Baada ya kuzuia uingiaji na usafirishaji nje bidhaa zifuatazo tumetengeneza faida au hasara?

Baada ya kuzuia uingiaji na usafirishaji nje bidhaa zifuatazo tumetengeneza faida au hasara?

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Tulimzuia Dangote kutoa makaa ya mawe kutoka S.Afrika, je migodi yetu ya makaa ya mawe ipo hali gani leo? Kutoka kwenye lesson leant tunaamni mawazo yetu yalikua sahihi?

Tulidhibiti usafirishaji wa mazao ya chakula nje hasa Kenya ambayo inategemea chakula kutoka kwetu, je Hali ya soko la ndani ipo vipi? Kenya bado wanatutegemea au wametafuta soko la vyakula Mataifa mengine? Je, mkakati wakudhibiti mahindi na mazao mengine kwenda Kenya vina tija?

Tulidhibiti uuzaji wa korosho serikali ikaanza kununua yenyewe huku wakulima wakilazimishwa kusubiri mnada hata kama wanataka kuuza japo kilo kumi walipe ada za watoto. Mfumo huu baada yamajaribio bado una tija au tunatakiwa kutafuta mfumo mbadala?

Tumepandisha Kodi kubwa kwa bidhaa zinazotoka nje vikiwemo vitenge na kana ili kuvisaidia viwanda vya Mo na vingine vya ndani viweze kukua na kupata soko. Je bado tunaamini viwanda vyetu vinauwezo wakuzalisha quality product au ushindani kutoka nje unahitajika? Kwanini wafanyabiashara wanazidi kuagiza mzigo kutoka nje pamoja na bei kuwa juu? Mkakati huu bado unatija au Waziri wa viwanda anatakiwa kutafiti upya na kuja na suluhu?

Elimu ni bidhaa na pia ni huduma, tumewabana shule binafsi wasitoe huduma hii kwa Watanzania kwa lengo lakukuza shule za serikali lakini watoto wote wa vigogo na wafanyabiashara au watu wanaojiweza wanasoma private school, je lengo la serikali kamaalikueleweka na watumishi wa Umma watunga sera litaeleweka kweli kwa wananchi wakawaida? Kwanini tusiacha huduma na bidhaa hii ya elimu iwe yaushindani huru?

Tumeanza kudhibiti uingizaji magari kwa lengo lakutafuta pesa ya ukaguzi iliyokuwa inakwenda kwa makampuni ya nje, je Intelligence inasemaje kuhusu mwitokio wa wanannchi? Kwanini tangazo lile limeleta mshtuko mkubwa? Je bandarini Kuna garage na rasilimali watu kutoka serikalini wenye uwezo wa kukagua na kutengeneza hayo magari? Je mipaka mingine haitaruhusiwa kuingiza magari yaliyoshuka nchi jirani?.

Tuwe na tabia yakibiashara, ukijaribu mkakati huu ukashindwa usiwe mgumu kukubali mapungufu nakuja na mkakati mpya, tujifunze kujifunza kutoka field tutoke maofisini.
 
Yaliyotokea kwa korosho pia yametokea kwa Kahawa. Baadhi ya Wakulima wana miezi 6 hawajàlipwa. Mfumo Wa ushirika una dosari kubwa
 
Biashara za cement,sukari,mafuta ya kupikia serikali ilipo ingiza mikono yake michafu tunaoumia ni sisi tunaoitwa wanyonge
Nani Sasa hivi anaweza kujenga kwa mshahara wa kima cha chini?

Aaagh tuseme nini ikiwa washauri wa uchumi ni watu aina ya Joseph Kasheku Musukuma
 
... ili tuendelee, Mwalimu alisema, tunahitaji vitu vinne vya msingi - ardhi, watu, siasa safi, na uongozi bora. Hayo mawili (ardhi na watu) yapo tele; sasa tunafeli wapi? Kwa kanuni ya Mwalimu siasa safi na uongozi bora ndipo tunapokwama!

Uongozi bora ni pamoja na kutunga na kusimamia sera zitakazolipelekea taifa mbele; sera ya elimu inayolenga ku-impart knowledge kwa watu (maendeleo ya watu - Lissu) ili waweze kubadili mazingira na raw materials into valuable outputs. Wachina na wahindi walifika hapo walipo kwa kuwekeza sana kwenye maendeleo ya watu wao kielimu; leo hii tunaishangaa China kwa kasi ya maendeleo waliyo nayo.

