Mfikirishi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 8,939
- 10,403
TBC wakitangaza inatosha!Nimeangalia headlines ya Azam leo tarehe 25 Julai 2024 kwenye UTV ambapo leo kulikuwa na issue kubwa ya RAIS kuadhimisha siku ya Mashujaa, habari hiyo haikuwa kwenye headline.
Kulikuwa na Treni ya kisasa ya Umeme ya SGR kufanya safari yake kutoka Dar hadi Dodoma lakini habari hiyo haikuwa kwenye Headline ya UTV ya Azam.
Azam hawapendi haya maendeleo yanayofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suhulu Hassan? Mbona ITV wamefanya coverage japo kwa muda mchache?
UTV inaonekana vizuri sana ila habari zao hazioneshi matukio makubwa. Editor ajitazame.
Ila UKWELI natamani siku itokee media ya kuhoji na kuchambua miradi ya ccm ili tuone kama Ina "value for money"!
Na ashirikishwe Luhaga Mpina katika chambuzi hizo!