Wakuu..
Tangu kujiunga na jamiiforums nilikuwa nikiamini wanachama wa jf ni binadamu wa kawaida. Lakini baada ya muda Fulani nilijitahidi kuwadodosa marafiki zangu na watu wengine, lakini hakuna hata mmoja aliyeonyesha kuwa anaifahamu. Kila MTU niliyemuuliza/kumdodosa alinijibu kuwa haifahamu jf. Hapo ndipo nikaingiwa na roho ya kudadisi ni kwa nini mtandao ambao kila mda umechangamka kwa post lakini watu ninaoishi nao hawaufahamu, ndipo nilipogundua jambo hili la ajabu.
Jambo hili ni kuwa jf ni kwa ajili ya magreat thinkers tu. Jamiiforums ina watu wenye ubongo mkubwa na unaofanya kazi kama compyta za CIA. Kiufupi jf ni ya watu wasiowaza mambo ya kijinga jinga. Kwa hiyo watu wale wote niliowauliza si ma great thinkers ndiyo maana hawaufahamu.
Ikabidi ni mimi nijifanyie utafiti kama nastahili kuwa great thinker. Na nikaja na majibu kuwa mimi sisistahili kuwa hata kijakazi kwa great thinker. Ni great thinker gani anajiita
mende msafi?, great thinker gani yangu ajiunge jf hajawahi kupata PM?. Ni great thinker gani anashindwa kutoa Uzi kwenye maana kiasi cha kuvuta watu 100 kukoment?
Nimekaa na kutafakari na nimeona kuwa sistahili kuwa hapa.
Kwa herini ma great thinkers.
Narudi fecebook...
Wenu,
Smallest thinker