Azam TV boresheni kamera zenu

Azam TV boresheni kamera zenu

Hakuna camera yoyote ya Azam inayoonesha tukio la video kwa namna hiyo. Hizo ni picha mgando zinazosambazwa na mashabiki mitandaoni. Baada ya kuona kuona hii picha yako ilinifanya niingie youtube pengine nitakutana na mgusano wa namna hiyo ili nijiridhishe kuwa kuna mgusano ila cha ajabu nakuta mtu kaweka caption ya video ya namna hiyo halafu ukija ku play ili uone. Unakuta video haioneshi kama alivyoiweka caption ya picha mnato. Kama uamini basi tafuta hiyo video halafu inaonesha tukio kama ilivyo kwenye hiyo picha ilivyoonesha iweke hapa hiyo video. Utatafuta hauwezi kuipata video ya hiyo picha iliyopostiwa hapo.

Kuna mapungufu kwa upande wa camera za Azam hilo lipo wazi kuna utata mwingine wa offside inatakiwa uamuliwe kwa camera za angle tofauti tofauti lakini pia wanaokataa mchezaji hawezi kudondoka mwenyewe basi sio wafuatiliaji wa mipira. Mchezaji anaweza kuruka juu kisha akarudi chini vibaya. Sijasema kama Kapombe hakuchezewa faulo au lah. Ila nachoona kwenye replay zote ni kwamba hakuna physical contact baina yao na wameachana kwa umbali
Inawezekanaje mtu akaruka juu alafu akabadili muelekeo akiwa angani na kuangukia mita kadhaa mbele bila kusukumwa? .. inaingia akilini kweli ?
 
Inawezekanaje mtu akaruka juu alafu akabadili muelekeo akiwa angani na kuangukia mita kadhaa mbele bila kusukumwa? .. inaingia akilini kweli ?
Iwe kweli ama uongo,
Jana simba imecheza vibaya, coach alimuongeza mzamiru na nyoni team ipate balance katikati ndo kwanza waliendelea kupwaya,
Onyango jana aliku hovyoo saana.
Kama Simba wanataka kurudi kwenye kiwango ni wakati sasa wa kuwaacha Erasto Nyoni, Bocco, Mzamiru,Onyango, Wawa,Gadiel,Ajibu,
Kapombe asiwe wa kutegemea atafutiwe mbadala mwenye uwezo mkubwa,
Apatikane na striker mzuri nje ya hapo tutajifariji ila hao wachezaji viwango vyao vimegota.
 
Inawezekanaje mtu akaruka juu alafu akabadili muelekeo akiwa angani na kuangukia mita kadhaa mbele bila kusukumwa? .. inaingia akilini kweli ?
Tuanzie hapa kwenye huko kubadili muelekeo vs kudondoka. Kapombe wakati anataka kuruka kichwa je alikuwa katika uelekeo upi na je baadae baada ya kudondoka akabadili uelekeo kutoka upande upi kwenda upi? Naomba nijibu kwa kulingana na ulivyoweza kuona kwenye video na sio kwa hisia zako
 
Binafsi nilivyoona ni kwamba camera haikuonyesha tukio zima, camera zimeanza kunasa baada ya kuruka na si kabla.
Ni wazi kwamba Kapombe alisukumwa, hakuna namna mtu anaweza kuruka juu kutoka point A na kwenda kuangukia point B.

For me, it’s a clear foul.
Siyo wewe hata mimi naungana na wewe! It's a clear foul
 
Kapombe alikosea timing akawahi kuruka hivyo alivyoona amepotea akamua kujiangusha...mwenzake alikua na timing nzuri akaupata mpira na kuuingiza nyavuni
 
simba wanaifanya ligi hii ya nbc ionekane ndiyo 'most corrupted league' kwenye sayari hii, alafu ile taasisi ya kupambana na rushwa sijui inafanyaga kazi ganii??
Ile taasisi sijawahi kuiamini yaani hata sikumoja haijawahi kamata hata trafiki mmoja barabarani!
 
Kwani Fei toto kwa namungo alifanyeje? Vitu vinavouwa mpira wa bongo ni vitatu (1)TFF (2)SIMBA (3)YANGA ukiwadhibiti hao kutakuwa soka bora na ni kitu hakiwezekani.
Hizi ni kauli za kizamani sana. Biashara, Namungo, Azam, Mtibwa na wengineo walishapata nafasi za kimataifa..iliwafaa nini.

Tuache kulaumu. Hizi timu zinafaida kubwa sana katika ligi na soka letu kuliko hizo maneno.

Ndiyo timu pekee pia zinazowapa mapato mengi timu zingine za mikoani huko.
 
Back
Top Bottom