Azam Confederation Cup, Yanga VS Coastal Union 24:04:2016

Mnataka haki hameni nchi mbona Jecha alitangaza matokeo na mpaka sasa hali imetulia hakuna cha vulugu hii ndo Tz bwana
 
Mi huwa nawaambia kila siku kushabikia mpira wa Tz ni upuuzi wa kiwango cha juu,huyo Malinzi alishawahi hata kuongoza mpira shuleni? mtu kaja tu from no where anapewa uongozi wa mpira. Tutamkumbuka sana Wambura alihujumiwa vya kutosha!!
 
Tunaposema Yanga inaua mpira wa bongo.Huwa tunamaanisha.
Sio Yanga tu hata Simba na kwa mbaali naiona Azamu nayo inaingia kwe mkumbo ule ule...........ngoja niendelee kukomaa na ligi ya Uingereza kwa wanaojua mpira!!!
 
Kibendera aliechezesha game ya Yanga ni halali yake kupigwa jiwe la kichwa anaonyesha mapenzi ya waziwazi kabisa kwa Yanga ndomana TFF wanajishushia heshima kadri siku zinavyoenda mana wanachukua waamuzi ambao hawana uwezo wa kuchezesha nusu fainali wanasababisha mpaka mechi inaishia njiani..
 
mimi ni mfuasi wa Yanga. sijaona maamuzi yoyote ya kuashiria eti Yanga imebebwa. huo ni ulalamishi wa kike (ingawa nawaheshimu sana wanawake).

lakini, on the balance of play over 90 minutes, Coastal walistahili ushindi. wamecheza mpira mkubwa kuliko Yanga....isipokuwa hawakuwa na mipango mizuri kwenye final third. nadhani Yanga bado wana uchovu wa lile valangati la kule Egypt.

so....for the sake of football, Coastal walistahili kushinda, and as a Yanga fan I wouldn't have complained too much because a better team ndiyo ingekuwa imeshinda!
 
Mchezaji ambaye si gollkeeper anaruhusiwa kucheza mpira kwa mkono,au wanaposema kubebwa unafikiri wenzako wanalalamikia nini...Straight red card kwa Oscar Joshua kwa rafu mbaya ambapo ilitolewa yellow card tu.
 
Mchezaji ambaye si gollkeeper anaruhusiwa kucheza mpira kwa mkono,au wanaposema kubebwa unafikiri wenzako wanalalamikia nini...Straight red card kwa Oscar Joshua kwa rafu mbaya ambapo ilitolewa yellow card tu.
perception & perspective, chief....
 
mie nakiri wazi yanga haikucheza vizuri na red card aliyopewa adyungi ni halali ,yy Alidhani ni basketball ile
 
Yaaani nyie wa mchangani mnashida sana..yaani mnaiombea mabaya Yanga as if mnaghalimika chochote na ushindi wake
 
Hivi yanga wamecheza na wamatopeni mikia mirefuuu kapakatwa maana ndio wanaongoza kulalama
 
Ifikie wakati sasa marefa waache mahaba....wachezeshe pambano kwa kufuata sheria za soka na sio kwa maagizo ya ngazi za juu....

Ni aibu kwa mwamuzi kuingia na matokeo mfukoni kama alivyofanya yule mwenyekiti........

Hali hii inashusha morali ya wachezaji katika ligi...kwani wanajua wazi kuwa wao hawastahili kuwa mabingwa na bingwa ameshapangwa......

Naishauri TFF msimu ujao wa ligi wasihangaike kupanga ratiba ndefu za ligi hali ya kuwa wameshamjua bingwa kabla hata ligi haijaanza....

Hizo pesa za wadhamini waandae sherehe za kumkabidhi ubingwa Yanga.......

Wasitupotezee muda wa kukaa kuangalia mpira huku wao wanamjua bingwa....
 
Mwaka huu mikia watasema sana.

Goli la Ngoma lilikuwa safi kabisa, hamna offside hapo.

Ni kweli Oscar alistahili straight red card lakini haibadili matokeo ya mchezo. Coastal waliingia uwanjani wakiamnini lazima washinde. Sijui jeuri hiyo wanaipata wapi ukiangalia nafasi yao kwenye msimamo wa ligi. No Coastal huyo huyo aliyepigwa nane bila wakiwa chini ya Julio.
 
Nani mwenye jina/majina ya mwamuzi yeyote kutoka Tanzania aliyechezesha mashindano yoyote ya CAF au FIFA kama mwamuzi wa kati ikiwa match kubwa au ndogo.
 
na coastal hao hao waliwapiga yanga mbili bila
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…