Juzi mwisho wa mwaka nilienda kuwatembelea mababu na mabibi zangu kule kijijini; bei kwa mfano ya ngozi ya ng'ombe utashangaa! Tanzania ni ya 3 Afrika kwa mifugo mingi, ilitakiwa tuwe among producers and exporters of the best leather products - viatu, mikoba, n.k. Watu wetu wanavaa yebo yebo huku ngozi ya ng'ombe kule kijijini ikiuzwa sio zaidi ya TZS 400 (mia nne) tu!

Tulitakiwe tuwe among the producers of the best cotton products; beverages; fruits and vegetables. Leo hii Tanzania ni ya kulialia uhaba wa mafuta ya kula? Sukari? Shame on us.
 
Huu nao ni udhihirisho kuwa chama chenu ni CHAMA CHA MAZEZETA. Madarasa hayatoshi mnaenda kununua ndege ambazo hazina faida yoyote bali Ni gharama kubwa sana kwa taifa
Bawacha ndio kambi kuu ya upinzani bungeni!

Nawatakia Dominica yenye baraka.
 
Mi[emoji113]tena!
IMG_20210123_192340.jpeg
 
... ili tuendelee, Mwalimu alisema, tunahitaji vitu vinne vya msingi - ardhi, watu, siasa safi, na uongozi bora. Hayo mawili (ardhi na watu) yapo tele; sasa tunafeli wapi? Kwa kanuni ya Mwalimu siasa safi na uongozi bora ndipo tunapokwama!

Uongozi bora ni pamoja na kutunga na kusimamia sera zitakazolipelekea taifa mbele; sera ya elimu inayolenga ku-impart knowledge kwa watu (maendeleo ya watu - Lissu) ili waweze kubadili mazingira na raw materials into valuable outputs. Wachina na wahindi walifika hapo walipo kwa kuwekeza sana kwenye maendeleo ya watu wao kielimu; leo hii tunaishangaa China kwa kasi ya maendeleo waliyo nayo.

Juzi mwisho wa mwaka nilienda kuwatembelea mababu na mabibi zangu kule kijijini; bei kwa mfano ya ngozi ya ng'ombe utashangaa! Tanzania ni ya 3 Afrika kwa mifugo mingi, ilitakiwa tuwe among producers and exporters of the best leather products - viatu, mikoba, n.k. Watu wetu wanavaa yebo yebo huku ngozi ya ng'ombe kule kijijini ikiuzwa sio zaidi ya TZS 400 (mia nne) tu!

Tulitakiwe tuwe among the producers of the best cotton products; beverages; fruits and vegetables. Leo hii Tanzania ni ya kulialia uhaba wa mafuta ya kula? Sukari? Shame on us.
Tanzania binadamu wako 60m lakini Watu ni wachache sana!
 
Roho mbaya ikamfanya kunyima Kenyatta mahindi wakulima wetu mahindi yakawaozea hawana pa kupeleka,Kenya wakaona isiwe tabu wakachukua mahindi zambia,wabongo wachache wakaona fursa hio wakakodi malori yenye usajili wa zambia wakapakia mahindi wakapeleka kenya,wamekuja ruhusu kuuza kenya fursa ikiwa imeshatupita mahindi ya zambia yamejaa kenya huku soon Kenya wapo kwenye msimu wa kuvuna mahindi.Wanasiasa wachache wasio na maono wapo radhi kuwanyima wakulima fursa nje sababu ya bifu zao Hali wao wanasaza kodi zetu.
 
If you fail to plan you plan to fail. In a silver jubilee of independence we still even don't know our priorities.
 
Wenzetu waliyaona haya thus awatoi leseni za udereva kwa mtu masikini ili asiangushe gari.
Madereva wazuri utokea kwenye fani hizi uchumi, biashara, international relations, sheria, maendeleo ya Jamii.
Kuendesha gari kunataka akili na sio nguvu.
 
Huyu mawazo yake yako kujenga . mengine hayamhusu sana
 
Ni kweli suala la biashara limekuwa changamoto. Hata wakulima wengi wanalia kutokana na kutokuuza mazao nje ya nchi, pamoja na kusema kwamba mazao ya vyakula yabaki ndani ya nchi ila watu hawana ela mfukoni kwa sasa
 
Back
Top Bottom