Aziz K anaweza kuwa ni one-season wonders na akajutia kuacha Ofa ya CR Belouzidad

Uongo bhana!
Kweli kabisa mpira naupenda na nimeucheza na ni mshabiki wa Simba lakini ushabiki wangu siyo wa kunifanya nipoteze muda mwingi kuongelea mambo ya Simba na Yanga kwani yana effect ndogo sana kwenye maisha yangu ya kila siku, tofauti na siasa kwani ndiyo zinaamua hatima ya nchi yetu na watu wake.
 
Hizo ofa zipo kwenye midomo ya waandishi wa habar na Viongozi wa Yanga tu,,, vinginevyo tuamini management ya Aziz Ki akiwemo wakala wake na yy mwenywe ni wajinga kuacha hiyo ofa eti kisa anaipenda yanga,, na hata yanga wenyewe kama wanaweza kumrubuni mtu akaacha million 97 Kwa mwezi afu wao wakampa 35,, ni zaidi ya uchawi icho walichofanya!!!
 
Wakati fulani tuwe tunajifunza kuheshimu maamuzi ya mtu. Kupangiana maisha siyo poa hata kidogo. Aziz Kii ni mtu mzima. Hivyo ana haki ya kufanya maamuzi yake binafsi.

Hata kama ataamua kuondoka Yanga, bado atakuwa hajafanya kosa. Maana huo ni uamuzi wake.
 
Wamem- foolish kijana wa watu, ....likely watu waliomzunguka .
Pengine hana ndoto ..
 
Mashabiki wa 5imba wanasikia uchungu Aziz kusaii Yanga,mwacheni ndio chaguo lake wakala na yy mwenyewe wanajua nini wanacho kifanya.
 
Tukumushane, Aziz K wa msimu huu,

Najinukuu

"yawezekana msimu uliopita ndo ukawa ni msimu wake bora kwenye maisha yake ya soka na akajutia kuiacha hii ofa yenye mshahara mnono na sign fee kubwa"
 
Aziz Ki si mchezaji wa maana kabisa, ukiondoa mashuti yake ana nini cha ziada kiwanjani? Hajuwi kukaba na hana mchango wowote ndani ya team zaidi ya kupiga makombora tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…