Kuhusu gharama ni vema ukajua kuwa Marekani kiuchumi yupo mbali sana, yaani ni kama umkosoe Mo au GSM kuwa kumiliki magari mengi ni gharama sana kwao.
Pili ni vema mkaelewa kuwa SILAHA alizonazo Russia inawezekana hata wenzake wanazo bora kama hizo au zaidi.
Tatu nyie mnaokosoa aircraft carrier nadhani mnatakiwa kufikiria kiakili zaidi kwasababu kama mwenzako kasogeza hizo carrier jirani na wewe halafu itokee vita baina yenu, je, unafikiri mwenye advantage zaidi ya mwenzake ni nani.
Obviously mwenye carrier atakuwa na advantage kwasababu atakuwa anakushambulia kutoka kwenye carrier na pia kutokea nyumbani kwake kwa kutumia long range missile au ICBM. NI RAHISI SANA WEWE USIYE NA CARRIER KUWA NEUTRALISED.
SISI TUPO KWEMBE, BUNJU, GOBA, KIVULE,UNUNIO, MBWENI INAYOKERA KIPINDI CHA MVUA, KIBADA, KWA MOROMBO, SAKINA, OLASITI, NYEGEZI, FUONI ZNZ, MWANAKWEREKWE, MIPANGO DODOMA .NDIO TUNAICHEKA MAREKANI KUMILIKI AIRCRAFT CARRIER NA KWAMBA ETI SI LOLOTE KWENYE VITA.
Hivi wewe Kinchi chako hiki kinaweza kuizamisha carrier kama inatokea kushambuliwa na taifa lolote kubwa .
Hebu tuacheni huu ushabiki wa Simba na Yanga kuleta kwenye mambo makubwa hivi. Nakumbuka Patrice Ngoma na Onana wakati wanasajiliwa walitangazwa sana nikajua ni zaidi ya Ronaldo