Ayobami junior: HIFADHI hili jina kichwani

Ayobami junior: HIFADHI hili jina kichwani

makaveli10

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2013
Posts
31,583
Reaction score
92,670
Takribani miezi 10 ama 11 hivi nilikuwa sijagusa mpira, siku hiyo mwili wangu unatamani mpira kuliko chochote, hata ule mchezo wa mguu bara mguu pwani siutamani kama ambavyo nimeamka na tamaa ya kucheza mpira, akili yangu haiwazi mengine kikamilifu ni mpira tu, kila mara najiona kama uwanjani, nafanya vitu vyangu.
Hatimaye jioni ikafika nikachukua viatu vyangu, mie huyo mdogo mdogo uwanjani, njianj nikakutana na jamaa zangu wawili watatu na kunitania

Jamaa "mkongwe naona unaenda kufanya vitu vyako, tunakuja huko kuona burudani"
Mimi: burudani wapi mtaalamu, viungo vyenyewe vibovu, naenda KUZIPASHA SHAHAWA zangu.
Tukacheka, kila mmoja akaenda na njia yake.

Kufika mazoezini watu, wakanilaki kwa furaha, "fundi, fundi, fundi. Miezi 10 si midogo, nikaona sura ngeni kadhaa,
Madogo wakaanza kunitania, leo umekuja, umekutana na fundi mwenzio, haya ubishi wetu leo unaisha, wengine, aahh, huyu kajizeekea, wengine mara hivi mara vile,

Nikamuuliza dogo mmoja wanaongelea nini hawa, mmoja akaniambia kuna jamaa hapa, wanaijeria miongoni mwao kuna huyo fundi, watu wakasema kaziba pengo lako uwanjani, burudani yako yote inapatikana kwake, ndio kukawa kumegawanyika pande 2, wengine wanakubali, wengine wanasema kwenye ubora wako hajafikia,nikatabasamu nikavaa viatu vyangu, mdogo mdogo uwanjani.. Dogo mmoja akaniambia maestro, leo unachezea timu yangu.

Baada ya kupasha pasha, mpira ukawekwa kati, tukaanza kukipiga, piga sana mali dk kama 45 hivi nishapiga pasi zangu kama 50 hivi, nishafanya dribbling zangu za kibabe kadhaa, mmoja akaniita, mkongwe inatosha, naomba sub, uliyofanya yanatosha.. Nami pumzi zilikuwa zishaanza kukata, nikajisemea ngoja nami nikae nje, kumuona vizuri huyu mnaijeria anayeitwa fundi, aisee ni fundi kweli kweli, anajua sana boli, kuna mambo tunatofautiana, ila bado anakaa kwenye kundi la watu wanaojua boli.kabla ya mazoezi kuisha nikajiondokea zangu..

Kesho yake nikaenda tena ila nilijikuta nimewahi, wakati niko bize na simu, akaja jamaa mmoja akakaa pembeni yangu, akanisalimu, kuinua kichwa ndio yule mnaijeria, piga stori kadhaa, akaniambia anatamani angeniona miaka 10 nyuma nilikuwaje, naonekana naujua sana mpira, nikampa historia yangu kiufupi, wazazi hawakutaka nikomae na mpira ila nikomae na school, lakini isivyo bahati zaidi nilipokuwa najiiba kwenda kucheza, nikaishia kupata majeraha mabaya sana, goti na nyama za paja.. Hivyo mpirani sina historia kubwa ya kutamba, hapo ndio ikawa mwanzo wa urafiki wetu na huyu fundi, nikaja kumjua zaidi baadae kadri tulivyozidi kuzoeana.

Jamaa anaitw ayobami junior, wenzake wanamuita BAGGIO, ni mnaijeria aliyepata kucheza kano pillars, kwara united na shooting stars, kacheza u23, alishindwa kucheza CHAN sababu ya kutokuelewana na manager wa timu.
YouTube ana video nyingi sana, nyingine mashabiki wanalalamika kwanini kaachwa timu ya taifa ya wachezaji wa ndani.

