B hits vs mabeste saga wasanii wa bongo flava kama hawajarudi shule wasahau kufanya music kimataifa

B hits vs mabeste saga wasanii wa bongo flava kama hawajarudi shule wasahau kufanya music kimataifa

C.T.U

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2011
Posts
5,074
Reaction score
3,743
Leo niko hapa kuliongelea hili swala la Bhits na saga yao ya kuondokewa na wasanii mahiri kama mabeste, vanessa mdee na dogo gosby nilichokigundua hapa ni kuwa wasanii wa watanzania bado hawajajitambua wao ni akina nani, kila kitu wao wanakichukulia poa sana, wao swala la mikataba wao wanaichukulia very simple yaani wanaichukulia poa tu.

Hawajui kuwa mikataba inaweza kumfunga mtu wao hawalitambui, hawajui kuwa mikataba inaweza kumfilisi mtu wao hilo hawalitambui (hili ni tatizo) leo kwa wale waliosikiliza clouds fm kulikuwa kuna interview iliyowashirikisha advocate wa bhits somebody kimaro pamoja na mabeste mwenyewe hapa ndipo nilipokuwa naona vituko.


tukirudi nyuma utakumbuka Hermy B alishawahi kusema kuwa ameinvest zaidi ya milioni 30 kwa mabeste mabeste na wapambe wake na watu wanaojiita ma fans wa mabeste walimtukana hermy b wa watu na kumsema mara oooh mara hivi

ukifuatilia hapa ni kwamba hawajui wameinvest kivipi hizo milioni 30 turudi nyuma 5 years back nani alikuwa anamjua mabeste? mimi nilikuwa simjui, wewe ulikuwaa humjui na yule alikuwa hamjui mabeste...
kama kuimba alikuwa anaimbia kitandani kwake ndani ya neti yake hakuna mtu yeyote aliyekuwa anamjua mabeste

valuation yake kama msanii ilikuwa haizidi 50,000 tsh

Hermy B , Pancho na wenzake wakamjenga na kumuweka hapa alipo sasa na valuation yake ni zaidi ya milioni thelathini za kitanzania

according na kimaro wanakwambia milleage waliyokuwa wamepanga wapate na mtu kama mabeste ilitakiwa iwe ya maana tunaongelea seven to eight figures

leo tu wameishia kwenye millioni 30
mabeste kaota mapembe
mabeste yeye ndio yeye
mabeste hajielewi
mabeste hajui anataka nini
mabeste hajui nini maana ya mkataba

kwani kipindi yeye ana sign mkataba wao Bhits walikuwa na mwanasheria yeye mabeste alikuwa yeye kama yeye pengine na girlfriend wake ambaye ndio PA wake sidhani kulikuwa kuna kiti kingine ambacho kilikuwa kimekaliwa na mwanasheria wa mabeste, sidhani kama mabeste alienda na mwanasheria wake ki sign ule mkataba.

Wamemaliza ku sign mkataba badala waende wausome ule mkataba na PA wake wao wanarudi gheto na PA wake wanafanya mapenzi YES si ni mpenzi wake... kuna Professionalism kweli hapo?? utoke wapi

Ndio maana wakawa wanitwa kwenda kupiga show zao wenyewe bila hata Bhits kujua
wanapiga shows zao wenyewe na kuweka mpunga mfukoni
wanapiga shows zao wenyewe bila hata ya bhits kuweka banners zao kwenye shows hizo

kwa sababu mabeste na PA wake walikuwa hawauelewi mkataba waliou sign na BHITS walikuwa wanachukulia poa tu

kitu ambacho valuation ya Bhits inakuwa pale pale huko mabeste akizidi kupaa

kwanini ufanye kazi ambayo haikulipi?? hata kama ni wewe unatupa kule

na kwa nini uende kinyume na mkataba??

