TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,866
- 5,747
Amesema:
1. CHADEMA wataisaidia ACT-Wazalendo kushinda Zanzibar
2. Baada kupona akiwa Ubelgiji ametembea sana na kwamba Tanzania ya Magufuli haina rafiki hata mmoja nje eti Mkapa hakuzikwa na mataifa ya nje
3. Wakienguliwa kugombea wataingia barabarani
4. Chadema wameweka wagombea Ubunge majimbo yote nchini
Kwa kauli hizi za Lissu , Watanzania mnachopaswa kujifunza hapa ni kuwa Lissu hakuna kitu kabisa. Lakini kauli zake zaidi zinatufundisha yafuatayo:-
1. CHADEMA wanawaogopa sana ACT-Wazalendo na wanaiona nafasi yao ya Kiongozi wa Kambi rasmi ya upinzani Bungeni ikipokonywa na ACT.na ndiyo maana Lissu alijikita sana kuejikanyaga kuelezea nia yao ya kuiunga mkono ACT kwa upande wa Zanzibar lengo ni ACT-Wazalendo kulegeza kamba kwa upande wa Bara, janja ileile ya Muungano wa UKAWA, ACT-Wazalendo komaeni. Kama Lissu anaamini katika umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu , basi awamu hii iwe ni zamu ya CHADEMA kuunga mkno mgombea wa chama lingine cha upinzani katika nafasi ya URAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tukifuata uhalisia Membe ni zaidi ya Lissu.
2. Kuna kila dalili kuwa uteuzi wa Lissu kuwa mgombea urais kupitia CHADEMA kuna mkono wa mabeberu kwa maana ya ufadhili(pesa, magari, vifaa vya Tehama kwa lengo la kuharibu uchaguzi), kufadhili machafuko n.k. hili linadhihirishwa na kauli yake kuwa.amezunguka sana nje na kwamba wakienguliwa wataingia barabarani. Waasisi wa machafuko ya Libya na Misri yaliowaondoa madarakani Ghadafi na Mubarak walianza na kuzunguka nchi za magaribi na kuhakikishiwa kufanikisha machafuko kwa maslahi ya nchi hizo na siyo kwa maslahi ya Libya na Misri.
Tukumbuke.kuwa wakati Rais Magufuli anapambana na kuhakikisha tunanufaika na madini yetu, ni Lissu huyu huyu aliyesema mabeberu yatatushitaki. Mabeberu yatashindwaje kumtumia wakati tangu awali alishaonesha nia ya kuwa kibaraka wao? Huko alikokuwa anazunguka alikuwa akizunguka kwa fedha za nani? Nadhani kauli zake zimetujibu. Uchaguzi wa Mwaka huu ni uchaguzi baina ya mzalendo na mabeberu (uchaguzi wa mleta maendeleo dhidi ya mfadhiliwa wa kuleta. Vurugu .nchini)
3. Wale waliokuwa wanajiita marafiki wa Tanzania ambao leo Lissu anasema siyo marafiki zetu eti kwasababu ya utawala.wa serikali ya awamu ya tano ni wanafiki, walikuwa wanatupaka mafuta kwa mgongo wa chupa wakati tukisifika kuongoza kwa umasikini, hawawezi kupendezwa na Tanzania kuingia katika orodha ya nchi zenye uchumi wa kati, hawawezi kupendezwa na kusikia Tanzania inajenga Reli ya mwendokasi, tanzania ina Ndege 13, Tanzania ina Viwanda, Tanzania inajenga barabara za juu nk. Hawa ni sawa na Mtu anayefurahia kumnyenyekea/kumpigia magoti ukimuomba masaada kila wakati lakini kawe hawezi kufurahia kuona na wewe umepata. na huna haja na msaada wake/wewe siyo wa kumpigia magoti tena.
