Azam yampokea Mpiana, Mapengo ya nyota hawa bado yawatesa

kinje ketile

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2015
Posts
5,089
Reaction score
9,664
Azam imempokea Mpiana Moziz kutoka FC Lupopo kuziba pengo la mcameroon Thiery Akono aliyeuzwa Malaysia. Imefanya mapokezi yasiyokuwa na 'mbwembwe'.

Wakati ikiendelea kujiimarisha Azam imeshindwa kabisa kuziba mapengo ya Bocco, Manula, Nyoni, Wawa na Kapombe na hivyo sasa imekuwa timu mshiriki zaidi kuliko mshindani wa vikombe katika miaka ya karibuni.

Ipo haja ya wao kujitathmini zaidi! Wakati huo huo wachezaji hao hao walioacha mapengo Azam ndio wamekuwa na mchango mkubwa kwa S.S.C. Kwa vilabu vya Afrika Mashariki na kati, ndio timu inayoongoza kwa ubora kwa mujibu wa CAF!
 
Ulichoongea kina uhalisia kwa kiasi fulani mkuu.

Lakini je umeshawahi kujiuliza kuwa wachezaji hao wamekaa Azam misimu mingapi na wamechukua ligi mara ngapi?

Unajua wakati Yanga anachukua VPL mara tatu mfululizo hao wachezaji wote bado walikua Azam?

Kuna kitu Simba imekifanya zaidi ya kuwasajili hao wachezaji waliokuwa wa Azam

Mi naona kuna kitu zaidi ya wachezaji na makocha kinachoila Azam, inabidi wajitafute sana.
 
Kwanza ni lazima kupata replacement yenye viwango vile vile au bora zaidi ya wachezaji walioacha pengo? Je Azam wanafanya hivyo? Au wanasajili kwa mihemko!

Pili Kuhakikisha wachezaji wanapata 'malezi bora' na tatu wajue nini thamani ya AZAM yaani ku deal na attitude/pyschology. Yaani wachezaji wajue Azam sio 'mshiriki mzuri tu' kwenye shindano lolote bali mpigania KOMBE. Kombe tamu jamani!
 
Tatizo linaloitafuna Azam, ni kwamba imeamua na inajinasibu kama Simba wing.

Ikiachana na usimbausimba wake na kusimama kama Azam itafika mbali. Uwekezaji wao mkubwa naona hauna returns
 
Tatizo linaloitafuna Azam, ni kwamba imeamua na inajinasibu kama Simba wing.
Ikiachana na usimbausimba wake na kusimama kama Azam itafika mbali. Uwekezaji wao mkubwa naona hauna returns
Hizi story mi nazisikia tu...pamoja na kufuatilia mpira kwa ukaribu lakini sijawahi zithibitisha...labda nithibitishiwe naweza kuliongelea hilo.
 
Ujinga wa Azam ni kukubali kuwa tawi la simba.
Timu yenye akili timamu, haiwezi kumuuliza Manula, Nyoni, Wawa, Boco na kapombe.
Tena wachezaji wote unawapeleka timu moja.

Kuna nyakati walitaka kunivunjia ndoa yangu na Yanga, lakini niliwastukia na kuamua kurudi kuisapoti timu yangu.
 
Hao wapuuzi walianzia madudu kwa yule mkurugenzi wa ufundi abduli sijui akauza wachezaji muhimu wote kwenda team moja ndugu hao mikia ..

Azam saivi uongozi mbovu wanatafuna hela za bosi wao ..
Halafu wanafukuza makocha kila siku
 
kwa hiyo na ninyi mlivowauzia Azam Ngasa, Domayo, Ngoma, Chirwa na ninyi ni tawi la Azam
 
Tatizo Kubwa la Azam FC ni Ubaguzi wa Wachezaji Wazawa na Wageni, Uchawi, Ubahili wa Kuhonga Mechi zao na Majungu kwa Viongozi wao Juu.
 
Tatizo linaloitafuna Azam, ni kwamba imeamua na inajinasibu kama Simba wing.

Ikiachana na usimbausimba wake na kusimama kama Azam itafika mbali. Uwekezaji wao mkubwa naona hauna returns
Buji buji hiii comments haikupaswa kutolewa na wewe tafadhali.
 
kwa hiyo na ninyi mlivowauzia Azam Ngasa, Domayo, Ngoma, Chirwa na ninyi ni tawi la Azam
...Kwa taarifa yako, wachezaji wote hao ukiacha Ngoma, walienda Azam baada ya mikataba yao kufika ukingoni/kuisha..Ngoma yeye aliomba kuvunja mkataba. Ni vizuri na ustaarabu kuongea kitu ambacho una uhakika nacho na sio kukurupuka tuuu
 
...Kwa taarifa yako, wachezaji wote hao ukiacha Ngoma, walienda Azam baada ya mikataba yao kufika ukingoni/kuisha..Ngoma yeye aliomba kuvunja mkataba. Ni vizuri na ustaarabu kuongea kitu ambacho una uhakika nacho na sio kukurupuka tuuu
hata hao kina manula waliachwa na Azam baada ya mikataba yao kuisha. Ngassa aliuzwa mkataba ulikua haujaisha
 
...Kwa taarifa yako, wachezaji wote hao ukiacha Ngoma, walienda Azam baada ya mikataba yao kufika ukingoni/kuisha..Ngoma yeye aliomba kuvunja mkataba. Ni vizuri na ustaarabu kuongea kitu ambacho una uhakika nacho na sio kukurupuka tuuu
Na pia afahamu wachezaji wote hao walienda Azam kwa miaka tofauti sio kama kwa mkupuo kama hao waliotoka Azam kwenda Simba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…