Baada ya kuanza kuwa bahili, michepuko yangu imenikimbia haipokei simu zangu

Baada ya kuanza kuwa bahili, michepuko yangu imenikimbia haipokei simu zangu

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kutokana na umri kusogea sana imenibidi nipunguze mambo ya starehe kama; kwenda sehemu za starehe, kunywa pombe, kucheza na warembo pamoja na kuchepuka.

Nimeamua kujituliza ili niwaachie na wengine waweze kujiburudisha kwenye hayo mazingira ya kujimwambafai.

Sasa changamoto iko hivi, wale walionizoea viwanjani na michepuko wamekuwa wakinipigia simu na kuniuliza, ''mbona uonekani kwenye viwanja?''

Nami nawajibu, ''uzee umenisogelea najaribu kwa sasa kuweka akiba ya uzeeni na ya kwenda kuishi huko kijijini; kwa sababu maisha ya mjini yameshanichosha.''

Wanakata simu kwa hasira na kuniita, ''wewe bwege nini, wakati tulipokuwa tunakunywa na kutupelekea moto vizuri hukujua hayo?''

Nabakia tu kucheka; kwa sasa nikiwapigia simu, hawapokei simu zangu, nimekuwa kama simba dume mzee niliye telekezwa.​
 
Kutokana na umri kusogea sana imenibidi nipunguze mambo ya starehe kama; kwenda sehemu za starehe, kunywa pombe, kucheza na warembo pamoja na kuchepuka...​
Hii inaweza kuwa habari ya kutunga

Ila huu ni ukweli ambao watu wautumie haijalishi ni vijana au wazee .
 
Baada ya kuacha michepuko naishi kwa amani sana hela za kusaza. Nikipiga posho ile excess niliyokuwa nahodha, kwa sasa narusha kwa wazazi kisha napokea baraka.

Kwa sasa ni mimi na mkanda nje, baasi
 
Kaza hapo hapo wewe sio wizara ya ajira au TAMISEMI,
Wakatafute kazi za kufanya

Kwa mwendo huo mkuu utapiga hatua
 
Back
Top Bottom