Azam Marine mambo shingoni. Zanzibar one na two mambo byeeee



Kilimanjaro zina stabilizer system sema sio za kisasa kama zilivyo Zanzibar 1.

Boat ambazo hazikua nazo ni Kilimanjaro 1 & 2, zile alizoziuza. Kilimanjaro 3 na 4 ziliwekewa huku tayari zikiwa zipo kazini. 5, 6 na 7 zimewekewa tokea kiwandani ila ni kutuliza boat wakati wa mawimbi. Lakini haya maelezo ni kwa mujib wa Chief Engineer Victor.


Ila kusema kweli ukipanda Zanzibar 1 kitu kimetulia kama ndege, ukichanganya na injini kuwa jet ndio kabisaaa full tambarare.
 
Huyu Chief Engineer ni yule jamaa anayevaa miwani nyeusi anatumia Jeep au pikipiki ya KTM.
 
Mkuu samahani kwa usumbufu, je bei ya boti kama ya azam au zanzibar1 ni kiasi gani?
Mkuu bei sahihi sijui maana hizo zimetengenezwa kwa oda.
Taarifa sahihi za bei tungepata kutoka kwa hizo kampuni pale wanapozileta ila kwa Tanzania zinakuwa siri.

Hapo ili tujue bei sahihi tusipige ramli inabidi tuwaulize watengenezaji kwa email ambayo ni Coco yatch au Richardson Devine Marine wazungu wako punctually lazima wakupe bei wanajua unaweza ukawa mteja.
 
Mkuu samahani kwa usumbufu, je bei ya boti kama ya azam au zanzibar1 ni kiasi gani?
Ukitaka zilizotumika kuna minada ya boti huko America, ulaya na Japan hizo catamaran boat za saizi hiyo uanzie na 7billion hapo ujapita TRA,kuisafirisha na kuisajili huku nchini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…