Baada ya kelele za Wananchi, barabara ya Mwanagati yaanza kutengenezwa

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Habari Wanajamvi,

Baada ya kelele za Wananchi wa Mwanagati, Ilala, Dar es Salaam kuhusu ubovu wa barabara yao na kusababisha hadi nauli ya daladala kupanda huku magari yakiwa yanaharibika, sasa imeanza kufanyiwa kazi.

Soma: Hali ya Barabara kwa Wakazi wa Mwanagati inasikitisha

Jana Desemba 21, 203 grader limepita na kusawazisha barabara hiyo kuhakikisha walau inapitika kwa urahisi na kuleta ahueni kwa Wananchi hao waliolalamika barabara hiyo kwa muda mrefu sana.





Pamoja na hayo pia barabara hiyo ambayo pia ipo katika Jimbo la Ukonga la Mbunge na Waziri wa Ardhi, Jerry Silaa imeanza kuwekewa lami ambapo tayari kipande kidogo kimewekewa lami huku Mkandarasi akiwa anaendelea na kazi



MY TAKE:
Wananchi tusiache kupiga kelele kwa tatizo lolote tunaloliona Viongozi wanapita humu na wanaona kila kitu.
 
Si bora mnapiga kelele na mnasikilizwa kuna maeneo mengine kusikilizwa ni kipengele
 
Asante kwa Bandiko Mkuu.

MAKELELE MENGI YANASAIDIA.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Kiufupi
Kiufupi Serikali haijengi Barabara Kwa sababu ya kelele za Wananchi Bali kama hiyo Barabara ilishakuwa kwenye Mpango wa Bajeti.
 
Kiufupi

Kiufupi Serikali haijengi Barabara Kwa sababu ya kelele za Wananchi Bali kama hiyo Barabara ilishakuwa kwenye Mpango wa Bajeti.
Unajua ni mara ngapi imeshakuwa kwenye mipango na fedha zake zikapangiwa kazi nyingine?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…