Awamu ya Tano na miradi ya maendeleo isiyo endelevu

Awamu ya Tano na miradi ya maendeleo isiyo endelevu

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Dunia na Ulimwengu unahitaji miradi endelevu ya maendeleo baada ya
mfumo wa miradii ya maendeleo kuonekana haina tija. (The world is focusing on Sustainable Development projects and programs not development projects). Kwanini miradi endelevu ya maendeleo?

1. Miradi endelevu lazima iwe shirikishi- moja ya hitajio la miradi shirikishi nikuwafanya wananchi na watumiaji wa mradi kuwa sehemu ya mradi na kujipa ile sense ya ownership (umiliki). Miradi mingi inayotekelezwa na awamu ya Tano siyo shirikishi katika ngazi ya siasa, kiserikali na jamii. Upo uwezekano miradi hii ikafa pale mwenye maono atakapoondoka madarakani.

2. Miradi endelevu ina sifa ya uwazi(Transparency). Miradi ya maendeleo ya awamu ya tano imejaa usiri mkubwa watu wakiaminishwa hata fedha za miradi hii ni fedha zetu za ndani huku ukweli ukiwa Ni kwamba tunakopa. Kukosekana kwa uwazi kunawafanya watawala watakaomrithi Magufuli kufanya kazi yakutukua makaburi Kama alivyofanya yeye. Kugukua makaburi kutapelekea tugombane na wakopeshaji wetu na waliotumika kukopa, taifa litaendelea kuishi kwa kufukua makaburi na kutuhumiana huku anayetuhumu akiwa mtuhumiwa ila tu mwenye sifa ya kushika mpini.

3. Miradi inayofanywa haikuzingatia taratibu za nchi- Ipo michakato imewekwa serikali inayoambatana na URASIMU, mfano taratibu za mikataba, manunuzi na upataji wakopeshaji na watekelezaji wa miradi. Urasimu uliowekwa kwenye serikali nyingi Duniani ililenga kuifanya serikali ifanye Jambo lililofanyiwa utafiti na likapita mikononi mwa watu wengi wenye taaluma tofauti ambao wataibua hoja zitakazopelekea kufanyika Jambo lenye maslahi mapana kwa Taifa. Awamu ya Tano kwa kiasi kikubwa imesukumwa na kuona matokeo ya miradi bila kuzingatia mlingano wa maslahi ya Taifa na miradi husika. Namna mradi unavyobuniwa, unavyopembuliwa hadi kuanza kutekelezwa kumekuwa na maelekezo mengi yanayofikia hata kuwatumbua wale wanaopingana na mawazo kutoka juu Jambo lililopoka Uhuru wa watoa maamuzi. Kimchakato mradi unaweza kuonekana umepita hatua zote ila kimantiki aliyeusukuma huo mchakato Ni aliyewateua watoa maamuzi.

4. Miradi endeleo haisukumwi na amri toka juu Wala maamuzi ya vyombo vya dola, miradi endelevu usukumwa na misingi ya sheria. Miradi yetu mingi imesukumwa na dola, nikawaida kabisa kumsikia Waziri aliyesoma economics akimshambulia na kumwondoa kwenye nafasi engineer bila hata kumpa nafasi yakujitetea kitaalam. Hi imewajengea hofu watumishi wa Umma na kuishi maisha ya Bora liende.

Hizi Ni baadhi ya hoja zinaifanya miradi ya maendeleo ya CCM kubaki na sifa ya miradi ya maendeleo na kupoteza sifa ya miradi ya maendeleo endelevu.
 
Magufuli aliwambia Wakurugenzi.

Nakupa Ajira.
Nakupa mshahara mzuri.
Nakupa Gari nzuri.
Nakupa posho.
Nakupa Nyumba .

Alafu wewe unakwenda kumyangaza mponzani.

HII NI KAULI YA KUTISHA SANA
 
MAMBO 27 YALIYOFANYWA NA SELIKALI YA MAGUFULI.

1. Hajatoa ajira miaka 5
2. Hajaongeza mishahara kwa miaka 5
3. Ameongeza makato HESLB toka 8% to 15%
4. Amefukuza wafanyakazi na hajawapa hata senti tano kisa vyeti feki
5. Kaondoa fao la kujitoa NSSF
6. Kaondoa wanunuzi binafsi wa kahawa waliokuwa wanatoa bei nzuri
7. Karudisha gharama za matibabu kwa watoto na wajawazito
8 .Anatoza maiti kodi kuzitoa mochwari
9. Kavunja katiba ya nchi kuzuia wapinzani kufanya mikutano halali ya siasa
10. Katunga sheria kandamizi kukomoa watu
11. Kabambikia kesi watu kwa visasi na chuki
12. Kafilisi wafanyabiashara kwa chuki binafsi
13. Kathibiti mashirika ya kutetea haki za binadamu
14. Kadhibiti na kutisha vyombo vya habari na kuviamrisha vimtangaze yeye tu na chama chake
15. Kavuruga sana mahusiano ya kimataifa
16. Kavuruga demokrasia na anataka wananchi waishi kama mifugo yake kufuata analotaka
17. Kazima bunge live na kulitumia bunge kama muhuri kufanya mambo yake
18. Mahakama imebinywa na imekuwa siyo huru tena
19. Kawadhibiti viongozi wa dini wanaomkosoa na kumwambia ukweli
20. Kanunua ndege bila kufuata sheria ya PPRA
21. Watu wengi wameuwawa na kupotea na kutekwa
22.Amelea na kulinda kikosi kazi cha "watu wasiojulikana"
23. Amepandikiza hofu,ukatili na dhuluma kama nyenzoza siasa mpya za Tanzania na utu umetoweka
24. Kakivuruga chama chake na kukimega vipande vipande
25. Kajenga uwanja wa ndege kwao bila ya approval ya bunge wala cabinet
26. Alisema tutaishi kama MASHETANI.. kwa madai kuwa tulikuwa tunaishi kama Malaika. Hakika amelitimiza hilo.🤔
27. Kuwa na kundi la watu wasiojulikana awamu hii ya tano na polisi hawajawai
 