hili ni swali ambalo mimi kila siku najiuliza sana na hii imetokea kwa kina VANESSA MDEE NA GOSBY yale yale kwenda kinyume na mkataba unavyosema na hii ni hulka yetu watanzania mkataba unasema hivi sisi tunafanya vile, mkataba unasema usifanye kitu hiki sisi tunafanya kitu kile , mkataba unasema fanya kitu hiki sisi hatukifanyi sasa kwa nini uli sign mkataba ambao ulijua kuwa mwisho wa siku utakubana?

kwanini uli sign mkataba ambao ulijua kuwa masharti yake huyawezi??

huko si ndio tunauita UMBUMBUMBU yaani kichwani mtu unakuwa hamna kitu


Kwa mtindo huu kamwe usitegemee kusign SONY BMG
kwa mtindo huu UNIVERSAL RECORDS utakuwa unaiona kwenye TV
kwa mtindo huu studio za CASH MONEY utakuwa unaziona kwenye internet

Hutaweza kuingia hawataki ujinga wa namna hii

Mziki sie tunachukulia kitu easy ans simple tu Label sie tunachukulia kitu easy kama vile mnavyoendaga maisha club ila kuna mengi sana nyie wasanii mnatakiwa myajue unless mtakuwa mnatoa tu macho kila siku
 
Shikamoo mkuu c.t.u ngoja nikifika mwanza ntasoma zaidi na kuchangia ila umeandka nondo.
 
Hahahahaaaa.. Watanzania hatupendi kusoma, hilo liko wazi..
Vanessa yupo ana celebrate Obama kum follow twitter.
Kumbe Mabeste ni msanii mahiri? Sikujua
 
Tstizo la wasanii wengi wa kibongo shule hamna kichwan hlo ndyo tatizo wanapenda kushine bila kuangalia kipato Chao kinaingia vp wasanii wa bongo amken mrudi shule hrs mchukue course fupi za kujitambua
 
Leo niko hapa kuliongelea hili swala la Bhits na saga yao ya kuondokewa na wasanii mahiri kama mabeste, vanessa mdee na dogo gosby

Mkuu usiamini unayosikia au unayoyaona kwenye mitandao na vyombo vya habari kuhusu sakata hili, mimi binafsi nimelifuatilia hili sakata kiasi kuongea na baadhi ya wahusika.

Hapa nitaongelea kwa kifupi,

Mabeste ameondoka Bhits tangu mwezi May, na yeye ameondoka baada ya mkataba wake kuwa umemalizika, mkataba wa mabeste umemalizika mwezi wa April, kwa sasa Mabeste ni independent artist,alipoamua kuto kuongeza mkataba baada ya kuona wenzake hawamsaidii na wala hakuona faida yoyote ya muziki wake, hakwenda kwenye vyombo vya habari kuutangazia uma, yeye aliendelea na shughuli zake za muziki kama independent artist, lakini kwa muda wote huu Bhitz walikuwa walimwomba arudi, lakini hakuwa tayari ku sign mkataba mpya.

Mwezi wa kumi mabeste alikuja na record mpya inayoenda kwa jina la "NISHAURI" bhitz wakatahamaki kwa kuwa wao waliamini mabeste hataweza kusimama kama independent artist, Pili ni Vanessa na Gosby hawa nao mikataba yao imeisha na wao vilevile walikataa kusign mikataba mipya baada ya kuona haiwalipi kibiashara ikiwa ni kuwekewa vizingiti vya kufanya shows za clouds, nao vile vile hawakwenda kwenye vyombo vya habari kutangaza kuto ku re new mikataba yao, baada ya hapo walikwenda kwa Prodocer Nahreel wa Mo record na kurecord wimbo mpya wa Vanessa wa "COME OVER" Kitendo kilichoushtua sana uongozi wa Bhitz, kwa kuwa kama kawaida yao hawakutegemea kama hawa vijana wangeweza kusimama kama independent artists, wakisahau kuwa kwa kipindi chote cha mikataba yao ya mwaka mmoja walikuwa wakijisimamia kwa kila kitu, kazi iliyotakiwa kufanywa na uongozi wa bhitz.

