Azam fc,wamekosea wapi?

Jitu Refu

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2016
Posts
823
Reaction score
811
Azam fc ilipoanzishwa nilijua itakuja kuwa kilabu bora sana afrika kama TP MAZEMBE na nyinginezo zilizofanikiwa,kwa kuwa azam fc wana boss(bakhresa) mpenda mpira na anapesa ya kutosha,nini kimewafanya wawe na uwezo kama wa simba na yanga(timu zinazoongozwa na wanachama) tu tena muda mwingine hizi timu zinaizidi azam fc(kiuwezo uwanjani).Au walichokosea ni kuingiza uyanga baada ya kumnunua mshabiki kutoka yanga(hapa natania),wamekosea wapi hawa?

Je?,unazani SIMBA na YANGA wataweza kufanikiwa zaidi ya hapo walipo wakiingia kwenye mfumo wa timu kumilikiwa na mtu mmoja au kampuni.
 
Inaanza mimba alafu unazaliwa ndio hatua nyingine za ukuaji zinafata,nadhani Azam ndio wanaanza kunyonya bado wana safari ndefu mpira ni zaidi ya mahela kuna kujenga utamaduni wa timu kitu ambacho kinahitaji muda.
 
 
Tatizo la Azam fc kujifanya wao ni simba b kwa hiyo laana ya mafisango mwaka huu imehamia simba b na sidhani kama ipo siku azam watakuwa kama tp mazembe
 
Wachezaji situkonao huku kitaa Choka mbaya hata elfu kumi inawapiga chenga
Ina maana boss wao kaona timu inaweza kumpeleka pabaya kaanza kubania pesa,au lengo lake lilikuwa n kuwa na timu ligi kuu basi hana mpango wa kuendelea zaidi
 
Kichuya ... Ila ndala fc msibweteke anaweza akawatwanga
 
Kocha mhispaniola mafundisho yake hayaeleweki nini?.. Lakini wanahitaji muda,mpira ni uwekezaji wa muda mrefu sana.
 
Ina maana boss wao kaona timu inaweza kumpeleka pabaya kaanza kubania pesa,au lengo lake lilikuwa n kuwa na timu ligi kuu basi hana mpango wa kuendelea zaidi
Huwezi ukaleta jopo la ufundi kutoka Hispania halafu useme hana nia...pamoja na uwekezaji wote huo...
 
Kinachokiua Azzam fc ni utawala watu wamewekwa kwa kujuana tu na sio taaluma
 
Tatizo la Azam fc kujifanya wao ni simba b kwa hiyo laana ya mafisango mwaka huu imehamia simba b na sidhani kama ipo siku azam watakuwa kama tp mazembe
Na hata Toto Africa ambayo ni Yanga B sidhani kama kuna siku watakuwa kama Tp Mazembe

Bila shaka wanalaana...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…