Baada ya kuliona jengo la Yanga FC, nimeanza kuamini uchawi upo

Shadeeya njoo huku klabu yenu inajadiliwa..
Kaka naona mleta uzi kaamua kuileta habari ambayo imelalia upande mmoja.

Mie nataka nimwambie tu hatukatai ila letu Wananchi lina unafuu ambapo hata ukipita unajua hapa ndio Makao Makuu ya Timu ya Wananchi.

Na sio pale naniliu pale 😜ambapo ukipita mpaka uulize njia ya kwenda huko iko wapi mana kuna machinga mpaka mlangoni.
 
Ngoja tulifuatilie na hilo la upande wa pili
 
Wabongo tunakosea wapi. Jamaa katoa mtazamo wake wewe unaleta mambo ya simba. Mbona kwenye uchumi huwa hatusemi tuwe masikini wote. Kwa mtazamo wako lazima simba ibadilishe jengo lake ndiyo yanga nayo ibadilishe jengo lake.
UMESHAINGIA LA SIMBA UKAONA JINSI NJE MPAKA NDANI LILIVYO BOVUUU.../ ACHA KUISIMANGA YANGA INGIA NDANI YA JENGO LA SIMBA AU INGIA KATIKA JENGO LENYE AZANIA BANK UPANDE JUU ULIANGALIE VIZURI JENHO LA SIMBA.
 
Hii Kitu inapatikana wapi Mkuu?
Nenda pale Kariakoo mtaa wa Lindi karibu na makutano ya lindi/ Sikukuu, opposite na Sapphire court hotel, kuna duka la mabohora wale wahindi wanauza Aluco bonds za rangi kila aina. Hizo Alluminum frames na vioo vya kila rangi vinapatikana gerezani kariakoo.
 
Mbona Wekundu wapo mahali ambapo kwanza ni maarufu sana, pili pana thamani kubwa kulinganisha kule kwenye mashamba ya mpunga(mafuriko kila wakati halafu eti mnapaita jangwani🤣🤣🤣)

Ukiwa kariakoo halafu ukapotea ukiuliza nataka kwenda Msimbazi klabu ya Lunyasi sio tu utaelekezwa bali watajitokeza watu wakupeleke hadi mlangoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…