Uongozi wa Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati AZAM FC Leo Limesimamisha Benchi zima la ufundi la Timu hiyo linaloongozwa na Kocha mkuu Mhispania Zeben Hernandez kutokana na Mwenendo mbovu wa Timu
source AZAM TWO
My Take: Ni jambo zuri Kwani kwa Uwekezaji ule Haiwezekani Wapinzani wetu wawe Stendi, Majimaji, Mbao nk.
Nafikiri sasa Watumie Mechi za Mapinduzi kama Pre-Season kwa ajili ya FA ili kumantain Uwakilishi wa Kimataifa, Ligi kuu kwa sasa ni kama Tumechelewa
=====
Azam FC imemtimua Kocha wake Mkuu, Zeben Hernandez Zeben na makocha wengine raia wa Hispania, wametimuliwa kazi leo baada ya Azam FC kwenda mwendo wa kusuasua.
Azam FC iko katika nafasi ya nne ikiwa na pointi 27 baada ya kucheza mechi 17.
Katika mechi 17 za Ligi Kuu Bara, Azam FC imechinda mechi saba, imepoteza nne na sare sita, hali ambayo wazi inaonekana kutoufurahisha uongozi wa Azam FC hata kidogo.