TUNDU LISSU NI DHAIFU , HANA HOJA NA WATANZANIA SIYO WALIBYA WALA WAMISRI
1. CHADEMA wataisaidia ACT-Wazalendo kushinda Zanzibar
2. Baada kupona akiwa Ubelgiji ametembea sana na kwamba Tanzania ya Magufuli haina rafiki hata mmoja nje eti Mkapa hakuzikwa na mataifa ya nje
3. Wakienguliwa kugombea wataingia barabarani
4. Chadema wameweka wagombea Ubunge majimbo yote nchini
Kwa kauli hizi za Lissu , Watanzania mnachopaswa kujifunza hapa ni kuwa Lissu hakuna kitu kabisa. Lakini kauli zake zaidi zinatufundisha yafuatayo:-
1. CHADEMA wanawaogopa sana ACT-Wazalendo na wanaiona nafasi yao ya Kiongozi wa Kambi rasmi ya upinzani Bungeni ikipokonywa na ACT.na ndiyo maana Lissu alijikita sana kuejikanyaga kuelezea nia yao ya kuiunga mkono ACT kwa upande wa Zanzibar lengo ni ACT-Wazalendo kulegeza kamba kwa upande wa Bara, janja ileile ya Muungano wa UKAWA, ACT-Wazalendo komaeni. Kama Lissu anaamini katika umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu , basi awamu hii iwe ni zamu ya CHADEMA kuunga mkno mgombea wa chama lingine cha upinzani katika nafasi ya URAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tukifuata uhalisia Membe ni zaidi ya Lissu.
2. Kuna kila dalili kuwa uteuzi wa Lissu kuwa mgombea urais kupitia CHADEMA kuna mkono wa mabeberu kwa maana ya ufadhili(pesa, magari, vifaa vya Tehama kwa lengo la kuharibu uchaguzi), kufadhili machafuko n.k. hili linadhihirishwa na kauli yake kuwa.amezunguka sana nje na kwamba wakienguliwa wataingia barabarani. Waasisi wa machafuko ya Libya na Misri yaliowaondoa madarakani Ghadafi na Mubarak walianza na kuzunguka nchi za magaribi na kuhakikishiwa kufanikisha machafuko kwa maslahi ya nchi hizo na siyo kwa maslahi ya Libya na Misri.
Tukumbuke.kuwa wakati Rais Magufuli anapambana na kuhakikisha tunanufaika na madini yetu, ni Lissu huyu huyu aliyesema mabeberu yatatushitaki. Mabeberu yatashindwaje kumtumia wakati tangu awali alishaonesha nia ya kuwa kibaraka wao? Huko alikokuwa anazunguka alikuwa akizunguka kwa fedha za nani? Nadhani kauli zake zimetujibu. Uchaguzi wa Mwaka huu ni uchaguzi baina ya mzalendo na mabeberu (uchaguzi wa mleta maendeleo dhidi ya mfadhiliwa wa kuleta. Vurugu .nchini)
3. Wale waliokuwa wanajiita marafiki wa Tanzania ambao leo Lissu anasema siyo marafiki zetu eti kwasababu ya utawala.wa serikali ya awamu ya tano ni wanafiki, walikuwa wanatupaka mafuta kwa mgongo wa chupa wakati tukisifika kuongoza kwa umasikini, hawawezi kupendezwa na Tanzania kuingia katika orodha ya nchi zenye uchumi wa kati, hawawezi kupendezwa na kusikia Tanzania inajenga Reli ya mwendokasi, tanzania ina Ndege 13, Tanzania ina Viwanda, Tanzania inajenga barabara za juu nk. Hawa ni sawa na Mtu anayefurahia kumnyenyekea/kumpigia magoti ukimuomba masaada kila wakati lakini kawe hawezi kufurahia kuona na wewe umepata. na huna haja na msaada wake/wewe siyo wa kumpigia magoti tena.
TUNDU LISSU NI DHAIFU , HANA HOJA NA WATANZANIA SIYO WALIBYA WALA WAMISRI