Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 866
Tatizo la kutokuwa na sifa haliko kwa hao wascandnavia,tatizo liko kwetu,na unaweza kuona wasacandnavia bado wanatufundisha namna ya kufuata sheria zetu sisi wenyewe.
Unless serikali iwe either imefanya utumbo kwa kutokuwa makini,ama 'Ilidhani" kuwa imesha pitisha sheria ya uraia wa nchi mbili.
Mzee Mwanakijiji,Nimepokea habari hizi za unyeti wa ndugu yetu Dr. Aziz Ponary Mlima ambaye nusura aukwae ubalozi wetu kwenye mojawapo ya nchi za Scandinavia. Bahati mbaya (sijui ni kwake au kwa nchi) ni kuwa wenye nchi yao kule walimkataa kwa sababu ambazo zilikuwa ndani ya uwezo wetu!
Labda hili suala la dual citizenship inabidi tulifikiria jinsi litakavyofanya kazi kwa public servants wetu isije kutokea yale ya Fujimori kule Peru!
Thanks ka nzi!
kwa hiyo unafikiri tunaweza kuwa na Rais ambaye si Mtanzania? sijazungumzia tatizo la kuwa na mtu ambaye si Mtanzania kushika nafasi mbalimbali hata Zanzibar waliwahi kukopa Jaji Mkuu kutoka Nigeria???
Marekani haina uraia wa nchi mbili kama watu wanavyoamini; Marekani inatambua uraia wake tu.
Is it possible to be a dual citizen of the United States of America and another country?
YES -- in many cases.
If you have been a dual citizen from birth or childhood, or else became a citizen of another country after already having US citizenship, and the other country in question does not have any laws or regulations requiring you to formally renounce your US citizenship before US consular officials, then current US law unambiguously assures your right to keep both citizenships for life.
The US State Department -- once quite combative in its handling of dual-citizenship claims -- has changed the way it handles these cases in recent years, and it is now much easier to retain such a status without a fight than it used to be.
The situation is slightly less clear for someone who becomes a US citizen via naturalization and still wishes to take advantage of his old citizenship. People who go through US naturalization are required to state under oath that they are renouncing their old citizenship, and conduct inconsistent with this pledge could theoretically lead to loss of one's US status.
However, the State Department is no longer actively pursuing cases of this nature in most situations. In particular, when a new American's "old country" refuses to recognize the US naturalization oath (with its renunciatory clause) as having any effect on its own citizenship laws -- and insists that the person in question must continue to deal with his old country as a citizen thereof (e.g., by using that country's passport when travelling there to visit) -- the US State Department generally no longer minds.
Similarly, the State Department doesn't seem to be doing anything any more to people who renounce their US citizenship as part of a foreign country's "routine" naturalization procedure (in a manner similar to what the US makes its new citizens do). However, if the other country in question requires its newly naturalized citizens to approach officials of their old countries to revoke their previous status, one will generally not be able to remain a citizen both of that country and the US.
Mtanzania,Mzee Mwanakijiji,
Ilikuwaje kwa Tanzania ambayo haina dual citizenship mtu ambaye sio raia akateuliwa kuwa balozi? Nasema hivyo kwa maana mtu ukiomba uraia wa nchi nyingine automatically unakuwa umepoteza uraia wa Tanzania.
Binafsi namfahamu Dr. Mlima na tumewahi kutofautiana na pia kukubaliana kwa mengi. Angepata hiyo kazi, angekuwa nafuu mno kuliko wengi wa hao mabalozi wetu.
Kama walimfikiria kuwa balozi, nina uhakika anaweza kufaa kwa kazi mbalimbali pale nyumbani hasa upande wa uchumi.
Tatizo hapa si uraia wa nchi mbili bali Scandinavia wamemkataa wakisema raia wao hawezi kuwa balozi katika nchi yake mwenyewe. Hata kama Tz tungekuwa na uraia wa nchi mbili bado ingekuwa kikwazo kwa Dr Azziz. Tatizo Dr Azziz hakuwa mkweli kwa serikali ya JK, alitakiwa aseme kwamba yeye kisheria ni raia wa (nchi kapuni) Scandinavia kabla JK hajapeleka maombi....usiri ndio umeumbua serikali.
jokaKuu,
Inavyoonekana Watanzania walikuwa hawajui kuwa mwenzetu kishajilipua na alipopewa uteuzi huo hakusema kuwa tayari ni raia wa kule.
Je, tuko tayari rais wetu awe ni raia wa Tanzania na Kenya at the same time? au wa Rwanda na TZ at the same time au nchi nyingine yoyote? Vipi kuhusu Ubunge, Uwaziri, Ukuu wa Jeshi, vyombo vya usalama n.k?
jokaKuu,Mzee Mwanakijiji,
..wewe umezungumzia uraia wa nchi mbili, sasa mimi kwa makusudi kabisa nikaenda to the extreme kwa mifano ya wahusika ambao hawakuwa raia wa Tanzania kabisa.
