Baada ya Matokeo ya jana: Mwanachama Agnatius Obel aibuka na haya

Baada ya Matokeo ya jana: Mwanachama Agnatius Obel aibuka na haya

grafani11 nina swali,kwa nini watu wenye pesa wasajili na sio timu?

cc Masuke Amavubi sembo barafuyamoto Sibonike

Sababu kubwa itakayotolea hapa ni kwamba team haina hela, lakini nani anayejua kwamba team ina hela au haina maana mwenye uwezo wa kujua ni kiasi gani kipo kwenye account ya klabu ndo huyo atakayekwambia team haina hela.

Sio vibaya viongozi kusaidia kupatikana kwa wachezaji, na hii ingekuwa ni nzuri zaidi endapo ingefanywa na watu maalum ambao wameajiriwa kwa ajili ya kufuatilia wachezaji wanaowahitaji. Ubaya wake unakuja pale kiongozi anaposajili na kuamua kummiliki mchezaji moja kwa moja badala ya kuiachia team immiliki.

Toka jana nasema huo mfumo wa kamati ni wa nini? Hizi kamati ndo zinazoharibu kila kitu, kuna haja ya kuwa na viongozi wa juu wawili, m/kiti na katibu na wajumbe kama wanne tu au watano, ondoa kamati zote hizo.
 
Last edited by a moderator:
friends of simba wanaharibu timu
Kwa hiyo unataka tuwaite 'enemies of simba'!?
Wote hata tunajadili matokeo ya tatizo, tatizo likiwa kuwa wanaosababisha hili tatizo ndio pia wanatagulizwa mbele kulitatua!
 
Mkuu grafani11 hapa sibonike kaelezea point ya msingi sana.NA HII NDIO ROOT CAUSE YA HAYA YOTE.

Tukitaka simba iwe timu inayoheshimika na yenye pesa na inayoendeshwa kisomi lazima ifanye kazi "independently".

Tusemezane ukweli......Viongozi wana maslahi yao binafsi.

Timu inahitaji aina mpya ya ufikiriaji...hawa waliopo kina Dewji wa Tangu enzi zile hakuna kipya.................

Mfumo wa uendeshaji inabidi ubadilishwe

TATIZO NI...NANI MWENYE UWEZO WA KUWAWEKA HAWA MATAJIRI PEMBENI?


Ni wanachama wenyewe. Sisi ndio tunachagua viongozi. Kwa njaa zetu (baadhi) tunachagua baada ya kupewa pipi ! (ndio pipi maana sina namna nyingine ya kueleza).

Angalia mfumo wa Spain (Barcelona na Real Madrid) ni tofauti na Uingereza ambako ni kampuni per se. Kule Spain wanachama (wanajitambua) ndio hupiga kura kupata viongozi - Rais wa Club ambaye huajiri watendaji.

Mfumo huu wa sasa wenye madhara makubwa utaendelea hadi wanachama wa vilabu tujitambue na kuweka viongozi wataosaidia kuleta mfumo bora. Najua tuna safari ndefu. Siku ya uchaguzi ndio matapeli yanawalipia wanachama kadi zao ili waweze kupiga kura ya kuwachagua!

Kila mwana Yanga au simba akichanga fee ya mwaka kwa Tanzania nzima, club inapata kiasi gani? Ongeza udhamini (TBL, Tv nk ) na viingilio. Hapo kuna haja ya kumpigia mtu magoti?
 
Nakubaliana na maoni yako yote isipokua hili la "Wenye Pesa"

Simba iko na hali mbaya kwa sasa kwa sababu ya kuwategemea hawa "Wenye Pesa"

Kuna kipindi hawa wenye pesa hawakuwepo kwenye timu na timu ilifanya vizuri sana....hebu tumuulize Masuke kipindi cha Kaduguda simba ilikuwaje?

