Autoimmune disease

Nani kakuambia ugonjwa wake una uhusiano na gluten? Wewe kusubtitle video hakukufanyi uwe daktari maana mwisho wa siku utajikuta unapotosha km unavyofanya sasa! Anachoumwa jamaa kinatokana na kuwahi kupata ugonjwa unaitwa Guillane Barre Syndrome ( tamka Giya Baree) huko nyuma ambao haukutibika kikamilifu ndio kwa sasa anapata CIPD km late complication. Mimi namshauri ashikamane na Neurologist wake vzr na sio kutapatapa humu ndani wahuni na wajinga wampotoshe
 
Mkuu nimekwambia mimi si daktari, nmekwambia nilipata informations kutoka kwenye videos nilizo subtitle kama mtu mwingine yeyote anayeweza kupata infos.
Na baadhi ya watu ambao walishauriwa kuacha kutumia chakula chenye gluten walikuwa na conditiins kama zake. Tena mmojawapo alikuwa yeye anashambuliwa cell za ubongo hadi alikuwa imefika kipindi hawezi kuzungumza wala kutembea. Alianzishiwa tiba ya kuminya immune system, na akashauriwa aache kutumia vyakula vye gluten na kwa sasa anaendelea vzuri.
Hapa tunapeana mawazo kutokana na experience na information tunazopata kwa kujisomea.
 
Kwa akili yako unafikir kuna mganga wa kienyeji au mitishamba anaujua ugonjwa unaitwa chronic inflammatory demyelinating polyneuropathy mpaka ajue dawa ya kuutibu? Au huyo mganga anatibu ugonjwa ambao haujui wala hajawahi hata kuusikia?
Magonjwa hayo zaman yalikuepo na yakatibika kwa njia za asili acha zarau.....
 
Unajua huyo alikuwa anaumwa ugonjwa upi na je, unafanana na aliosema anaumwa mleta mada? Kufanana dalili hakufanyi magonjwa au tiba kuwa Sawa! Malaria na Typhoid zote zinaleta homa lakini hazifanani wala tiba zake sio sawa! Back to the topic kwanini unatak huyo jamaa akusikilize wewe unayebahatisha badala ya kumsikiliza specialist doctor ( Neurologist) anayemtibu? Ni mtu mjinga pekee anayeweza kufuata ushauri wa mtu mwenye elimu ya kuunga unga akaacha kumsikiliza Daktari bingwa aliyeenda darasani miaka 10
 
Walitibu magonjwa wasiyoyajua majina? Na km waliyatibu ilikuwaje Waafrika tulikuwa tunakufa mapema kulinganisha na races nyingine?
Magonjwa yote yana majina kulingana na jamii husika...inshu ya kufa ipo kinadharia sana haina ukweli huo........
 
Humu watu wanaleta matatizo yao, watu wanashauriana kwa experience na knowledge walionayo... Ni mhusika mwenyewe anaamua kufuata au kutofauta.
Mimi nilikuwa na ndugu yangu aliumwa akawa anapgwa ganzi ilianza vidole vya miguuni ikapanda hadi kiunoni, anaishi miguu inawaka moto inakaza halali kutembea hawezi, tumezunguka hospital anatumia dawa lakini wapi.
Kuna mtu humu si daktari alishauri atumie dawa inauzwa 12000 wakat hapo tulikuwa tumeshatumia ela nyingi, tumetembelea hospitali kibao.
Ile dawa alipoanza kuitumia alianza kupata nafuu mpaka leo yuko sawa anatembea yuko vzuri na hiyo ilikuwa 2017 hadi 2018.
Na watu wengi huwa wanakuja humu baada ya kuwa wanaona matibabu wanayopewa hayaleti matokeo.
 
Magonjwa yote yana majina kulingana na jamii husika...inshu ya kufa ipo kinadharia sana haina ukweli huo........
Hebu tueleze huo ugonjwa unaitwaje kikwenu,utuelezee namna unavyotokea na tiba yake inavyofanya kazi. Baada ya maelezo hayo nitakuunga mkono tiba yako
 
Inawezekana kweli 1 in a million case! Lakini ukifuatilia maelezo ya wengi wetu humu ndani ni upotoshaji tupu
 
Inawezekana kweli 1 in a million case! Lakini ukifuatilia maelezo ya wengi wetu humu ndani ni upotoshaji tupu
Sisi madaktari wa mtaani huwa hatuhitaji kuona vipimo na hata ukituonyesha hatuwezi kuelewa so tunashuriana kwa kuhisi, experience au kusoma au hata kusikia kuwa fulani alikuwa na dalili fulani zinafanana zako alipona kwa kufanya hivi.
So labda tuweke angalizo kwamba ushauri huu usiwe mbadara wa ushauri wa daktari. Ufuate at your own risk.
 