..kama alivyopendekeza Julius, iandikwe sheria ya uraia ambayo itazuia wale wenye dual citizenship kushika nafasi fulani fulani ambazo ni too sensitive.
..personally, napendekeza Raisi wetu asiwe na dual citizenship. pendekezo langu halisukumwi na masuala ya loyalty ktk nafasi ya Raisi, bali ni suala la hadhi tu ya nafasi hiyo.
hapa ndiyo tatizo la uraia wa nchi mbili labda pia litaonekana. Je, tuko tayari rais wetu awe ni raia wa Tanzania na Kenya at the same time? au wa Rwanda na TZ at the same time au nchi nyingine yoyote? Vipi kuhusu Ubunge, Uwaziri, Ukuu wa Jeshi, vyombo vya usalama n.k?
Unapolana uraia unatakiwa uandike barua ya kuukana, Na huko nyumbani wanatakiwa kutangaza nadhani mara 3 kwamba umekana..
Yebo Yebo,Hii ndio SABABU nyingine muhimu ya kutufanya tupitishe SHERIA ya Uraia wa Nchi 2 haraka iwezekanavyo. Watanzania wenye uraia wa nchi 2 wapo ila kama ilivyotokea Scandnavia tunashindwa kuwatumia kulitumikia taifa.
Kwa nini hakuukana uraia wa Scandnavia (sijui nchi gani) na kuurudia Utanzania?
Jasusi,Mtanzania,
Good to see you again. Nasikia huyu si wa kwanza. Kuna mtu kasema kuna maafisa wengi tu waliotumika kwenye foreign service wana u duo.Tatizo linakuja pale nyumbani kwa kutokuwa makini katika vetting system, au walimwuliza kama amewahi kuchukua uraia wa nchi nyingine na akakana na hence wenyeji wake wakamuumbua. Pale London nasikia tumeshawahi kuwakilishwa na balozi ambaye naye alikuwa ni duo, au aliyewahi kukana uraia wa Tanzania.
Hapo ndio inapelekea ile pointi ya Joka Kuu kwamba wamefanya makusudi?Hii ndio SABABU nyingine muhimu ya kutufanya tupitishe SHERIA ya Uraia wa Nchi 2 haraka iwezekanavyo. Watanzania wenye uraia wa nchi 2 wapo ila kama ilivyotokea Scandnavia tunashindwa kuwatumia kulitumikia taifa.
Kwa nini hakuukana uraia wa Scandnavia (sijui nchi gani) na kuurudia Utanzania?
MgonjwaUkimwi,Sio kweli, hautakiwi kutoa talaka kwa uraia wa Tanzania ili upate wa ng'ambo. Hapo umedanganywa kwa kishindo. Nchi za ng'ambo wala hazijali uraia wako wa asili, ukiwa na vigezo wanakupa bila hata swali moja juu ya uraia wako wa asili.
Lakini itakuwa jambo jema kama tukimuliza Balozi Mombo kuhusu mambo haya au Membe mwenyewe, ila kwani yupo katika Taifa gani??inadaiwa yeye ni raia wa huko huko tayari.. sasa nchi inampendekezaje raia wa nchi nyingine kuwa balozi wake?
Jmushi1,Hapo ndio inapelekea ile pointi ya Joka Kuu kwamba wamefanya makusudi?
Kwanini wamtake aukane uraia,kwani tuna lack watu wengine wenye qualifications zinazokidhi hadi hapo tutakapo pata ufumbuzi wa uraia wa nchi mbili?
Pia hapo unaposema kuna watanzania wenye uraia wa nchi mbili unaweza kufafanua?
Ningeshukuru mkuu kwasababu kama bado hatujapitisha sheria ya uraia wa nchi mbili,ninavyoelewa ukishapata uraia wa nchi nyingine automatically unakuwa umeukana uraia wa Tanzania,is that true ama niko wrong?
Jasusi,
Nipo ndugu yangu ila mambo yamekuwa mengi.
Hiyo ni failure kubwa sana katika vetting system yetu. Inajulikana Dr. Mlima amekaa Sweden muda mrefu, ameoa huko kama sikosei na hata alivyochukuliwa kwenda kumsaidia Mkapa alitokea huko. Ningetegemea wangeanzia huko kuchunguza.
Huko mbele hili tatizo litakuwa hata kubwa zaidi maana watanzania wanaoishi na uraia wa nchi mbili kwa kujificha sasa wako wengi sana.
Kwa udhaifu kama huu, sitashangaa kweli mtu asiye raia kisheria akiweza kuchaguliwa kuwa rais.
Waruhusu tu dual citizenship ili kuwaondolea Watanzania tatizo la kuficha na kudanganya.
Sijakupata mkuu.nieleweshe tena tafadhali.