Baada ya kumjali na kupigania mafanikio yake, leo nimegeuka kuwa mshamba

Kama ni wa kwako atarudi, kama si wa kwako potezea. Na sio ndo ukae umsubiri. Fanya maisha yako jomba. Muache ajifunze na aone hayo anayoyafanya ni ya kawaida sana. Kama yana umuhimu kwake ataendelea nayo. Akiona wewe una umuhimu kwake atarudi.
Hapo mm ndio huwa nakuwaga tofauti kidogo na wengine. Kama ni wake, basi hataondoka. Kitendo cha kuondoka tu, huyo sio wake. Yani aende huko apelekewe moto weee, mambo yakiwa magumu ndio arudi tena kwa jamaa???
 
Pole sana mkuu..
Hayo ni mapito tu.

Ww sio wa kwanza kukumbana na hali kama hiyo,...
Nafikiri ni kujifunza kumsahau na usimame tena.

Simama imara
 
Haiwezekani uitwe mshamba sheikh, pambania goli hata Kama ni la offside sheikh.
Kwanza kwanini akuache baada ya kumtafutia kazi?? Kibaya zaid akutukane mshamba???
Huyo mpige kupapai tu hakuna namna au mpige bastola
 
Hamia chadema
 
Wanawake wote hawa Tanzania bara na visiwani unalalamika kutopokelewa simu na mmoja

Pole sana aisee
 
Atakuwa ni mpenzi wako wa kwanza huyo.

Ukipata mwingine akakupiga tukio kama hilo tena ndo utakuwa umefuzu.

Utakuwa sawa muda si mrefu, ila ukiendelea na ujinga wako wa kukaa ndani utachelewa kuwa sawa.
kweli awe anatoka nje kusafisha macho
 
Weka akiri na nguvu kwenye mambo yako mzee, kuwa busy as if nothing wrong, ukiendelea kumfatilia anajisikia wa thamani zaidi. Afu adi hapo ni ngumu kuishi pamoja maana hatambui thamani ya kujitoa kwako.

Miaka kadhaa ilinitokea Kama haya yaliyokutokutokea, nilichokifanya niliachana nae kwa moyo mmoja na chochcote nilichowahi kumsaidia niliona Kama ni msaada tu ambao naweza kumpa yeyote muhitaji, sikutaka kumuona special Tena .. ilinisaidia sana

Muda wowote unapotoa msaada ata Kama unaempa msaada ni mpenzi wako ebu jaribu kutomfanya special sana, hasa ukiwa huna Imani nae. Msaidie Kama unavyoweza msaidia mtu mwingine yeyote Tena bila kutazamia kurejeshewa fadhira, Mimi imenisaidia sana.

Nilipokuwa chuo frani nilikuwa na bint ambaye pia ningeweza kumuoa, nilimlipia ada ya mwaka mzima, moyoni mwangu sikutaka kuchukulia kwamba ni lazima nimsaidie Kama mpenzi, Ila nilitoa msaada kwasababu amekwama na nilichukulia poa japo yeye alidhani nilimpa kwasababu ni mpenzi wangu..... Aligundua siku nilipomsaidia mtu mwingine tofauti na yeye na alimaindi sana, nikamwambia namsaidia yeyote kwa chochote nilicho na uwezo nacho...akaniuliza Mimi ilinisaidia Kama Nani, nikamwambia Kama mwingine yeyote.. ata alipoamua kuendelea na maidha yake haikuniuma kabisa.

Take easy ni sehemu ya maidha ya mahusiano tu...utafika tu.
 
Insikitisha na pole sana...

Ukiwa nae hajiamini ila anakushutumu wewe kwa kutojiamini sababu unamfuatilia...
Hapendi kuongozana na wewe...

Jibu ni kwamba ana makandokando mengine pembeni ndiyo maana...
 
Kuna member humu aliwahi kusema. Mwanamke hawezi kulala na baba yake kwa sababu baba anatimiza majukumu yake. Alichokuwa anataka kumaanisha ni kwamba ukiona unamsaidia mwanamke unakuwa kama umechukua nafasi ya baba yake, hivyo hawezi kuwa na hisia na wewe.
 
Maisha haya huwezi kujua umuhimu wa kitu mpaka kitakapofutika kwenye uwepo wako.

Japo hatujasikia upande wa binti ila ngoja twende na upande mmoja, kubali kuwa umempoteza hili ni swala muhimu sana katika kuvuka viunzi vya kihisia, Pili jiweke mbali naye mpotezee kwa namna utakayoweza, tatu usiwe na papara ya kutafuta mwanamke mwingine.Huu ni wakati wa ww kuweka muda mwingi kwenye elimu na biashara zako ama sivyo utajikuta umepoteza vyote. Mwisho kabisa kisasi ni cha MUNGU muachie yeye atakulipia muda na rasilimali fedha ulivyopoteza.
 
Hivi ke wamekwisha huko mitaani?
 
Unashindwa kumpotezea mtu ulo kaa nae kwenye mahusiano miezi kumi tu??

Jitahidi kujichanganya.. wapo watoto kibao wazuri hujakutana nao jichanganye kwanza utajikuta unaghairi hata na kuoa kwenyewe mkuu[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…