Baada ya Alikiba kuwa mdhamini mkuu wa Kombe la Dunia, Waopambana kumshusha watafanikiwa kweli?!

Lavit

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2011
Posts
14,834
Reaction score
32,522
Toka Alikiba arudi kwa mara ya pili kwenye game kumekuwa na kundi kubwa sana la watu wasiomtakia mema katika muziki wake, wamekuwa wakihubiri uzalendo na kusapoti kazi za nyumbani ila ikifika kwa Kiba hali inakuwa tofauti.

Tukirudi mwaka 2014 baada ya kutoa kibao cha Mwana maneno mengi sana yakasemwa kwamba jamaa kachoka na afanye kazi nyingine eti kibao cha mwana ni kibaya sana, Mwana ilifanikiwa kupenya katika kila sikio la mpenda burudani, na hata video ambayo ilipondwa na kila mtu iliweza kutrend nchi kibao duniani na kumletea kiba tuzo lukuki.

Kiba hakuiishia hapo, amekuwa akitoa hits nyingi zikiwemo Aje, Seduce Me na Sasa Mvumo wa radi. Wengi wa wakosoaji wake wamekuwa wakiponda nyimbo zake huku wakirefer nyimbo zake za nyuma, kwamba kila akitoa ngoma mpya basi ile ya zamani automatically inakuwa kali. Hivyo basi hata ukali wa ngoma hii ya sasa utaweza kuonekana pale atakapotoa ngoma nyingin.

AK hajaishia hapo tu, ameza kuwa balozi wa Willaid, amefanikiwa kusainia na label kubwa zaidi duniani yaan Sonny, amekuwa na patnership na Rockstar Africa, kaanzisja label yake "kings music" na kubwa zaidi mwaka huu kaja na kinywaji chake cha Mofaya yeye akiwa mmiliki mweza wa kiwanda hicho.

Kubwa zaidi Kinywaji chake cha Mofaya ni moja ya Wadhamini wa World Cup kwa hapa nyumbani.

Ila ukienda mbele zaidi watu haya yote hawayataki, wanataka kumuona AK akiwa hafanyi lolote na mwisho wa siku waseme hajielewi.

Mimi nionavyo kuna kundi la watu wana ajenda ya kumshusha AK, swali langu ni je watafanikiwa au ndo jamaa atazidi kuchanja mbuga katika mafanikio ya Kimuziki na kiuchumi?
 
This is what AK does, and I like him for
 

Attachments

  • FB_IMG_15263606450008743.jpg
    16.1 KB · Views: 98
Sifa kubwa ya wabongo ni unafiki mkuu muulize heaven on desert aka Kifesi atakuambia..namna alivyokuwa anaoga matusi humu alipoanza kumnadi diamond
Sijui kwanini tuko hivyo... ifike muda lazima tukubali tu kazi zetu na wasanii wetu, tukiwa na wasanii kibao wenye mafanikio mbona bado ni sifa kwetu kama nchi.
Nakumbuka huyo jamaa alivyokuwa anaoga matusi kwenye nyuzi zake, ila hao hao leo ndio watetezi wakuu wa Diamond hata akifanya upumbavu!
 
Badala mumshauri akanunue dagaa pale katonga awe anapeleka kasulu mnazidi kumpamba na kumpampu tu ashindane na waliomzidi.

Shauri zenu na zake! huyo sasa anaangukia pua.
Levo za kibakuli ni kina dogo janja na best naso😛

Haka kabifu ndio kanamuweka kiba njini,,,,,,, sasa Mond ameshtuka hampi tena kick!
 
Kwani anafanya ushindani au nyie mnashindanisha anachofanya???

AK anajiamini sana yule jamaa
Alikuwepo, atakuwepo na atazidi kuwepo
 
Kwani anafanya ushindani au nyie mnashindanisha anachofanya???

AK anajiamini sana yule jamaa
Alikuwepo, atakuwepo na atazidi kuwepo
Kizuri kinaendelea kujiuza ilihali upande wa pili kibaya kinajitembeza bila aibu

KWANGWARU 96•7%
MVUMO WA RADI 03•3% 😛
 
Ajiandae na na fitina ktk industry ya vinywaji huko wapinzani wake ni Azam,Mo ,Kung fu etc na kama hujui Azam nae katoa energy drink ambayo ina package kama ya Mofaya (hizo ni fitina zenyewe) ,bado hapa kwenye bei Azam ni bidhaa inayotengenezwa TZ kwa hiyo bei yake itakuwa ndogo.Ila ajitahidi kuweka reasonable price ambayo kila mtu atahistamili kwa SA ni Rand 10 (Tsh 1800+).Pili zile tabia kwamba hoo mimi sina show off,BIASAHARA YOYOTE MWENZAKE NI SHOW OFF,lazima aitangaze haswa hizi tabia haupo active ktk social network nyimbo zenyewe anatowa moja moja ,zinaweza zikaathiri bidhaa zake sokoni.Manake uchambuzi wako unalenga upinzani kimziki na si biashara yake ya vinywaji.

 
hahahaha eti mdhamini wa kombe la dunia hahaha
 
ngoja kwanza!
MDHAMINI MKUU WA WAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAT?
 
we jamaa una akili sana asee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…