Baada ya kufika Moscow leo nimeamua kufuatilia saga la Dr. Shika, kumbe anasema ukweli

Baada ya kufika Moscow leo nimeamua kufuatilia saga la Dr. Shika, kumbe anasema ukweli

Muanzisha mada ameonya unapokopi na kupesti kijuha ila naona huko mitandaoni wameibeba tu ....Wabongo bana
 
Uzuri vyombo vya kijasusi vya wenzetu maneno huwa ni machache vitendo zaidi. Huyu Dr. tunaemuona punguani wao utakuta wapo kimya lakini vyombo vyote vya kipelelezi alivyovitaja vinamfatilia kila taarifa yake na mwenendo wa maisha yake toka hapo awali.

Sisi huku na vyombo vyetu tunaendeleza kupiga mdomo na kumkebehi tuu bila kutaka kwenda ndani zaidi na kutopuuza na kumpuuza. Wenzetu wakiona ni mtu potential order huwa mbili execution ifanyike ili asiendelee kuropoka kama wataona ni potential lakini kuna mbadala wake ambae ni loyal kwao au wamchukue kimya kimya kama hakuna mbadala wake.

Sidhani kama tukimfatilia kwa undani zaidi atatugharimisha lolote au atatupunguzia chochote endepo tukijiridhisha na kumkuta kweli ni Juha.

"Msituni kila mbinu hutumika" tumfatilie na kujiridhisha juu ya ujuha wake.
 
Lancefort Ltd ni kampuni iliyosajiliwa nchini Russia miaka kadhaa iliyopita, na kwasasa haifanyi kazi kwa kipindi kirefu baada ya watendaji wake kupotea gafla kwa mazingira ya kutatanisha.

Kutoka mjini Rostov on don napokaa mpaka Moscow ni mwendo mrefu kidogo ambao ni km 1200 na zaidi, kwa mwendo wa trein ni 5hrs,
nimefika mjini moscow na kuanza kuuliza hasa legality ya kampuni hiyo ndani ya moscow na Urusi kwa ujumla, nimefanikiwa kupata maelekezo ya kukutana na Mtanzania mmoja (Elibariki Dishon) anaisha mtaa wa Tverskaya Street, ambaye kanikaribisha na kuanza kufanya uchunguzi wangu, nikaamua kwanza nipate hifadhi ndani ya hotel ya Sputnik.

Baada ya kwenda kwa watanzania wanaoishi huku nimegundua huyu mzee alipata matatizo kwa kuhisiwa ni spy wa Marekani, ambaye kapandikizwa kutokea Afrika, na amekuwa akitafutwa na kufuatiliwa nyendo zake zote kuanzia kwenye kampuni yake na nyumbani alipokuwa anaishi.
Mke wake bi Luisa Kvonkov ndo alibanwa na kueleza kwao ni Tanzania Magu, Lakini inasemekana kwamba kuna kampuni kubwa la kimarekani aidha shirika la upelelezi ambalo liko nyuma ya kampuni ya Lancefort, ndio chanzo cha kutiwa msuko suko uko alikokuwa anamiliki kampuni hiyo.

Shirika la Lancerfort limekuwa likimiliki asset kubwa nchini urusi na kwingineko duniani wakati chanzo cha hela yao hakijulikani, hivyo moja kwa moja kuhisiwa ni miongoni mwa mashirika ma spy ambao wafadhili wake ni wamarekani ambao wana uhasama wa mda mrefu na Urusi.

Wametelekeza mali nyingi kukiwemo na private jets na magari ya thamani.

Kupitia wapelelezi wa ndani ya urusi ambao walilichunguza shirika ambalo inasemekana rais wake ni Dr Luis Shika kwa kipindi kile, waligundua mawasiliano ya karibu na baadhi ya mashirika yafuatayo AMNESTY INTERNATIONAL, CIA, FBI , HGRE, OKLE, ambayo mara nyingi huwa ni waanzilishi wa upelelezi katiKa nchi nyingi,

Baada ya kugundua hayo walitekwa na kuwekwa mateka na wawili kuuwawa, mmoja wapo akiwa mkenya Edward Koinange na mwingine wa Siera Leone Yunusu AKhbu, Na wawili kukimbilia Tanzania lakini Rais wao akapelekwa hospitali baada ya kuwatoroka akiwa ameumizwa vibaya, hakutibiwa Urusi alitoroshwa kinyemela mpaka mjini Dnipro Ukraine, na kutoroshewa Tanzania,
Baada ya kufika Tanzania hakuenda moja kwa moja kwao akajificha mjini Dar es salaam, (Haya ni maelezo kwa mujibu wa mtu wake wa karibu)
Baadae kutorokea Uhispania Mjini Malaga , amekaa malaga miez 8 Na kurudi Tanzania,