Dunia na Ulimwengu unahitaji miradi endelevu ya maendeleo baada ya
mfumo wa miradii ya maendeleo kuonekana haina tija. (The world is focusing on Sustainable Development projects and programs not development projects). Kwanini miradi endelevu ya maendeleo?

1. Miradi endelevu lazima iwe shirikishi- moja ya hitajio la miradi shirikishi nikuwafanya wananchi na watumiaji wa mradi kuwa sehemu ya mradi na kujipa ile sense ya ownership (umiliki). Miradi mingi inayotekelezwa na awamu ya Tano siyo shirikishi katika ngazi ya siasa, kiserikali na jamii. Upo uwezekano miradi hii ikafa pale mwenye maono atakapoondoka madarakani.

2. Miradi endelevu ina sifa ya uwazi(Transparency). Miradi ya maendeleo ya awamu ya tano imejaa usiri mkubwa watu wakiaminishwa hata fedha za miradi hii ni fedha zetu za ndani huku ukweli ukiwa Ni kwamba tunakopa. Kukosekana kwa uwazi kunawafanya watawala watakaomrithi Magufuli kufanya kazi yakutukua makaburi Kama alivyofanya yeye. Kugukua makaburi kutapelekea tugombane na wakopeshaji wetu na waliotumika kukopa, taifa litaendelea kuishi kwa kufukua makaburi na kutuhumiana huku anayetuhumu akiwa mtuhumiwa ila tu mwenye sifa ya kushika mpini.

3. Miradi inayofanywa haikuzingatia taratibu za nchi- Ipo michakato imewekwa serikali inayoambatana na URASIMU, mfano taratibu za mikataba, manunuzi na upataji wakopeshaji na watekelezaji wa miradi. Urasimu uliowekwa kwenye serikali nyingi Duniani ililenga kuifanya serikali ifanye Jambo lililofanyiwa utafiti na likapita mikononi mwa watu wengi wenye taaluma tofauti ambao wataibua hoja zitakazopelekea kufanyika Jambo lenye maslahi mapana kwa Taifa. Awamu ya Tano kwa kiasi kikubwa imesukumwa na kuona matokeo ya miradi bila kuzingatia mlingano wa maslahi ya Taifa na miradi husika. Namna mradi unavyobuniwa, unavyopembuliwa hadi kuanza kutekelezwa kumekuwa na maelekezo mengi yanayofikia hata kuwatumbua wale wanaopingana na mawazo kutoka juu Jambo lililopoka Uhuru wa watoa maamuzi. Kimchakato mradi unaweza kuonekana umepita hatua zote ila kimantiki aliyeusukuma huo mchakato Ni aliyewateua watoa maamuzi.

4. Miradi endeleo haisukumwi na amri toka juu Wala maamuzi ya vyombo vya dola, miradi endelevu usukumwa na misingi ya sheria. Miradi yetu mingi imesukumwa na dola, nikawaida kabisa kumsikia Waziri aliyesoma economics akimshambulia na kumwondoa kwenye nafasi engineer bila hata kumpa nafasi yakujitetea kitaalam. Hi imewajengea hofu watumishi wa Umma na kuishi maisha ya Bora liende.

Hizi Ni baadhi ya hoja zinaifanya miradi ya maendeleo ya CCM kubaki na sifa ya miradi ya maendeleo na kupoteza sifa ya miradi ya maendeleo endelevu.
Elimu elimu elimu, kwa kweli watu hawaelewi maana ya "sustainable development au miradi endelevu kwa kiswahili "
Halafu miradi inayoshirikisha watu pia inategemeana na situation, u can not say kwamba ukitaka kujenga flyover kwa mfano ni jinsi gani utawashirikisha watu ili wakubaliane na serikali ??
Ni kwamba miradi yote au Mingi inayofanyika ni maamuzi ya viongozi, hata iwe ulaya etc.
Kuhusu sustainability or kuwa endelevu ni kwamba utaweza kujiendesha na kuleta matokeo chanya katika Maisha ya watu socially, na economically
 
Back
Top Bottom