Baada ya kugundua Mashabiki wa Simba SC wanapenda Kudanganywa nami Nikawadanganya vilivyo

Baada ya kugundua Mashabiki wa Simba SC wanapenda Kudanganywa nami Nikawadanganya vilivyo

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Baada ya MINOCYCLINE niliyebarikiwa Jicho la Kiufundi kuja na Uzi hapa hapa JamiiForums Wiki Moja imepita kuwa Raja Casablanca FC ni Maji Marefu kwa Simba SC yangu ( yetu ) nilipokea Matusi, Kashfa na Dhihaka nyingi na hatimaye kile nilichokisema leo kimetokea.

Na baada ya Kugundua na Kuwasoma Mashabiki wa Simba SC hasa walioko hapa JamiiForums wanapenda Kudanganywa na siyo Utaalam wangu wa Kimpira MINOCYCLINE nami kwa Makusudi nikaamua sasa Kuwahadaa, kuwajaza Ujinga na Kuwaaminisha Kisichowezekana na Wengi Wao wakajaa katika Mfumo wangu na Kuwaokota ile mbaya.

Simba SC ingemfunga leo Raja Casablanca FC ningeenda kwa Makusudi kabisa Kunya ( Kuukweka ) pale MP1 Lugalo Makongo.

Timu imejaa Viongozi Wahuni, Wapigaji, Waamini Uchawi, wenye Majungu na Kusalitiana ndani kwa ndani huku ikisajili Michezaji Mikapi ( Rejects ) leo ndiyo uje umfunge Raja Casablanca FC ambayo inaendeshwa Kiuweledi huku ikimtanguliza Allah ( Mungu ) na siyo kuzunguka Mitaani kama Wendawazimu kufanya Hamasa ya Mechi ambayo Moyoni unajua hutoshinda na Kuendesha ( Kinyumenyume ) Basi la Timu ( Wachezaji ) kuingia Uwanja wa Mkapa kwa Kuamini Waganga wa Unguja, Morogoro na Tanga waliopangiwa Hotel ya Kifahari maeneo ya Mbezi Beach mita chache na Makazi ya CDF Mmoja Mstaafu ambaye mpaka leo amebakia kuwa ndiyo CDF Kipenzi cha 95% ya Wanajeshi wa Tanzania.

Mkome / Tukome.

Cc: adriz
 
F27BAB17-075E-4286-9767-9E28B9DCB359.jpeg

Mama hata angeweka bilion 1, wasingepata hata la offside
 
... baada ya Kugundua na Kuwasoma Mashabiki wa Simba SC hasa walioko hapa JamiiForums wanapenda Kudanganywa na siyo Utaalam wangu wa Kimpira MINOCYCLINE nami kwa Makusudi nikaamua sasa Kuwahadaa, kuwajaza Ujinga na Kuwaaminisha Kisichowezekana na Wengi Wao wakajaa katika Mfumo wangu na Kuwaokota ile mbaya.
Sema tu unabii wako umeenda tofauti, usione aibu! Kama ingetokea jinsi ulivyotoa unabii, ungekuja hapa kujisifu. Nadhani unachotaka ni kuua soo. Umebugi na mara nyingi tu huwa unabugi
 
Bro si wewe ulitudanganya simba itashinda rejea Uzi wako wa Toyota Alphard
 
Kibwetere yupo Kila mahala kukwepa melekezo yake inategemea akili ya kuzaliwa nayo⛔🚷
 
Back
Top Bottom