SAUTI YAKO
JF-Expert Member
- Jan 25, 2014
- 2,944
- 2,032
Ninaandika kwa mwandiko wa machozi mengi baada ya kushuhudia kilichotokea Bukoba ziwani namna tulivyoshughulika kuokoa watanzania wenzetu na hata wengine kupelekea kupoteza maisha Sitaki kujikita sana huko maana tuko siku nyengine mpya. Je hii inchi yetu. Imekosa kweli vifaa vya uokaji?
Mpaka watu binafsi waje watoe kama, wananchi watoe nguvu zao kuvuta ndege au kijana mmoja ajitoe muhanga kupambania maisha ya wengine? KODI ZETU WATANZANIA. Je azitoshi kununua vifaa vya uokaji vikawepo kila mkoa, Mbona kodi zetu zinanunua Magari mengi ya kifahari kwa viongozi Mbona kodi zetu zinatumika sana kuwasafirisha Viongozi kwenda nje kuomba mikopo, kwanini tangu ajari za mv spice Mv bukoba mbona kodi zetu hazitumiki kwenda nje kuomba vifaa vya uokozi?
Mv Spice, MV Bukoba hadi leo tumepata majanga ya ndege wahusika wanaotutawala hamjajifunza jambo au ni makusudi.
Ninawaomba Viongozi wetu kwa msemo huu wa wahenga ukitaka kula na kipofu usimshike mkono,
Kupitia ajari hii nilijua kuna watu wangekuwa tayari kwa kuona aibu wangejiuzuru lakini hamna hilo hadi muda huu. Basi nyie mlogoma kujiuzuru tokeni mbele endesheni kampeni za kututaka watanzania tuchangie vifaa vya uokozi muhimu kila mkoa tupo tayari kupitia TOZO.
Kuliko kuona bado tuko kwenye zama za watu binafsi kujitolea kama,kujitolea kuogelea,kujitolea majeneza, kujitolea kama.WABUNGE MKO WAPI KUITAKA SEREKALI ITOE TAMKO LA KUNUNU Helcpter za UOKOZI Watanzania tumechoka viongozi wa michongo.
Mpaka watu binafsi waje watoe kama, wananchi watoe nguvu zao kuvuta ndege au kijana mmoja ajitoe muhanga kupambania maisha ya wengine? KODI ZETU WATANZANIA. Je azitoshi kununua vifaa vya uokaji vikawepo kila mkoa, Mbona kodi zetu zinanunua Magari mengi ya kifahari kwa viongozi Mbona kodi zetu zinatumika sana kuwasafirisha Viongozi kwenda nje kuomba mikopo, kwanini tangu ajari za mv spice Mv bukoba mbona kodi zetu hazitumiki kwenda nje kuomba vifaa vya uokozi?
Mv Spice, MV Bukoba hadi leo tumepata majanga ya ndege wahusika wanaotutawala hamjajifunza jambo au ni makusudi.
Ninawaomba Viongozi wetu kwa msemo huu wa wahenga ukitaka kula na kipofu usimshike mkono,
Kupitia ajari hii nilijua kuna watu wangekuwa tayari kwa kuona aibu wangejiuzuru lakini hamna hilo hadi muda huu. Basi nyie mlogoma kujiuzuru tokeni mbele endesheni kampeni za kututaka watanzania tuchangie vifaa vya uokozi muhimu kila mkoa tupo tayari kupitia TOZO.
Kuliko kuona bado tuko kwenye zama za watu binafsi kujitolea kama,kujitolea kuogelea,kujitolea majeneza, kujitolea kama.WABUNGE MKO WAPI KUITAKA SEREKALI ITOE TAMKO LA KUNUNU Helcpter za UOKOZI Watanzania tumechoka viongozi wa michongo.