Baada ya fungate ya utawala mpya kuisha, 'vita' imeanza rasmi

Baada ya fungate ya utawala mpya kuisha, 'vita' imeanza rasmi

Stephen Ngalya Chelu

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2017
Posts
8,252
Reaction score
18,335
Katika siku 100 kwanza za Rais SSH alipata uungwaji mkono mkubwa kutoka makundi mengi kwa muda mfupi. Ilikuwa kama nchi ndo imetoka kupata uhuru kutoka kwa mkoloni. Kumkosoa katika jambo lolote lilikuwa kosa kubwa sana maana ungepewa majina kama Mataga, Sukua gang nk. Ilionekana kama alipata mashabiki wa kufa kupona kwa kipindi kifupi kabisa.

Sasa baada ya mkutano wake na wahariri mambo yameanza kubadilika hasa baada ile kauli yake kuhusu katiba na marufuku ya kufanya siasa kwa vyama vya siasa. Watu wameanza kusogea katika nafasi zao za awali kwa kasi kubwa. Ni kama utamu wa fungate la utawala mpya umeisha hivyo wameanza kuonja ladha halisi ya kile kichokuwa nyuma ya fungate.

Watanzania wanafahamika vizuri wakianza kusakama. Hutowaona barabarani ila maneno yao yatakufikia ulipo na yatakuchachafya kwelikweli. Nadhani hiki kipindi kimeshaanza rasmi.

Ngoja tuone atatumia njia gani kuhimili vishindo; kuacha waongee, kuziba masikio, kuwafunga midomo au kukimbia.

Yetu macho.
 
Katika siku 100 kwanza za Rais SSH alipata uungwaji mkono mkubwa kutoka makundi mengi kwa muda mfupi. Ilikuwa kama nchi ndo imetoka kupata uhuru kutoka kwa mkoloni. Kumkosoa katika jambo lolote lilikuwa kosa kubwa sana maana ungepewa majina kama Mataga, Sukua gang nk. Ilionekana kama alipata mashabiki wa kufa kupona kwa kipindi kifupi kabisa.

Sasa baada ya mkutano wake na wahariri mambo yameanza kubadilika hasa baada ile kauli yake kuhusu katiba na marufuku ya
Mikutano ya kisiasa ya chimboni husika ya nje na ile ya ndani ya kitaifa haijazuiwa, hivyo hoja hiyo haina mashiko, pia hoja ya katiba mpya nayo ni mufilisi, haina mashiko kama mkuu wa nchi atakuwa bwege na asiyejitambua! Kwa hiyo sioni shida ktk hoja hizo! Cha msingi ni kuilinda Tz na watz kwa wivu wote kama alivyofanya mtangulizi wake ma sio kucheka na nyani wa ndani na nje!
Agenda ya chanjo ya corona haitakuja kumuacha salama asipo stuka!
 
Mikutano ya kisiasa ya chimboni husika ya nje na ile ya ndani ya kitaifa haijazuiwa, hivyo hoja hiyo haina mashiko, pia hoja ya katiba mpya nayo ni mufilisi, haina mashiko kama mkuu wa nchi atakuwa bwege na asiyejitambua! Kwa hiyo sioni shida ktk hoja hizo! Cha msingi ni kuilinda Tz na watz kwa wivu wote kama alivyofanya mtangulizi wake ma sio kucheka na nyani wa ndani na nje!
Agenda ya chanjo ya corona haitakuja kumuacha salama asipo stuka!
Hayo umeyasema wewe, na wenyewe wana yao.
 
Samia akifikri ataendesha nchi kwa kuwafurahisha chadema atafeli mapema sana!
. Amuulize JK, mpaka vijana wadogo kama kina Mnyika wakimwita dhaifu!
Anaonekana ni mtu anayevutika kirahisi na anayependa kumfurahisha kila mtu.

Akiendesha nchi kihivyo, atakuwa na wakati mgumu sana!

Kuongoza nchi inahitaji uwe kichwa ngumu kiaina..
 
Mikutano ya kisiasa ya chimboni husika ya nje na ile ya ndani ya kitaifa haijazuiwa, hivyo hoja hiyo haina mashiko, pia hoja ya katiba mpya nayo ni mufilisi, haina mashiko kama mkuu wa nchi atakuwa bwege na asiyejitambua! Kwa hiyo sioni shida ktk hoja hizo! Cha msingi ni kuilinda Tz na watz kwa wivu wote kama alivyofanya mtangulizi wake ma sio kucheka na nyani wa ndani na nje!
Agenda ya chanjo ya corona haitakuja kumuacha salama asipo stuka!
Mwambie huyo Mama, Katiba MPYA ni mhimu kwa watanzania kuliko unavyofikiria.
 
Katika siku 100 kwanza za Rais SSH alipata uungwaji mkono mkubwa kutoka makundi mengi kwa muda mfupi. Ilikuwa kama nchi ndo imetoka kupata uhuru kutoka kwa mkoloni. Kumkosoa katika jambo lolote lilikuwa kosa kubwa sana maana ungepewa majina kama Mataga, Sukua gang nk. Ilionekana kama alipata mashabiki wa kufa kupona kwa kipindi kifupi kabisa.

Sasa baada ya mkutano wake na wahariri mambo yameanza kubadilika hasa baada ile kauli yake kuhusu katiba na marufuku ya kufanya siasa kwa vyama vya siasa. Watu wameanza kusogea katika nafasi zao za awali kwa kasi kubwa. Ni kama utamu wa fungate la utawala mpya umeisha hivyo wameanza kuonja ladha halisi ya kile kichokuwa nyuma ya fungate.

Watanzania wanafahamika vizuri wakianza kusakama. Hutowaona barabarani ila maneno yao yatakufikia ulipo na yatakuchachafya kwelikweli. Nadhani hiki kipindi kimeshaanza rasmi.

Ngoja tuone atatumia njia gani kuhimili vishindo; kuacha waongee, kuziba masikio, kuwafunga midomo au kukimbia.

Yetu macho.
Kwan we unatakaje
 
Katika siku 100 kwanza za Rais SSH alipata uungwaji mkono mkubwa kutoka makundi mengi kwa muda mfupi. Ilikuwa kama nchi ndo imetoka kupata uhuru kutoka kwa mkoloni. Kumkosoa katika jambo lolote lilikuwa kosa kubwa sana maana ungepewa majina kama Mataga, Sukua gang nk. Ilionekana kama alipata mashabiki wa kufa kupona kwa kipindi kifupi kabisa.

Sasa baada ya mkutano wake na wahariri mambo yameanza kubadilika hasa baada ile kauli yake kuhusu katiba na marufuku ya kufanya siasa kwa vyama vya siasa. Watu wameanza kusogea katika nafasi zao za awali kwa kasi kubwa. Ni kama utamu wa fungate la utawala mpya umeisha hivyo wameanza kuonja ladha halisi ya kile kichokuwa nyuma ya fungate.

Watanzania wanafahamika vizuri wakianza kusakama. Hutowaona barabarani ila maneno yao yatakufikia ulipo na yatakuchachafya kwelikweli. Nadhani hiki kipindi kimeshaanza rasmi.

Ngoja tuone atatumia njia gani kuhimili vishindo; kuacha waongee, kuziba masikio, kuwafunga midomo au kukimbia.

Yetu macho.
Maskini mama Samia alijichanganya pale walipokuwa wanampumbaza. Sasa anaanza kazi ili kuelekea 2025.
 
Back
Top Bottom