Mwaka 2012 wakaidhinisha malipo kutoka marekani ambayo bado yapo kwenye mlolongo wa
kukamilisha mchakato,

WITO KWA BALOZI ZETU TUNAOMBA MUWASAIDIE HAWA WATANZANIA WANAOKUWA NA MATATIZO MUWASAIDIE

Tukiachana na Shika wapo watanzania wengi wanaokosa msaada wa karibu sana kutoka Kwa balozi zetu hizi ,

Ukisoma ukatafakari haitadhuru

Tufanye nimemaliza

KUNA MENGI SITAYAANDIKA HAPA KUTOKANA NA KUJUA KWAMBA KUMBE HII ISHU NI CRUCIAL , NA KULINDA USALAMA WA DR,

PIA YATAENDELEA KUWA KUMBUKUMBU ZANGU NA KUZIPELEKA MAALI ZITAITAJIKA KWA KUMSAIDIA DR,

USIKURUPUKE KUKOPI HABARI HII, MAANA CODES ZOTE NINAZO MIMI UTASHINDWA KUITETEA,MTU PEKEE MWENYE UWEZO WA KUWEKA EVIDENCE NI MIMI, IKITOKEA UKAKOPI SEMA UMEITOA WAPI,

Britanicca

fac4c12cdf742cab874da9e575e22549.jpg
Huyu mzee asaidiwe kwanza apate uhakika wa milo mitatu akili ikae sawa atasema mengi
 
nakataa kabisa,ukiangalia hiyo website hakuna picha za ofisi,adress ya kampouni hakuna, e mail wanatumia msn wakati proffesionally ilitakiwa labda drshika@lancefortltd.ru then angalia vizuri website yao..www.lancefort.narod.ru ni free hosting sio za kulipia thats why kuna narod katikati ni kama .blogspot.com au .yola.com,website kwa mjanja akiingalia kwa macho tu changa la macho
Uki search google hawana rekodi ya kueleweka no results kabisa,kampuni moja inafanya shughuli kama 40,kuanzia fertilisers,petroleum,pharmaceutical hakuna hata picha za ma executives,mnadanganyika sababu kuna website tena ya free hosting?
CIA,FBI watengeneze bogus company in a foreign soil ambayo ina deal hadi na gesi na petrol?they must be crazy,CIA,FBI wakitaka info nzuri za nchi kama Russia huwa wanatumia wan KGB wa kulekule ndani(MOLES)refer story ya OLEG KALUGIN
nakataaa nakataaaa nakataaaaa ,mtoa mada hata kama kaeleza alichoambiwa simply ni kwamba mzee LUNYALULA KIDOLA aliwanywesha chai ya moto wabongo wa huko ku explain issue yake ya kukatwa vidole na kupoteza meno aka acome up with a fascinating story. NOOOOO
Unaongea hizo habari ukiwa wapi???,, Nenda urusi ukabishane!,
 
Wasomi wa zamani kidogo wa siri sirini wanajua kabisa kuwa

Katika maisha yako dunia hii yenye blocks mbili mahasimu wa ubepari na ujamaa...(Kwa Africa) waogope sana hawa watu wachache miongoni mwa wengine (Labda kama wamekufa au kuchanganyikiwa)

- Edward Koinange (KE)

- Edgar Manase Laizer (Mtz)

- Yunus Akhibu (S L)

- Luis Shika (Tz)

- Mary Nomvete (S.A)

- Josephine Emeka (Nig)

Hao hata wakiota lazima watamke USA.
Hahaha
 
Bunge likiisha na ishu itaisha wabongo ni wajinga sana tumesahaulishwa mambo kibao
 
Mh! Kumbe sio mtu wa mchezo kama tulivyodhani!! Yaan kuhusishwa na CIA na warusi sio mchezo wazee.. Hapo hakuna kubahatisha.. Maana ktk Vitendo vya upelelez duniani urusi nao wamo namba za juu.. Mpk marekani wanamlalamikia kuwaingilia uchaguz wao.. Me nafkr tuishie hapo kwny kufukua habar za huyo mzee kwa waelewa nafkr watakuwa wameshamjua.. Na ni kwann yupo vile..

Sent from my Infinix-X551 using JamiiForums mobile app
 
Ametuma sms kwa mabosi nipeni changu,

Spain mji wa Malaga ofisi CIA North Africa Operation zipo pale,
Hata counter terrarism operation za Niger,Nigeria,Libya,Morroco,Misri etc,misheni nyingi za africa ya kaskazin zinaanzia pale
Yes malaga.Spain
 
Back
Top Bottom