Upo sahihi, Mimi Kuna miaka ya hivi karibuni niliwahi kuwa na ushabiki kupitiliza ,
Basi Kuna mwanangu mmoja huwa tunaenda wote kutazama mpira kwenye Banda umiza, basi Mimi Yanga yeye Simba.
Basi mechi iliisha Simba kuibuka na ushindi wa goli tano , Emanuel Okwi akiwa kwenye kiwango bora.
Baada ya mechi kuisha nilienda kwenye gari nikaingia mchizi naye anataka kuzama kwenye gari kwakuwa tuliishi mtaa mmoja,hivyo anataka turudi wote kama tulivyokuja nikamzuia, nikamwambie aachane na Mimi na atafute usafiri mwingine.
Nimekasirika, nimefura ile mbaya.
Mchizi alishangaa sana, lakini Mimi nikakanyaga mafuta nikaishia,
Lakini usiku wa siku hiyo siku na amani kwa kitendo nilichomfanyia mchizi wangu, nilijuta sana, asubuhi nilienda kazini kiunyonge na nikijaribu kumpigia simu anakata, nikaamua kumuibukia nyumbani kwake, nakumbuka licha ya kujieleza na kuomba msamaha sana, lakini akawa mgumu , nikatumia busara nyingi sana hatimaye tukarudisha urafiki wetu, tangu hapo hii mipira nashabikia juujuu tu.