#COVID19 Azim Dewji amvaa Gwajima sakata la chanjo, amwambia ana akili ya kuhubiri siyo Sayansi

Jibuni hoja za gwajima
 
Baki nae hadi siku atakapo mfufua mama yake Kama alivyodai
Gwajima ana utaalamumu gani wa bailogia na kemia achilia mbali viriology ?
Nyie subirini hekaya zake Kama hutaki chanjo nani kakulazimisha?
Mkuu tukiachana na gwajima ambae si mtaalamu kama ulivyosema, hao wataalamu wa nchi hii hadi sasa wametusaidia nini Kuhusu huu ugonjwa?

Kama vipi wajitokeze wajibu kitaalamu kila mtu aelewe na afate ushauri wao
 
Hajapigiwa kura huyu alipitishwa kwa njama za wizi alioushiriki kikamilifu.
Kwa hiyo huyu katika dini sii mhubiri ila ni Simioni mchawi.
Matendo ya Mitume 8:20-24
[20]Lakini Petro akamwambia, Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.
[21]Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za Mungu.
[22]Basi, tubia uovu wako huu, ukamwombe Bwana, ili kama yamkini, usamehewe fikira hii ya moyo wako.
[23]Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo, na tena u katika kifungo cha uovu.
[24]Simoni akajibu, akasema, Niombeeni ninyi kwa Bwana, yasinifikilie mambo haya mliyosema hata moja.
 
Dewji ni dalali wa kuuza chanjo...anatetea percentage yake
 
Hao waliompa ushauri mkuu wa nchi kwamba chanjo ni salama walifanyia utafiti wao wapi na kwa chanjo zipi?
Mkuu....

Kwa hiyo unadhani hizo chanjo zimeingia nchini na kuidhinishwa bila ya kufanyiwa tafiti?!!!

Je hakukuwa na SAMPLE iliyotumwa hapa nchini miezi kadhaa nyuma na kufuata mlolongo wa KUANGALIWA....Wataalamu wanajua....labda walimfanyia SOKWE.....

Nina imani serikali yetu adhimu haikukurupuka Kwani si mara ya kwanza KUPIMA UBORA WA CHANJO TOFAUTI.....
 
Kwanini yeye(Gwaji boy) amepinga hiyo chanjo kwa kutumia facts za kisayansi au amesema tu hachanjwi bila ya kutoa sababu za kitaaluma.
Hivi alivyochanjwa ndui utotoni wazazi wake walitumia sayansi ipi mpaka wakakubali achanjwe? Je ilimdhuru?
Uoga wake wa chanjo ni bora akafafanua kisayansi ili wenye akili timamu wachambue mbivu na mbichi kutoka kwenye 'utafiti' wake au kama huyo 'Askofu' Gwajima amefunuliwa na bwana kupitia malaika wake basi pia hana budi kutuhabarisha.
 
hatutaki chanjo kawaambieni bwana zenu mabeberu
Duuuh 🤣🤣

Beberu anaweza kuwa hata Mnyamwezi ,Mzaramu ama Mhaya....

Ubeberu hauna RANGI YA NGOZI MKUU ....

Kuna mabeberu wengi tu humu mitaani......

Chanjo hizo SI mara ya kwanza kutolewa na SERIKALI TENA ZIKITOKA HUKOHUKO.....

Mbona huzikatai DAWA ZA UKIMWI(AIDS) na TB(KIFUA KIKUU)....nazo zinatoka nje ya nchi....

#TwendeniTukachanjwe
#JikingeNaUmkingeMwenzako
#KaziIendelee
 
Je hakukuwa na SAMPLE iliyotumwa hapa nchini miezi kadhaa nyuma na kufuata mlolongo wa KUANGALIWA....Wataalamu wanajua....labda walimfanyia SOKWE.....
I know you're not serious. Yaani chanjo ifanyiwe utafiti kwa miezi michache, tena kwa kujaribiwa kwa sokwe halafu utuambie ni salama kwa binadamu!

You must be joking.
 
Sasa hao wanaojiita watetezi wa chanjo si wajibu Kwa nini hizo chanjo haziruhusiwi kutumika huko majuu! Watu wajibu hoja kisomi siyo kumnyamanzisha Gwajima na kumtisha. Hoja hujibiwa na hoja. Kama wamekubali udalali na kutufanya tuwe panya wa majaribio. 28.07 waende na familia zao kupewa chanjo,ila sisi wengine watuache
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…