Baada ya kuruhusu mikutano ya kisiasa, Rais Samia afute Sheria zote, zilizopitishwa katika utawala wa awamu ya 5, zilizotaka kuiua Demokrasia yetu

Baada ya kuruhusu mikutano ya kisiasa, Rais Samia afute Sheria zote, zilizopitishwa katika utawala wa awamu ya 5, zilizotaka kuiua Demokrasia yetu

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Ni dhahiri kuwa Kwa Kila mpenda Demokrasia hapa nchini, anapaswa ampongeze Kwa dhati, Rais Samia Kwa hatua alizochukua za kishujaa za kufutilia Kwa mbali zuio haramu, lililokuwa limewekwa na mtangulizi wake, mtawala wa awamu ya 5. Mwendazake Magufuli, za kupiga marufuku mikutano ya kisiasa ya vyama vya kisiasa nchini

Kama mnakumbuka vizuri Kuna Sheria nyingi zilizokuwa zikipelekwa bungeni, katika kile kilichokuwa kikiitwa miswada ya dharura na kupitishwa "fasta fasta" na waheshimiwa wabunge wetu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa kweli, Kwa mwendo tuliokuwa, tukienda nao, nchi hii ni dhahiri, ingerejeshwa Kwa "mabavu" katika mfumo wa chama kimoja!

Kama nchi naamini tulikuwa tukienda vizuri katika mfumo wa kisiasa wa vyama vingi, hadi mwaka 2015, alipoingia madarakani, Mwendazake Magufuli, ambaye utawala wake, uliamua Kwa makusudi kupiga U turn na kuirejesha nyuma nchi yetu katika kuijenga Demokrasia nchini.

Tukumbuke pia mtawala wa awamu ya 5, alidiriki kutamka hadharani kwenye sherehe za chama Chao Cha CCM, mwaka 2016, zilizofanyika mjini Singida, dhamira yake ya kutaka kuviua Kwa "mabavu" vyama vyote vya upinzani nchini, kuwa ifikapo mwaka 2020!

Vitendo vilivyofuata baada ya kauli yake hiyo, kama vile kumiminiwa risasi 16 mfululizo Kwa kiongozi wa Chadema, Tundu Lissu mwaka 2017, kubambikiziwa kesi mbalimbali Kwa viongozi wengi wa Chadema, vinadhihirisha kuwa kweli mtawala huyo alidhamiria kuviua Kwa "mabavu" vyama vyote vya upinzani, hususani Chadema, ifikapo mwaka aliotabiri yeye wa 2020!

Kwake yeye aliona ni kosa linalofanana na uhaini, Kwa kiongozi yeyote wa chama Cha upinzani, kukosoa sera zake "binafsi" na za chama chake Chake Cha CCM!

Hata hivyo Rais Samia "ametengua" fikra na matendo ya mtangulizi wake, Kwa kutamka kuwa Serikali yake ipo tayari kukosolewa, kwani anaamini kuwa hiyo ndiyo njia pekee ya kuweza wao watawala kuweza kujirekebisha na kuwaletea maendeleo endelevu watanzania.
 
Sheria moja wapo ambayo Kabudi alimshauri mwendazake ni watumishi wa taasisi za Serikali wakiwa na migogoro wasiende CMA..
 
Sheria moja wapo ambayo Kabudi alimshauri mwendazake ni watumishi wa taasisi za Serikali wakiwa na migogoro wasiende CMA..
Duh.........😎

Huo ni mfano mmojawapo wa namna mtawala huyo alivyodhamiria kuiua Demokrasia yetu, ambayo tulifanikiwa kuijenga, tokea nchi yetu irejee kwenye mfumo wa vyama vingi mwaka 1992
 
Zipo Sheria nyingi, zilizotungwa wakati huo, kama vile ya vyombo vya habari na Sheria ya mtandaoni, ambazo zililenga kuua haki ya msingi ya Mwananchi wa nchi hii kuweza kujieleza
 
Hahahaaaa,hahahaaaa,ujinga ni mzigo,hivi nyie mnafikiri chuki zenu kwa jpm zitasaidia?,Samia pia bado ni mkuu wa nchi,zingueni,ATAWAZINGUA
 
Upo sahihi kabisa.