Simba inatakiwa ijisimamie kama timu...kwa pesa za timu...isitegemee mtu...hapo tunaweza kwenda proffesionally

Kipindi cha Kaduguda mchango mkubwa wa kifedha ulikuwa unatolewa na Dioniz Malinzi, kaka yake Jamal Malinzi. Nadhani kwa sasa ni m/kiti wa BMT. Sina hakika sana kama alikuwa anasaidia tu for good faith au alikuwa mfadhili, sikuwahi kuona jezi imeandikwa Cargo Stars. Na wakati ule kama kumbukumbu zangu ziko sawa kuna ama Simba Cement ama NBC waliinject hela yao pale. Mambo hayakuwa mazuri sana ila tatizo lilikuwa ni hawa jamaa wa FoS na vyombo vya habari, walikuwa hawapatani na Kaduguda.
 
Last edited by a moderator:
Ni wanachama wenyewe. Sisi ndio tunachagua viongozi. Kwa njaa zetu (baadhi) tunachagua baada ya kupewa pipi ! (ndio pipi maana sina namna nyingine ya kueleza).

Angalia mfumo wa Spain (Barcelona na Real Madrid) ni tofauti na Uingereza ambako ni kampuni per se. Kule Spain wanachama (wanajitambua) ndio hupiga kura kupata viongozi - Rais wa Club ambaye huajiri watendaji.

Mfumo huu wa sasa wenye madhara makubwa utaendelea hadi wanachama wa vilabu tujitambue na kuweka viongozi wataosaidia kuleta mfumo bora. Najua tuna safari ndefu. Siku ya uchaguzi ndio matapeli yanawalipia wanachama kadi zao ili waweze kupiga kura ya kuwachagua!

Kila mwana Yanga au simba akichanga fee ya mwaka kwa Tanzania nzima, club inapata kiasi gani? Ongeza udhamini (TBL, Tv nk ) na viingilio. Hapo kuna haja ya kumpigia mtu magoti?


Precise

Lakini pia how if timu ikiuza shares 50% ika raise funds za kutosha .Kwa value ya shares za simba najua IPO yake itatengeneza billions.

Hizo billions zinaweza kutumika kufinance projects nyingi za timu

Hio 50% inaweza kufanya majority shareholder awe na say katika timu.

50% zinazobaki zinaweza kumilikiwa na wanachama.

Issue hapa ni kuifanya timu ijiendesh yenyewe.

Kama ulivyosema michango tu na fedha za wadhamini zinatosha kulipa mishahara yote ya mwaka mzima na kambi ya timu kwa mwaka mzima...sasa iweje waseme timu haina hela?
 
Precise

Lakini pia how if timu ikiuza shares 50% ika raise funds za kutosha .Kwa value ya shares za simba najua IPO yake itatengeneza billions.

Hizo billions zinaweza kutumika kufinance projects nyingi za timu

Hio 50% inaweza kufanya majority shareholder awe na say katika timu.

50% zinazobaki zinaweza kumilikiwa na wanachama.

Issue hapa ni kuifanya timu ijiendesh yenyewe.

Kama ulivyosema michango tu na fedha za wadhamini zinatosha kulipa mishahara yote ya mwaka mzima na kambi ya timu kwa mwaka mzima...sasa iweje waseme timu haina hela?


Hilo ni zuri na linawezekana but lazima mfumo wa kampuni uje kwanza ndio mengine yafuate. Zitauzwa shares za kampuni. Wanachama wapewe nafasi ya kununua share zao ingawa hapa kuna mtihani kwa wale wanaolipiwa ada ya mwaka ili wapige kura.
 
Na Saleh Ally
KOCHA wa zamani wa Yanga, Ernie Brandts huenda ndiye aliyeongoza kwa kulalamika kwamba anashindwa kutoa kila alichokuwa nacho kiuwezo kwa kikosi chake kutokana na ubovu wa kupindukia wa miundombinu.



Brandts raia wa Uholanzi, haikuwa mara yake ya kwanza kufundisha soka Afrika. Alifanya kazi nchini Rwanda kwa zaidi ya misimu mitatu, tena kwa mafanikio makubwa.