Na baada ya kuona kuwa wamewapoza wasanii hawa, wakaingiwa na hasira na wakaanza kufanya mahojianao na vyombo vya habari wakiwapaka matope wasanoii hawa kuwa wamewatimua kwa kuwa hawakuwa na adabu na walikuwa wanaenda tofauti na mikataba yao na mambo mengine mengi ya uzushi kama kuinvest shilling million 30 kwa kodi ya nyumba ya mabeste, na mengine mengi ya uongo.

Kwa nini Bhitz waliamua kuhusisha vyombo vya habari, jibu ni moja tu, walikuwa wanataka kuwapaka matope vijana hawa , kwa mashabiki, maproducer na wadau wa music kwa ujumla, watoto wa mjini watakwambia jamaa wakikuwa wanataka kuwaharibia.

Ikumbukwe kabla ya Mabeste, Gosby na Vanessa, wasanii wengie waliokimbia Bhitz kutokana na maslahi ya kibiashara ni pamoja na MansuLi, AY, Mwana FA etc

Tuko kwenye soko huria na kila mtu anauwezo wa kuchagua kufanya biashara na nani bila kulazimishwa wala kuburuzwa.

Asalam

Sr.
 
hao jamaa zako mapromota uchwara ni wanafiki wameenda redioni na begi la nguo kuthibitisha eti walikuwa wakimwazima jamaa nguo, hata bHits hawawezi kuifikia Sony kwa stahili hiyo
 
hao jamaa zako mapromota uchwara ni wanafiki wameenda redioni na begi la nguo kuthibitisha eti walikuwa wakimwazima jamaa nguo, hata bHits hawawezi kuifikia Sony kwa stahili hiyo

Nakubaliana na wewe hiram

Hawa jamaa baada ya kutoswa wanachofanya sasa hivi ni kumdhihaki na kumtungia uongo Mabeste, mwanzoni walidanganya kuwa wamemlipia million 30 ya kodi ya nyumba Mbagala, baada ya watu kuwatoa nishai, jana wakaingia clouds na beg la nguo, eti walimnunulia nguo, unawezaje kuninunulia nguo miaka mitatu iliyopita na wakati huohuo nguo hizo ziko kwako na siyo mpya....hawa vilaza biashara imeawashinda
 
Kweli siasa zishaingia kwenye tasnia ya muziki! Soko Huria linasakamwa sana Tanzania
 
Kaka Dozen nimesikiliza kwa makini mahojiano leo nimegundua hao hao B HITZ wanamatatizo sana huyo AMANI mdogo wake HERMY B anajaribu kujitetea kwa vitu visivyo na msingi anaongozwa na hasira na jazba mkataba wamesaini 2012 na ume expire iweje waongelee maswala ya nyuma yanaingiaje? Na HAMY b alimaanisha kwenye sms yake ila wamejua kama wamekosea ndiomana AMANI amejaribu kutumia kazi yake kutetea kama fimbo ya kumchapia mabeste ila kiukweli amechemka kuja na begi la nguo pamoja picha kwa stahili hiyo amejivua vyeo,,,salute nyingi sana kwa Pr wa Mabeste ameongea point sana na yeye ndio kaja kuwaweka uchi kabisa BHITZ

Hii nimeidaka kwenye mjadala unaondelea kwenye mtandao wa istagram, maproducer wamezoea sana kuwanyanyasa wasanii lakini naona sasa wasanii wameamka, watu design hii unawatia kwenye vyombo vya sheria...nyambafu
 
Ilo saga kama umelisikiliza vizuri ipo wazi b hitz ndio wameloose na kwa jinsi wanavyolialia nadoubt kama watakuwa wamejifunza
 
Back
Top Bottom