Aveva na kundi lako siku zenu simba zinahesabika

Aveva na kundi lako siku zenu simba zinahesabika

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Simba kukosa tena ubingwa mwaka huu ni jambo ambalo sisi wanasimba hatutakubali , Hii nakujulisha mapema usije kusema tumekuvizia .

Tutakutimua bila huruma , viongozi gani mnaokosa mbinu kiasi hicho ? Hakuna ligi katika miaka mitano iliyopita iliyokuwa rahisi kwetu kama hii , sasa inashangaza sana tunafungwa na timu iliyojaa migogoro na isiyo na kocha wa uhakika kama Azam.

Ni vigumu sana kuwakamata Yanga ( wazee wa fitna ) wakishakaa kileleni , na hili wewe unalijua vizuri sana .

Safari hii tusipobeba ndoo hakutakuwa na Mswalie Mtume , ni heri muondoke wenyewe kwa hiyari yenu .

Simba haiwezi kuwa kichwa cha mwendawazimu.
 
Mkuu hizi shutuma mbona huzielekezagi pia kwa mwenyekiti wako Mbowe?
 
Mbinu atoe Aveva kwani yeye kocha..

Yeye kaajiri makocha kwa kazi hiyo


Mpaka muwaombe radhi familia ya Mafisango ,walifukuzwa kama mbwa chang'ombe

Kaombeni msamaha na mpeleke rambirambi mliyokula

Mpaka mseme pesa ya rambirambi mlipeleka wapi
 
Kama team inapewa kila kitu na wanarukaruka tu unataka viongoz wafanye nini?mchawi wa Simba ni kuamini wanaonewa na kuna team zinabebwa nimeona hata leo na Azam maamuzi sahihi makocha washabik na viongoz wanataka kuingia uwanjani!kuna maamuzi yalikua dhidi ya Azam unaona kabisa wachezaji wa Azam walivyoandaliwa kisaikolojia pale refa anapotoa maamuzi wasiokubaliana nayo
 
Mbinu atoe Aveva kwani yeye kocha..

Yeye kaajiri makocha kwa kazi hiyo


Mpaka muwaombe radhi familia ya Mafisango ,walifukuzwa kama mbwa chang'ombe

Kaombeni msamaha na mpeleke rambirambi mliyokula

Mpaka mseme pesa ya rambirambi mlipeleka wapi
Hii tuhuma aelekezewe Aden Rage , kwanini unatutupia watu wote ?
 
Kwani Simba ni timu ya ukoo ? Achana nayo , kashangilie timu unayoona ni bora,vidonda by tumbo na BP vya nini?
 
Nyie piganeni. Ilikuwa ni wishful thinking kwamba mtachukua ubingwa
Kwa timu ipi hasa?

Kila timu inajua mbinu za Kichuya na hamna plan B. Nani atoke na nani aingie kubadili matokeo? Hakuna?

Endeleeni kujenga timu lakini kiwe Kikosi kipana zaidi. Hilo Kombe la FA mpo kwa hisani ya TFF wanaojali mapato kuliko kanuni!
 
Acha mikwara uliahidi kumuondoa Aveva miaka 2 iliyopita hadi leo anadunda
 
Nafasi mlionayo ni moja tu , nayo ni kesho tu .
 
Back
Top Bottom