Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakati Serikali ya Marekani chini ya Rais Donald Trump ikikata misaada yake kwa mataifa mengine, Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Marianne Young, amesema nchi yake itaendelea kutoa misaada ya kimaendeleo na kibinadamu kama sehemu muhimu ya ushirikiano wa kimataifa.
Balozi Young amebainisha hayo wakati wa mahojiano maalumu na Mwananchi Jumatatu, Februari 17, 2025, akizungumzia athari za mabadiliko ya sera za kimataifa katika misaada ya kigeni. Ameangazia athari kwa Tanzania na jumuiya ya wafadhili wa kimataifa.
Tangu ameingia madarakani, Januari 20, mwaka huu, Trump alitia saini amri kadhaa za kiutendaji ikiwemo ya kusitisha kwa muda misaada ya kimataifa inayotolewa na shirika la USAID, jambo ambalo limesababisha mamia ya watu kupewa likizo ya bila malipo.
Akizungumzia uamuzi huo wa Marekani, amesema wanatambua Marekani imesitisha utoaji misaada hadi watakapofanya tathmini, hata hivyo amesema Serikali ya Uingereza itaendeleza dhamira yake thabiti ya kutoa misaada ya kimaendeleo na kibinadamu kama sehemu muhimu ya ushirikiano wa kimataifa.
“Tunaamini kwamba hatua shirikishi kati ya washirika wa kimataifa ni muhimu kwa ajili ya kuendeleza viashiria muhimu vya maendeleo, ikiwa ni pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs),” alisema Balozi Young.
“Mbali na ufadhili huo, pia tunatumia fedha zinazotolewa na serikali kupitia uwekezaji wa kimataifa wa Uingereza, ambayo imekuwa mdau mkuu nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 50. Kwa sasa, mfumo wetu una pauni 50 milioni (Sh655 bilioni), na tunalenga kuongeza hii maradufu hadi pauni milioni 200 katika miaka michache ijayo.
“Pia, tunazingatia kutumia fedha binafsi. Hili ni eneo muhimu ambapo serikali ya Uingereza inashirikiana kikamilifu na taasisi za kimataifa ili kuongeza msaada wa kifedha na kushughulikia upungufu wa ufadhili uliopo,” amesema.
Source: Mwananchi
Balozi Young amebainisha hayo wakati wa mahojiano maalumu na Mwananchi Jumatatu, Februari 17, 2025, akizungumzia athari za mabadiliko ya sera za kimataifa katika misaada ya kigeni. Ameangazia athari kwa Tanzania na jumuiya ya wafadhili wa kimataifa.
Tangu ameingia madarakani, Januari 20, mwaka huu, Trump alitia saini amri kadhaa za kiutendaji ikiwemo ya kusitisha kwa muda misaada ya kimataifa inayotolewa na shirika la USAID, jambo ambalo limesababisha mamia ya watu kupewa likizo ya bila malipo.
Akizungumzia uamuzi huo wa Marekani, amesema wanatambua Marekani imesitisha utoaji misaada hadi watakapofanya tathmini, hata hivyo amesema Serikali ya Uingereza itaendeleza dhamira yake thabiti ya kutoa misaada ya kimaendeleo na kibinadamu kama sehemu muhimu ya ushirikiano wa kimataifa.
“Tunaamini kwamba hatua shirikishi kati ya washirika wa kimataifa ni muhimu kwa ajili ya kuendeleza viashiria muhimu vya maendeleo, ikiwa ni pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs),” alisema Balozi Young.
“Mbali na ufadhili huo, pia tunatumia fedha zinazotolewa na serikali kupitia uwekezaji wa kimataifa wa Uingereza, ambayo imekuwa mdau mkuu nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 50. Kwa sasa, mfumo wetu una pauni 50 milioni (Sh655 bilioni), na tunalenga kuongeza hii maradufu hadi pauni milioni 200 katika miaka michache ijayo.
“Pia, tunazingatia kutumia fedha binafsi. Hili ni eneo muhimu ambapo serikali ya Uingereza inashirikiana kikamilifu na taasisi za kimataifa ili kuongeza msaada wa kifedha na kushughulikia upungufu wa ufadhili uliopo,” amesema.
Source: Mwananchi