Beki huyo wa zamani, alidai Yanga ilishindwa hata kumnunulia magoli madogo kwa ajili ya kupambana na zoezi la ubutu wa utumiaji nafasi, viongozi walimuahidi kila siku jua lilipochomoza, wakampotea jua lilipochwea.


Miaka saba iliyopita, Kocha Nielson Elias raia wa Brazil, aliamua kuondoka Simba baada ya kugundua timu haikuwa hata na uwanja wa mazoezi na kusema anaamini timu hiyo haitafika popote hadi itakapopata uwanja.


Karibu kila kocha kutoka nje ya Tanzania amelalama kuhusiana na uwanja kwa kuwa Yanga na Simba zenye tofauti ya mwaka mmoja tu kiumri, moja ikiwa na miaka 80 na nyingine 79, bado hazijui zinachokifanya.


Bara:
Wako wanaoshangaa Mtibwa Sugar, Azam FC kuonyesha soka bora kuliko Yanga au Simba. Wanasahau timu hizo ziko ‘busy' na soka kwelikweli.


Azam FC au Mtibwa Sugar zinamiliki viwanja vyake zinavyovitumia kwenye ligi pia. Haziwezi kupangiwa mazoezi kama ilivyo kwa Yanga au Simba zinazotangatanga na wakati mwingine kufanyia mazoezi kwenye viwanja vibovu kama Tanganyika Packers, Bora Kijitonyama au Loyola Sekondari.


Timu hizo kongwe ziko busy na viwanja vya shule, vya timu za daraja la tatu au vinavyomilikiwa na timu za veterani. Jamani, hadi veterani wana uwanja wao wa mazoezi, Yanga na Simba hawana!


Timu nyingi za mikoani zina viwanja bora vya mazoezi. Hata kama utasema zitacheza ligi kwenye viwanja vingine visivyokuwa na ubora lakini ukweli zitakuwa zimefanya mazoezi bora kwa wakati wa kutosha na zinakuwa tayari kukabiliana na lolote kwa stamina na pumzi, ndiyo maana zinaweza kupambana mwanzo mpaka mwisho tofauti na Simba na Yanga.


Usilalamike Yanga au Simba kutokuwa na stamina. Mazoezi ya gym nayo ni ya kuibia kwa kuwa lazima zilipie kwenda, kweli kwa miaka yote zimeshindwa kuwa hata na chumba cha gym na vifaa vyake!


Hivi viongozi wa klabu hizo hawaoni au wanafumba macho kwa kuwa wanajua wanafanya siasa na si masuala ya mpira?


Wachezaji wa Yanga na Simba wana nafasi ya kuwa na majina makubwa lakini wasiwe na soka kubwa.


Azam FC imepambana ndani ya miaka minne imebeba ubingwa wa Tanzania tena kabla ya hapo ikiwa imeshika nafasi ya pili mara mbili mfululizo.


Inawezekana kuna wakati Azam FC wanakosea, lakini lazima tukubali hatua wanazopiga kwa vitendo, baadaye watakuwa imara kuliko timu nyingine halafu tutawasingizia mengine wakati ukweli tunaona sasa.


Afrika:
Simba na Yanga ni timu zenye ndoto ya kufanya vema katika michuano ya Afrika, hasa ile iliyo chini ya Shirikisho la Soka Afrika (Caf).


Jiulize, kwa timu yenye miaka 80 au 79, halafu haina hata uwanja wa Mazoezi inawezekana vipi? Nani anaamini Yanga na Simba zinaweza kucheza soka bora kushindana na timu kama Enyimba ya Nigeria, TP Mazembe au AS Vita ya DR Congo huku zikiwa hazina hata uwanja wa mazoezi!


Timu hizo mbili za Tanzania si timu zenye ndoto ya kufanya vema. Mtu anayetaka kutimiza ndoto zake ni yule anayepiga hatua baada ya hatua akienda anakotaka kufanikiwa.