Sheria zile zilizolenga kuimarisha udikteta na kuua demokrasia, kuua uhuru wa maoni, zifutwe/zifanyiwe marekebisho. Sheria hizo ni pamoja na:

1) Sheria ya mitandao na vyombo vya habari

2) Sheria ya takwimu

3) Sheria ya vyama vya siasa

4) Sheria ya kinga ya viongozi kutoshtakiwa iliyoongeza idadi ya viongozi ambao hawawezi kushtakiwa. Sheria ile ilimwongeza Spika na Jaji Mkuu.
 
tukiamua kuingia kwenye demokrasia tuingie wazima wazima sio kihuni uwanja uwe huru.
ila wapinzani wetu nao ni shida,mtu ashakua mbunge wa upinzani anajivua ubunge kuunga mkono juhudi kisha anahamia ccm anagombea tena kwa tiketi ya ccm anashinda hapo pasina shaka amenunuliwa.
 
Lakini Ruto kakataa habari za Siasa baada ya uchaguzi. Sisi tumeruhusu siasa baada ya uchaguzi! Hivi wakenya wakoje lakini?
 
Ni dhahiri kuwa Kwa Kila mpenda Demokrasia hapa nchini, anapaswa ampongeze Kwa dhati, Rais Samia Kwa hatua alizochukua za kishujaa za kufutilia Kwa mbali zuio haramu, lililokuwa limewekwa na mtangulizi wake, mtawala wa awamu ya 5. Mwendazake Magufuli, za kupiga marufuku mikutano ya kisiasa ya vyama vya kisiasa nchini

Kama mnakumbuka vizuri Kuna Sheria nyingi zilizokuwa zikipelekwa bungeni, katika kile kilichokuwa kikiitwa miswada ya dharura na kupitishwa "fasta fasta" na waheshimiwa wabunge wetu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa kweli, Kwa mwendo tuliokuwa, tukienda nao, nchi hii ni dhahiri, ingerejeshwa Kwa "mabavu" katika mfumo wa chama kimoja!

Kama nchi naamini tulikuwa tukienda vizuri katika mfumo wa kisiasa wa vyama vingi, hadi mwaka 2015, alipoingia madarakani, Mwendazake Magufuli, ambaye utawala wake, uliamua Kwa makusudi kupiga U turn na kuirejesha nyuma nchi yetu katika kuijenga Demokrasia nchini.

Tukumbuke pia mtawala wa awamu ya 5, alidiriki kutamka hadharani kwenye sherehe za chama Chao Cha CCM, mwaka 2016, zilizofanyika mjini Singida, dhamira yake ya kutaka kuviua Kwa "mabavu" vyama vyote vya upinzani nchini, kuwa ifikapo mwaka 2020!

Vitendo vilivyofuata baada ya kauli yake hiyo, kama vile kumiminiwa risasi 16 mfululizo Kwa kiongozi wa Chadema, Tundu Lissu mwaka 2017, kubambikiziwa kesi mbalimbali Kwa viongozi wengi wa Chadema, vinadhihirisha kuwa kweli mtawala huyo alidhamiria kuviua Kwa "mabavu" vyama vyote vya upinzani, hususani Chadema, ifikapo mwaka aliotabiri yeye wa 2020!

Kwake yeye aliona ni kosa linalofanana na uhaini, Kwa kiongozi yeyote wa chama Cha upinzani, kukosoa sera zake "binafsi" na za chama chake Chake Cha CCM!

Hata hivyo Rais Samia "ametengua" fikra na matendo ya mtangulizi wake, Kwa kutamka kuwa Serikali yake ipo tayari kukosolewa, kwani anaamini kuwa hiyo ndiyo njia pekee ya kuweza wao watawala kuweza kujirekebisha na kuwaletea maendeleo endelevu watanzania.
Dogo umeonesha udhaifu wa hali ya juu kwenye kujenga hoja. Unasemaje sheria zote zilizowekwa Awamu ya Tano ziondolewe na hujatoa mfano wa sheria hata moja unayotaka iondolewe. Maana yake aidha hazipo au huzijui. Yaani umeropoka!
 
Back
Top Bottom