Hebu tueleze huo ugonjwa unaitwaje kikwenu,utuelezee namna unavyotokea na tiba yake inavyofanya kazi. Baada ya maelezo hayo nitakuunga mkono tiba yako
Mleta mada amekujua kuomba info kama kuna mtu alishawai kupata matibabu mbadala kutoka kwa wataalamu wa dawa zakienyej hivyo ulipaswa kuumpa moyo na sio kumcancell hakuna tiba hizo.....
Kwa upande wangu sijui ila wapo wanaojua.......
 
Hiyo dawa inaitwaje mkuu maana hizo dalili za huyo ndugu yako zinafanana kama na za kwangu kabla sijaanza kupata matibabu ya immunoglobulin.
Miguu kukaza sana hasa baada ya kupumzika kwa muda ama kulala.
 
Hiyo dawa inaitwaje mkuu maana hizo dalili za huyo ndugu yako zinafanana kama na za kwangu kabla sijaanza kupata matibabu ya immunoglobulin.
Miguu kukaza sana hasa baada ya kupumzika kwa muda ama kulala.
Mkuu, ngoja nitamuuliza nikwambie maana sikumbuki jina lake ngoja nitamuuliza nikwambie mkuu nikimpata kwenye simu maana nimejaribu hapa naona hapatikani na tuko mikoa tofauti na bahati mbaya huyo jamaa alinitumia PM kwenye ID yangu ya zamani ambayo siikumbuki hata password. Ila nikimpata ntakwambia mkuu.
 
Mleta mada amekujua kuomba info kama kuna mtu alishawai kupata matibabu mbadala kutoka kwa wataalamu wa dawa zakienyej hivyo ulipaswa kuumpa moyo na sio kumcancell hakuna tiba hizo.....
Kwa upande wangu sijui ila wapo wanaojua.......
Exactly! Nimekuja hapa kuomba ushauri kwa mtu aliewahi kutibiwa huu ugonjwa akapona kabisa ama kwa mtaalam anaeweza kunipa ushauri jinsi ya kufanya kukabiliana na hili tatizo.
 
Mwili unashambulia mylen sheath na kupelekea impulse ku slow down.
Pole sana ila mara nyingi autoimmune diseases ni irreversible, komàa hivo hivo ku slow down progress.
 
Kwa akili yako unafikir kuna mganga wa kienyeji au mitishamba anaujua ugonjwa unaitwa chronic inflammatory demyelinating polyneuropathy mpaka ajue dawa ya kuutibu? Au huyo mganga anatibu ugonjwa ambao haujui wala hajawahi hata kuusikia?
Kwa akili yako unafikir kuna mganga wa kienyeji au mitishamba anaujua ugonjwa unaitwa chronic inflammatory demyelinating polyneuropathy mpaka ajue dawa ya kuutibu? Au huyo mganga anatibu ugonjwa ambao haujui wala hajawahi hata kuusikia?
TIBA ya asili inaweza kusaidia kutibu pia magonjwa sugu.
Usidharau mitishamba.
 
Mwili unashambulia mylen sheath na kupelekea impulse ku slow down.
Pole sana ila mara nyingi autoimmune diseases ni irreversible, komàa hivo hivo ku slow down progress.
Nurse wangu pia ameniambia hivyo kwamba inawezekana ntakua tegemezi wa hii therapy kwa muda mrefu sana that’s why nimekuja hapa kuomba ushauri wa tiba mbadala.
Kuwekea immunoglobulin kila mwezi inachosha sana na pia matibabu yake yana gharama
 
Pole sana kama uko dar nenda Upanga ulizia dispensary ya Family care chini ya mtu anaitwa Profesa Matuja

Mueleze A_Z atakusaidia akishindwa rejea kwangu ila nitakutaka Mbeya mwezi mzima ili uwe sawa .

Pole sana .
Vyakula tunavyokula ndivyo vitakavyotuuwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…