Kushindwa leo, ukijipanga upya na kupambana tena hadi ukafanikiwa ndiyo sehemu ya ubora. Hauwezi kusema timu isiyo hata na uwanja wa mazoezi ina ndoto za kuwa bingwa wa Afrika, kitakuwa kichekesho cha karne.


Yanga na Simba ni roli aina ya Scania lenye injini ya Volkswagen Beatle maarufu kama mgongo wa chura.


Scania yenye injini ya mgongo wa chura, ikiwa na mzigo mkubwa halafu inataka kupanda mlima, jiulize mara mbili, nini kitafuatia?


Hadithi za Yanga na Simba hata kuwa na uwanja wa mazoezi tu, umezisikia tokea lini? Hata mimi hii si mara yangu ya kwanza kuandika, hawa watu ni wa aina gani hadi hawaelewi!


Hili suala la kusisitiza Yanga na Simba wanapaswa kuwa na uwanja, kweli wao hawajui! Huo ni wajibu wao na wanajua umuhimu wake.


Leo Yanga na Simba wanasema wanakuza vijana, eti wana timu B. Wakati mwingine ni kichekesho tu kulazimisha kukuza watoto wanaotumia viwanja vyenye mabonde, vikavu.


Kweli watakuaa, wachache wasiokata tamaa wataonekana lakini kuna mengi wanakosa kama suala la vifaa na hasa viwanja lingepewa kipaumbele na wao kukua kwenye misingi sahihi.


Usisahau kuwa afya za wachezaji kwa maana ya magoti, enka, nyama za paja na vinginevyo haziko salama.


Ukitaka kunielewa zaidi baada ya mazoezi, angalia viatu vya Haruna Niyonzima wa Yanga na Jonas Mkude wa Simba, fananisha na cha Didier Kavumbagu wa Azam FC au Ame Ali wa Mtibwa Sugar.
 
Kipindi cha Kaduguda mchango mkubwa wa kifedha ulikuwa unatolewa na Dioniz Malinzi, kaka yake Jamal Malinzi. Nadhani kwa sasa ni m/kiti wa BMT. Sina hakika sana kama alikuwa anasaidia tu for good faith au alikuwa mfadhili, sikuwahi kuona jezi imeandikwa Cargo Stars. Na wakati ule kama kumbukumbu zangu ziko sawa kuna ama Simba Cement ama NBC waliinject hela yao pale. Mambo hayakuwa mazuri sana ila tatizo lilikuwa ni hawa jamaa wa FoS na vyombo vya habari, walikuwa hawapatani na Kaduguda.

Ukijaribu kuangalia hapa maadui wa Simba ni hawa wanaojiita FOS.Hawa ndio tatizo la mabadiliko
 
Ndio maana nikasema ni 'brilliant idea' mkuu. Ni sawa na kumpatia mtu gari katika nchi ambayo magari hayajawahi kuwepo kabisa, hakuna barabara, spare parts, mafundi, petrol stations nk. Kibaya zaidi hii gari uchomoe hata matairi alafu unamwachia mtu kwa ajili ya matumizi katika mazingira hayo hayo. Kuna gap kubwa hapa kati ya gari aliyoachiwa mtu na mtumiaji mtarajiwa. Huo ndio ukubwa wa hizi timu na wanachama wake.
Mfano wa timu hizi ni pale Mengi alipotumia muda mwingi sana sio kama mwanachama bali kama mjuzi wa biashara kuwapiga msasa Yanga ni jinsi gani wangeliweza kuibadili timu kutoka kwenye 'uombaomba' mpaka kwenye kugawana dividends za shares. Ni chini ya 5% ya waliomuelewa alichokuwa anawaeleza kabla na yeye kuamua 'kujitoa'. Kumbuka Mengi huyu huyu (forget about his negative side of life maana ni binadamu) alipoleta wazo la SKUVI miaka ya 90 mwanzoni, wengi wetu hatukuelewa alichokuwa akiaddress lakini nasikia kuna baadhi ya waliomsikiliza na sasa hivi ni matajiri wakubwa katika miradi ile ile aliyowaelekeza.
Samahani kutumia mfano wa mtu mmoja lakini nia yangu sio kumsifu bali kukuonyesha jinsi watu wanaojiita 'wanachama' wa Simba/Yanga walivyo wagumu kubadilika ili nawe ujue kitu unachokiongea cha kuleta mabadiliko kilivyo kigumu huko!


