Mkurugenzi wa TBC anamuongelea Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, marehemu Benjamin Mkapa, katika sekta ya habari anasema alikuwa mtendaji mahiri aliyependa umakini kitu ambacho TBC wamekuwa wakisisitiza mpaka sasa kitu ambacho Mkapa alikisimamia wakati akiwa mhariri.
Pia ameongelea Mkapa akiwa Rais, amesema kuna watu wanazungumza kuwa Mkapa alikuwa hapendi waandishi wa habari kitu ambacho sio kweli kwani alikuwa hapendi waandishi wa habari wavivu, wasio na umakini kwani unaweza kumkuta muandishi wa habari anaandika anakosoa tu lakini yeye mwenyewe hana maarifa au hajui kinachoendelea kiasi impe uhalali wa kukosoa wengine.
Amesema kukosoa ni jambo zuri lakini mwingine anakosoa huku lugha yake haina ufasaha vinginevyo Mkapa alikuwa anapenda uje na hoja zako hakuna haja ya kutukanana.
Pia ameongelea Mkapa akiwa Rais, amesema kuna watu wanazungumza kuwa Mkapa alikuwa hapendi waandishi wa habari kitu ambacho sio kweli kwani alikuwa hapendi waandishi wa habari wavivu, wasio na umakini kwani unaweza kumkuta muandishi wa habari anaandika anakosoa tu lakini yeye mwenyewe hana maarifa au hajui kinachoendelea kiasi impe uhalali wa kukosoa wengine.
Amesema kukosoa ni jambo zuri lakini mwingine anakosoa huku lugha yake haina ufasaha vinginevyo Mkapa alikuwa anapenda uje na hoja zako hakuna haja ya kutukanana.