AZAM MEDIA ongezeni idadi ya Camera mnazotumia kunasa matukio ya mechi katika ligi kuu ya NBC

AZAM MEDIA ongezeni idadi ya Camera mnazotumia kunasa matukio ya mechi katika ligi kuu ya NBC

Tipstipstor

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2021
Posts
1,528
Reaction score
3,352
Nawapongeza kampuni ya Azam media kwa kuonesha mechi za ligi kuu NBC live, kitendo ambacho kimeipa hadhi ligi yetu si tu Africa ya mashariki bali Africa nzima.

Wito wangu kwa wamiliki wa Azam media ni kuwa ongezeni idadi ya Camera katika production team yenu ili muweze kunasa matukio takribani yote uwanjani.Ligi ya EPL ni bora ulimwenguni kutokana na production quality yao, wanatumia zaidi ya camera 30 uwanjani kunasa matukio yote ndani ya uwanja , pembezoni na pia kwa mashabiki jukwaani ila huku kwetu kamera zinazotumika hazizidi 3. Kamera moja tu ya jukwaa kuu ndio inatumika kunasa zaidi ya asilimia 80 ya matukio yote ndani ya uwanja.

Kitendo ambacho kinapelekea baadhi ya matukio muhimu kushindwa kuoneshwa kwa wakati mfano replays za offside kwenu zimekuwa tatizo, inaweza kutokea mchezaji kampiga mwenzake kiwiko wakati hana mpira na bado mkashindwa kuonesha tukio. Juzi wachezaji wa mbeya kwanza walileta fujo baada ya simba kupata goli na bado mlishindwa kunasa tukio, kuna kipindi wachezaji wanacheza tackiling mbaya zinazoweza kuhatarisha maisha ya soka ya mchezaji mwenzake ila mmekuwa hamnasi matukio kutokana na idadi ndogo ya camera mlizonazo.

Yusuph,Abubakar,Omar na mzee wenu bakhresa nawashauri muwapeleke uingereza,spain au ujerumani baadhi ya wafanyakazi wenu wa Azam media waende kujifunza mambo muhimu katika production. Bado mpo local sana.

Mwisho katika watangazaji wa mechi, jaribuni kuongeza mchambuzi wa mechi ili aweze kutafsiri baadhi ya sheria na matukio yanayotokea uwanjani. Watangazaji wenu kama Baraka mpenja, Hashim Ibwe, Iddi salum kidedea wanajua kuhype mechi ila sio wachambuzi wa mpira. Igeni mfano wa TBC walivyokuwa wakitumia combination ya Jesse John na Hayati Mwalim kashasha. Jesse anatangaza ili ikifika sehemu inayohitaji technical explaination anamwachia mwalim kashasha afafanue.

Ni hayo tu kwa leo.
 
Kuuzwa kiasi gani haijalishi , tunalipa pesa ya ving'amuzi kila mwezi kwa ajili ya mpira anachotakiwa yeye ni kuongeza ufanisi ktk production
 
Kusema camera hazizidi 3 napinga.

1. Kuna kamera 1 inayochukua uwanja wote.

2. Kuna camera 1 kila nyuma ya goal (yaani 2).

3. Kuna camera 1 inayotembea tembea hapa chini karibu na benchi, kuna muda inafika hadi kwenye corner.

4. Kuna kamera ambayo haihami (ile ambayo camera man anakaa).

5. Kuna camera upande wa pili inayochukua kwenye benchi

KWA HIYO KAMA CAMERA 5 AU 6 HIVI INGAWA KWA KWELI HAZITOSHI KWA UWINGI WA MATUKIO YA UWANJANI
 
Azam wanajitahidi sana, nilikua naona Dstv anavyorusha afcon nikasema kumbe azam ni babu kubwa.
 
azam amejitautisha kdg sana na mtangulizi wake startv.bado kazi anayo.
kamera zake zimetegwa uelekeo mmoja..mpira ukihamishwa ghafla upande wa pili wachezaji huonekana wadogowadogo.Drones ndio soln baas
 
Kusema camera hazizidi 3 napinga.

1. Kuna kamera 1 inayochukua uwanja wote.

2. Kuna camera 1 kila nyuma ya goal (yaani 2).

3. Kuna camera 1 inayotembea tembea hapa chini karibu na benchi, kuna muda inafika hadi kwenye corner.

4. Kuna kamera ambayo haihami (ile ambayo camera man anakaa).

5. Kuna camera upande wa pili inayochukua kwenye benchi

KWA HIYO KAMA CAMERA 5 AU 6 HIVI INGAWA KWA KWELI HAZITOSHI KWA UWINGI WA MATUKIO YA UWANJANI
TUkio lenye utata lililopelekea Simba kupewa Penalty mechi za mwishon hapa lilionwa na kamera moja tu, na Kamera hiyo nayo haikuona vizuri hivyo mpaka leo bado ni utata

Hiyo ya Nyuma ya goli ingeweza kutatua huu utata but pengine ilikua imeelekea kwengine.
 
Nawapongeza kampuni ya Azam media kwa kuonesha mechi za ligi kuu NBC live, kitendo ambacho kimeipa hadhi ligi yetu si tu Africa ya mashariki bali Africa nzima.

Wito wangu kwa wamiliki wa Azam media ni kuwa ongezeni idadi ya Camera katika production team yenu ili muweze kunasa matukio takribani yote uwanjani.Ligi ya EPL ni bora ulimwenguni kutokana na production quality yao, wanatumia zaidi ya camera 30 uwanjani kunasa matukio yote ndani ya uwanja , pembezoni na pia kwa mashabiki jukwaani ila huku kwetu kamera zinazotumika hazizidi 3. Kamera moja tu ya jukwaa kuu ndio inatumika kunasa zaidi ya asilimia 80 ya matukio yote ndani ya uwanja.

Kitendo ambacho kinapelekea baadhi ya matukio muhimu kushindwa kuoneshwa kwa wakati mfano replays za offside kwenu zimekuwa tatizo, inaweza kutokea mchezaji kampiga mwenzake kiwiko wakati hana mpira na bado mkashindwa kuonesha tukio. Juzi wachezaji wa mbeya kwanza walileta fujo baada ya simba kupata goli na bado mlishindwa kunasa tukio, kuna kipindi wachezaji wanacheza tackiling mbaya zinazoweza kuhatarisha maisha ya soka ya mchezaji mwenzake ila mmekuwa hamnasi matukio kutokana na idadi ndogo ya camera mlizonazo.

Yusuph,Abubakar,Omar na mzee wenu bakhresa nawashauri muwapeleke uingereza,spain au ujerumani baadhi ya wafanyakazi wenu wa Azam media waende kujifunza mambo muhimu katika production. Bado mpo local sana.

Mwisho katika watangazaji wa mechi, jaribuni kuongeza mchambuzi wa mechi ili aweze kutafsiri baadhi ya sheria na matukio yanayotokea uwanjani. Watangazaji wenu kama Baraka mpenja, Hashim Ibwe, Iddi salum kidedea wanajua kuhype mechi ila sio wachambuzi wa mpira. Igeni mfano wa TBC walivyokuwa wakitumia combination ya Jesse John na Hayati Mwalim kashasha. Jesse anatangaza ili ikifika sehemu inayohitaji technical explaination anamwachia mwalim kashasha afafanue.

Ni hayo tu kwa leo.
Kweli Mkuu
 
Back
Top Bottom