Baada ya kuthibitika kutumika kisiasa kuikandamiza CHADEMA ni vema Mkurugenzi wa TAKUKURU akajiuzulu

Baada ya kuthibitika kutumika kisiasa kuikandamiza CHADEMA ni vema Mkurugenzi wa TAKUKURU akajiuzulu

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Ni wazi TAKUKURU baada ya kushindwa kubaini makosa kwenye michango ya wabunge wa Chadema , kutokana na kudanganywa na Peter Lijuakali, Mbunge aliyeanza vituko Chadema kutokana na chuki ya kukataliwa kwenye kinyang'anyiro cha uongozi wa Chadema Mkoani Morogoro, ikaanza njama zingine nje ya tuhuma za awali.

Kwa vile TAKUKURU imeamua kutumika kuishambulia Chadema kwa maelekezo ya mwanaccm Lijuakali na kuacha kufuata weledi kama ilivyoainishwa kwenye Katiba ya nchi, na kwa ushahidi mwanana alioweka Katibu Mkuu wa Chadema Mh Mnyika, ambao umeivua nguo Takukuru bila shaka yoyote ni vema basi MKURUGENZI WA TAKUKURU akajiuzulu ili kulinda heshima ya Taasisi ya umma ambayo si mali ya CCM.

Wala asione aibu , atoke tu kama wengine walivyotoka, hakuna atakayemshangaa bali atapongezwa na kujilindia heshima yake .

"Nitasema kweli daima , fitna kwangu mwiko"
 
Taasisi za umma sasa hivi haziwajibiki kwa umma bali zinawajibika kwa rais. Hawawezi kuwajibika maana anayewatumia kwenye siasa chafu anaridhika na huo utekelezaji wa siasa chafu.

Huwa ninasema ukiona Takukuru wanamchukulia mtu hatua ujue huyo sio kipenzi cha rais, au rais ana chuki naye. Tumefikia mahali taasisi ya umma inamtumikia mtu, na sio majukumu yake ya kisheria.
 
Taasisi za umma sasa hivi haziwajibiki kwa umma bali zinawajibika kwa rais. Hawawezi kuwajibika maana anayewatumia kwenye siasa chafu anaridhika na huo utekelezaji wa siasa chafu. Huwa ninasema ukiona Takukuru wanamchukulia mtu hatua ujue huyo sio kipenzi cha rais, au rais ana chuki naye. Tumefikia mahali taasisi ya umma inamtumikia mtu, na sio majukumu yake ya kisheria.
Hakika! Kigwangwala amekutwa wazi wazi akihonga baiskeli na pikipiki huko Nzega akaachwa lakini wanaopeana elfu kumi kumi wanadakwa!
 
Taasisi za umma sasa hivi haziwajibiki kwa umma bali zinawajibika kwa rais. Hawawezi kuwajibika maana anayewatumia kwenye siasa chafu anaridhika na huo utekelezaji wa siasa chafu. Huwa ninasema ukiona Takukuru wanamchukulia mtu hatua ujue huyo sio kipenzi cha rais, au rais ana chuki naye. Tumefikia mahali taasisi ya umma inamtumikia mtu, na sio majukumu yake ya kisheria.
Shida ni kwamba hata mwizi huenda kuiba palipo na cha kuiba!

Kwa hiyo chadema wangekuwa wasafi usingeona takukuru wakiweka kambi kwa muda wote huo hapo chadema!
 
Hakuna taasisi ya kuzuia Rushwa hizi nchi maskin zinajidanganya na ndiko wanasiasa wanakofichia madudu
Haiwezekan TISS hawaend front lkn PCCB wanakwenda
Futa PCCB unda taasisi imara tatu kupambana na uhalifu wa kijamii
1 polisi
2 TISS
3 prosecution office yenye uwezo wa kupeleleza yanyewe
Hapo kila ofisi ikiwa na nguvu ya kwenda front kuchunguza na kufungua mashtaka kwa usaidiz wa prosecution office na ziwepo kila wilaya

Nikiwa rais naifuta TAKUKURU siku hiyo hiyo

Niliwashauri
TAKUKURU mkimaliza CHADEMA hamieni na CCM
 
Ni wazi TAKUKURU baada ya kushindwa kubaini makosa kwenye michango ya wabunge wa Chadema , kutokana na kudanganywa na Peter Lijuakali , mbunge aliyeanza vituko Chadema kutokana na chuki ya kukataliwa kwenye kinyang'anyiro cha uongozi wa Chadema Mkoani Morogoro , ikaanza njama zingine nje ya Tuhuma za awali...
kweli kabisa, hili hata wana CCM wenyewe tumeliona!
 
Msianze kupiga kelele za kujaribu kuingilia uchunguzi.
Haya mambo mtaonekana mnajaribu kuwalinda watu dhidi ya makosa yao flani kama yapo.

Acheni uchunguzi uishe kisha wahusika wasipokuwa na hatia watakuwa wamesafishwa au wakiwa na hatia wataenda kujitetea mahakamani. Mambo kama ndiyo yametufikisha pabaya kwenye rushwa na ubadhirifu wa mali za umma.

Hiki ulichokifanya hapa ni tabia za siasa za CCM ya zamani au siasa za kiafrika za kulinda viongozi wabadhirifu kwa mgongo wa siasa.
 
Msianze kupiga kelele za kujaribu kuingilia uchunguzi.
Haya mambo mtaonekana mnajaribu kuwalinda watu dhidi ya makosa yao flani kama yapo...
Si kweli kabisa ukisemacho , hawa walichokitaka wamepewa na wamehoji zaidi ya watu 60 , wakiwemo hata wanaccm, wamejua kwamba hakuna tatizo lakini bado hawaamini.

kilichoshitukiwa ni kwamba wanatafuta mambo mengine nje ya tuhuma zilizoletwa, kwa hali hii unataka tuwe mabwege na tukae kimya? hebu jaribu kumsikiliza Mnyika labda utaelewa .
 
wamejua kwamba hakuna tatizo lakini bado hawaamini
Umejuaje kama wamekuta hakuna tatizo wakati hawajatoa taarifa(report) yao ya uchunguzi?
Je makosa ya jinai yana mwisho wa uchunguzi?
kilichoshitukiwa ni kwamba wanatafuta mambo mengine nje ya tuhuma zilizoletwa
Je, hayo mambo mengine kama nayo ni ya ubadhirifu au uvunjaji sheria hayapaswi kuchunguzwa? Hauoni kwamba inawezekana baada ya kuhoji hao watu uliosema yakaibuka mambo mengine yanayopelekea uchunguzi zaidi?

Kwani uchunguzi wao ni kesi iliyo endelea mahakamani na kutolewa hukumu hadi ulalamikie kwanini wanaendelea kuchunguza zaidi wakati hukumu ya mwisho ilishatolewa kwa tuhuma ya makosa husika?

Mimi binafsi Bush-lawyer sijaona msingi wowote wa kisheria wa kutoa uhalali wa watu kulalamikia TAKUKURU kufanya uchunguzi zaidi.
 
Back
Top Bottom