Jamaa ni fundi mnoo, kosa alilofanya ni kuja kichwa kichwa, ila naamini dirisha hili dogo anaweza kupata timu...
Kilichomponza ni ile hamu ya kucheza nje ya ligi yao, viongozi wa timu yake shooting stars, hawaachi kumpigia simu arudi, ila mwenyewe anakuambia alishajiapiza mkataba ukiisha yeye na ligi ya naijeria ndio wamemalizana, hataki kabisa kucheza ligi ya kwao, bahati mbaya zaidi akakutana na wakala kanjanja, mgeni kwenye game, bongo hana connection ya kutosha, hivyo anataabika kupata timu.
Siku 1 kaja home tunatizama game ya Dodoma jiji sijui na pamba wale, ghafla namuona mtu kainuka kwa furaha kubwa, kaenda mpaka kwenye tv, namuuliza vipi akanionesha mchezaji wa Dodoma jiji, akaniambia huyu ni ematah, nimecheza nae ligi ya nyumbani, hawa mie nikicheza wao wanapiva salute, akaniambia inshaallah ni dalili njema kwake, kidogo akamuona jamaa anaitwa obata, akaniambia wamecheza timu moja.

Akaanza kusaka namba zao, akapata ya john noble, wote hawaamini kama yupo bongo, noble akamwambia the only mistake kafanya ni kuja Bongo bila timu, ni ngumu timu za huku kumthamini, ila asijali atacheza kwa kiwango chake, ila hatoipata thamani yake kwa haraka, wenzake kina ematah wamekuja bongo tayari wana connection, wamesha sign pre contract.

Kama jamaa atapata timu dirisha dogo na asizuzuke na wadada wa mjini basi katika ligi yetu kuna burudani imeongezeka.



 
Nigerians wanajilipua balaa, imagine mtu katoka kwao hana connection yoyote aisee then anakuja kuona washikaji wake kwenye luninga.
But nadhani wanasukumwa zaidi na uhakika wa kile anachokijua vyema, iwe mpira au katika nyanja zingine za maisha kama elimu nk. Kongore kwao
 
Mpeleke timu za mikoani akaanzie huko kisha uwezo wake utampeleka mjini.
1.Mashujaa
2. Pamba jiji
3.Costal union
4.KenGold
5. Fountain gate
6.Kagera sugar
Na zinginezo.
 
Nigerians wanajilipua balaa, imagine mtu katoka kwao hana connection yoyote aisee then anakuja kuona washikaji wake kwenye luninga.
But nadhani wanasukumwa zaidi na uhakika wa kile anachokijua vyema, iwe mpira au katika nyanja zingine za maisha kama elimu nk. Kongore kwao
Jamaa kwao kusafiri ni rahisi na hamasa wanayo kubwa tofauti na sisi hapa mpaka unazeeka haujawahi kuvuka mpaka wowote!
 
Natamani kungekua na namna asaidiwe apate timu, wa hivyo wanakuaga na hasira sana mana wanaanzia chini kabisa.
Akipata nafasi, watu wa burudani ya mpira wataongezeka kwenye ligi yetu, jamaa ana IQ fulani ya mpira unaenjoy kumtizama, kwanza ni bingwa wa kuscan, shingo haitulii uwanjani.
 
Nigerians wanajilipua balaa, imagine mtu katoka kwao hana connection yoyote aisee then anakuja kuona washikaji wake kwenye luninga.
But nadhani wanasukumwa zaidi na uhakika wa kile anachokijua vyema, iwe mpira au katika nyanja zingine za maisha kama elimu nk. Kongore kwao
Hawa mabwana lazima wapambane, kule kwao watu wengi saana halafu viongozi wanakula zaidi.

Ni wapambanaji haswa, kama sikosei akpan alivyokuja simba walimtosa hakukata tamaa, akaenda zanzibar, akaja ibukia coastal akaja simba.

