Baada ya makundi kupangwa CAF, washabiki wa Simba na Yanga wanaombeana mabaya. Hii ni aibu!

Baada ya makundi kupangwa CAF, washabiki wa Simba na Yanga wanaombeana mabaya. Hii ni aibu!

covid 19

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2014
Posts
6,967
Reaction score
17,452
Kwa heshima kubwa na kwa lengo la kuleta mafanikio kwa soka la Tanzania, ni wakati wa kuangalia mbali zaidi ya migawanyiko ya kiushabiki baina ya klabu na kuanzisha ushirikiano imara baina ya timu kubwa mbili za mpira wa miguu nchini, Simba na Yanga.

Katika hali ya mpira wa ushindani kuelekea mashindano ya champion CAF, napendekeza wakubwa wetu hawa wa soka nchini wajiunge nguvu katika mechi za kimataifa ili kuleta heshima na sifa kwa nchi yetu, Tanzania.

napendekeza Simba na Yanga zitafute njia za kushirikiana katika maandalizi, mafunzo, na ushirikiano katika mechi za kimataifa. tunaweza kuona mafanikio makubwa zaidi ya soka la Tanzania katika jukwaa la kimataifa.

Mimi nitoe wito kwa viongozi wa Simba na Yanga, wachezaji, na mashabiki kuchukua hatua za kuanzisha ushirikiano huu muhimu hasa kipindi hiki. Ni muda sasa kuweka tofauti za klabu na kujitolea kwa pamoja kwa ajili ya maendeleo ya soka letu na kuiwakilisha vyema Tanzania katika jukwaa la kimataifa.

Tanzania inaweza kuwa na sauti kubwa katika soka la kimataifa, na ushirikiano wa Simba na Yanga unaweza kuwa hatua kubwa katika kufikia lengo hilo. Tufanye kazi pamoja kwa lengo letu kubwa la kuiletea Tanzania heshima kupitia soka letu.
 
Hata Liverpool hawezi kuwaombea mema Manchester United

Ama Arsenal kuwaombea mema Tottenham hotspur

Ukisikia watani wa Jadi ndiyo hao
 
Mkuu huu ni ulimwengu wa soka na sio ulimwengu wa siasa.

Uzarendo upo timu ya taifa na sio virabu.
 
Sio Aibu, ni watanzania ndio walivyo ,mie pia mwanzo nilikua nashangaa kama wewe

Watanzania hawapendani,wanafiki
 
Simba wabadilike,wapo slow na soft sn.Wanatakiwa kuongeza kasi na uimara(ngangari) kwa wachezaji.

Vinginevyo hawatafua dafu kabisa.

Yanga spirit yao na speed wakiiongeza kidogo watawaduwaza wapinzani ktk group na watu watashangaa
 
Binafsi siwezi kuwaombea mema Simba.

Nibora inchi iendelee kuwa kichwa cha mwenda wa zimu, lakini sio kuwaombea Simba mafanikio, nasema sipo tayari.
 
Sio Aibu, ni watanzania ndio walivyo ,mie pia mwanzo nilikua nashangaa kama wewe

Watanzania hawapendani,wanafiki
Tukutane timu ya Taifa, lakini sio kwenye ngazi ya vilabu, katika hilo mutanisameh.
Nishangilie Simba!!? Mh, haiwezekani.
 
IMG-20231006-WA0118.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom