Baada ya kipigo toka kwa Azam FC akili yangu imeyumba

mwehu ndama

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2019
Posts
630
Reaction score
2,151
Tokea timu Yangu pendwa ya Yanga sc ifungwe na azam fc, katika mchezo wa ligi kuu, akili yangu haiko sawaa, dishi limeyumba kabisaa, naongea peke yangu kama mwehu njiani.

Nakunywa pombe siku ya nne Leo, pia ikumbukwe nilimfukuza mke wangu, pisi ya maana ili nijikite kwenye kuishabikia yanga yangu, nahisi baada ya mechi ya mamelod nitaanza kuokota makopo barabarani
 
🤣
 
Hahahahaha utakua na tatizo..ila watanzania bana
 
Jina lenyewe tu ni ushahidi tosha kichwani kumejaa matope, badala ya ubongo. Hivyo huhitaji maelezo marefu kujipambanua wewe ni nani.
 
tulia mpira uko hivyo hatuwezi kushinda kila mechi,tutarudi kwa nguvu kubwa sana
 
Nini kimekuchanganya kayi ya haya?

1. Kufungwa na Azam.
2. Kufungwa na Fei Toto, Sukari.
3. Yote kwa pamoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…