Jamaa hajakata tamaa, kwanza anaona aibu kurudi kwao, japo viongozi wa shooting stars wanampigia simu arudi watamuongeza na mshahara, ila hiyo haipo akilini mwake.
Yeye anaamini hata championship ataanzia,
Nimeenda nae kwenye ndondo kadhaa hakuna ndondo nimefika watu wasishangae uwezo wa mshikaji
 
Mpeleke timu za mikoani akaanzie huko kisha uwezo wake utampeleka mjini.
1.Mashujaa
2. Pamba jiji
3.Costal union
4.KenGold
5. Fountain gate
6.Kagera sugar
Na zinginezo.
Soka letu lina changamoto, kuna vitu ukisogea ndio unajia kwanini wakati mwingine tunasajili sawadogo na uwezo unaonekana kabisa mbovu.

Siwezi ongelea saana maana haitapemdeza lakini tulijaribu timu fulani ya mkoa, kocha mkuu akampenda ila akataka milioni 3 kwanza ili apitishe jina. Na hiyo hkuficha aliweka wazi kabisa, huyu ni mzuri lakini aweke 3 ili ampitishe, ikashindika.. Tumlipe baada ya kusaini kagoma.
 
Jamaa kwao kusafiri ni rahisi na hamasa wanayo kubwa tofauti na sisi hapa mpaka unazeeka haujawahi kuvuka mpaka wowote!
Nadhani wingi wao, inabidi wafosi, na sisi tulisafikia watu miliomi 200+ itabidi tuwe tunajiripua tu.
 
Soka letu lina changamoto, kuna vitu ukisogea ndio unajia kwanini wakati mwingine tunasajili sawadogo na uwezo unaonekana kabisa mbovu.

Siwezi ongelea saana maana haitapemdeza lakini tulijaribu timu fulani ya mkoa, kocha mkuu akampenda ila akataka milioni 3 kwanza ili apitishe jina. Na hiyo hkuficha aliweka wazi kabisa, huyu ni mzuri lakini aweke 3 ili ampitishe, ikashindika.. Tumlipe baada ya kusaini kagoma.
Too sad, yaani imagine kocha ndo anataka 3 millioni kupata mtu ambaye ana uwezo na anaweza kupandisha CV ya huyo kocha kama mchezaji akiisaidia tumu kufanya vizuri
 
Too sad, yaani imagine kocha ndo anataka 3 millioni kupata mtu ambaye ana uwezo na anaweza kupandisha CV ya huyo kocha kama mchezaji akiisaidia tumu kufanya vizuri
Nilichoka sana

Can you imagine, za chini chini ile hela ni yeye na baadhi ya viongozi.
Kuna tetesi zilimfikia CEO bwana kuna mafundi wanaujua sana hapa, ikapangwa mechi ya kirafiki siku ya j4 ili CEO aje kuwaona, kwa taarifa hizo siki ya j2 usiku viongozi wakaja, wakawaambia majamaa kuwa hiyo ndio mwisho kuanzia j3 hawapaswi kuwepo mazoezini, ikabidi waondoke, siku ya game sijui kama walitafuta watu wa kuwapachika ama walimjibu nini CEO wao.

Baadae kabisa kocha akaja kusema, viongozi ndio wametia ugumi, wana wachezaji wao.
Sisi hatutaka kujua ukweli wa maneno yake, kikubwa ndio ishabuma tena.
 
Moyo unanituma kufanya kitu kwa Ayobami JR Ila sijui nianzie wapi Ila sijaangalia hata vedio yake moja Ila maneno yako yamenijaza upepo na huruma juu yake hasa vile nawaona vijana Wana viapji Ila wameishia mtaani tu .

Sasa muone jamaa kafunga safari kutoka nchi za mbali yupo bongo anacheza ndondo na uwezo anao Ila wanamzingua eti hela kwanza 😭😭

Kaka ikiwa Kuna timu manager atamkubali na akasema ili jamaa aweze kucheza inatakiwa amlipe ndiyo amsajili nitakuwa tayari kulipa hiyo hela chini ya maandishi ya Mimi na huyo meneja kikubwa Ayabamoh JR aende mbele .
 
Back
Top Bottom