisa kuwa you are wrong on what you think about Lyatonga.
Mfano mzuri uko kwa magufuli, amejaribu kung'ara kwenye wizara ya ujenzi, kungia ardhi imekuwa kinyume ameuzia nyumba ndugu zake, kuna uwezekana hata Lyatonga angefanya hivyo.
 

- Ukishaona mafisadi wameamua kufanyia vikao vyao vya siri mkoani mwako, basi ujue wana sababu kubwa sana nayo ni they feel at home na very comfortable huko kwako kwamba kuna wananchi wengi na ni mazingara wanayofanana nayo, that is very sad truth!

- Mkuu ahsante sana kwa your Great Thinking, labda tu nikukumbushe hii mada ni about wapiganaji na Mrema, na sio mawaziri wakuu wa zamani, Bwa! ha! unaweza kufungua thread inayowahusu ukatoa kilio cha uhuni wao maana ni muda sasa unalilia sana hiyo ishu, ambayo kila ukipewa nafasi kuichambua unashindwa na kuingia mitini, bwa! ha! ha!.

Respect.

Kamanda FMEs!
 
 

Acha utani mkuu,kuwa raisi wa Tanzania is much more than what?Pia ungesoma posting ya Philemon Mikael ungeweza kuona kuwa sifa ulizotaja hapo juu hazijawa proof kuwa a certain leader will accomplish anything.... Hapo nyuma kama ungenisoma vyema ungegundua pointi yangu kuwa siasa za vyama zimetuangusha...Sasa hapo kwenye red highlight ebu nieleze what do you mean?Vigezo tunavyowekeana sisi waafrika ndio vimetufanya tushindwe kujitawala,na certainly mzungu alivutiwa na udhaifu huo na ndio maana akatutawala,hatujui tunataka nini na kwanini....Vigezo alivyovitoa mwalimu vya kumchagua Mkapa ni tofauti kabisa na hivi unavyovitoa hapa..Kwamba ufanisi wake akiwa wizarani ndio kigezo cha yeye kuchaguliwa kama unavyotaka kudai si kweli,matter of fact hakuna aliyewahi kufikiri kuwa Mkapa will be a president,na sisi watanzania tulikuwa hatuna utaratibu wa kujichagulia viongozi bali someone decided for us! Pia vipi kuhusu Mwinyi? Ni ufanisi upi huo uliopelekea kuwa na sifa za urais?

Tanzani bado ni nchi changa sana na hatuwezi kuweka vigezo vya kumpata kiongozi nje ya hali halisi tuliyonayo...Kama ingekuwa ni enzi zile na wewe ukaambiwa uchague kati ya Mrema na Mr Smith basi si ajabu ungemchoose Mr Smith kwa vigezo ulivyoweka...Sisi tumezoea kuambiwa cha kufanya na kuchaguliwa viongozi na kwa hiyo uwezo wetu wa kutambua kiongozi anayetufaa ni mdogo ama inawezekana haupo kabisa kwa watanzania walio wengi..Tusiishi kwenye nchi ya kufikirika,kwamba tunaweza kutumia vigezo vya lets say USA ili kumpata kiongozi bora wa Tanzania...Yani umesoma elimu ya mzungu ya jinsi gani ya kumpata kiongozi halafu directly una imply kwamba inaweza kutumika Tanzania ama nchi nyingine ya Afrika,haya mambo huenda stage by stage,hatujafikia kutumia vigezo vya juu,bado tuko chini,tunahitaji mtu tuliye naye,mwenye kutuelewa ili kuondoka hapo tulipo,mkoloni kututawala kwa vigezo hivyo alivyokufundisha imetufikisha wapi? Kwa vigezo hivyo mtanzani atakombolewa kweli? Umesema Mrema ni mzalendo,halafu then hafai kutuongoza,urais kama taasisi,uzalendo ni hatua kubwa ya kwanza na mengine atapata msaada wa kimawazo kwani hizi si zile enzi za zidumu fikra sahihi za mtu mmoja.

Wananchi nao wanatatizo la kufuata sheria,mnajuwa kabisa kuwa sheria hazifuatwi,lakini nyie ndio wa kwanza kusema kuwa viongozi mnaowachagua ni vinara wa kufuata sheria...Kweli hiyo? Tungekuwa hapa tulipo? Eti you knew Mkapa will make a better president than Mrema,hapo umenichosha,umeshindwa kutambua tatizo kuu lililotufikisha hapa tulipo,bado hulielewi na tatizo la kusahahu mapema unalo...Yani ufisadi kushamiri na maisha ya mtanzania kuporomoka ndio kujenga uchumi kunakokufanya uwe proud kuwa ulimpigia Mkapa kura...?Tutaona mengi!
 
 
 
 
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…