Una wazo zuri sana mkuu lukindo

Structure yetu inaweza sana kuendana na klabu za Hispania

Tunatakiwa kuiga mfumo ule

Tukitenga 50 % shares tukauza....tuna uwezo wa ku raise billions....at least tuwe na facilities zetu kama uwanja wa kawaida na hostels pamoja na vitega uchumi.

Tuweze kuwa na mechanism ya ku control bidhaaa za timu.

Kama tutaweza kuifanya simba ikawa na mafanikio ya kibiashara tutawavutia sponsors wakubwa ambao nao watabenefit na ukubwa wetu.

Ila ili kufanya yote haya simba inabidi iwe a person (Iwe kampuni inayosimama yenyewe kama yenyewe).Iajiri wafanyakazi.

Nakumbuka kauli ya Wambura kwamba simba inahitaji wadhamini sio wafadhili.
 
Last edited by a moderator:
Huku mikia wakiendelea kuumiza vichwa, Selemani Matola ameomba aachie ngazi. Tunaendelea kusubiri makubwa zaidi, yetu masikio na macho.
 
Tatizo kubwa la timu yetu ya Simba liko uwanjani. Team haina stamina kabisa, hususani 2nd half ikifika dk ya 60 kwenda mbele karibia players wote wa SSC wanakuwa wamechoka.

Kwa hili pia namlaumu kocha Phiri maana ndie aliyeiandaa timu tena alikaa nayo kambini karibia miezi miwili yaani majuma 8, kwann mpaka leo SSC hatuna pumzi uwanjani? Hata Mtemi Ramadhani kaongea jana inasemekana players hawataki mazoezi magumu,nilishangaa kidogo kuwa wanagomea mazoezi au wanadanyia kuumwa pindi mazoezi yakizidi ugumu? Ni vigumu sana kocha kufanyisha mazoezi magumu ya pumzi wakati timu ipo kwny mashindano.

Suala la Danny Serunkuma, me ntakuwa tofauti na wadau wengi kidogo. Me namuona kamabado ni mchezaji muhimu kwetu na anasaidia sana timu kukaa na mpira mbele. Kutolewa kwake pia inaweza kuwa sababu ya kufungwa juzi na MCC maana mpira ulikuwa haukai mbele kabisa, atakayebisha abishe lakini afuatilie kwanza kwa makini.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, kuhusu HP kumuingilia mwalimu, je anakuwa anamuingilia pale timu inapofanya vibaya tu? Katika kipindi kimoja cha michezo HP aliwahi kuhojiwa kuwa "Inasemekana wewe na wenzako mnamuingilia mwalimu katika kutekeleza majukumu yake" alijibu kwamba hakuna anayemuingilia mwalimu ktk kazi yake isipokuwa tunapoona mambo tofauti lazima tutoe ushauri, akatolea mfano mechi ya Simba v Yanga ile 2liyokuwa nyuma 0-3 HT then tukaja kurejesha zote 3. Anasema wakati wa mapumziko waliingia changing room Kibadeni aliwaambia wachezaji kuwa mmeshafungwa goli 3 basi msiruhusu mengine, lakini wao wakamshauri mwalimu afanye mabadilikom kwani kiungo kimekufa kabisa Humud lazima apumzishwe. Kweli mabadiliko yalifanyika Ndemla na Lucian waliingi wakabadilisha game goals 3 zikarudi, Je kuna ubaya gani hapo.

Kipindi cha uongozi wa Rage ni mara ngapi alikuwa anazikimbia mechi za Simba 2napotaka kucheza na Yanga? Tena wakati mwingine anaenda nje ya nchi kabisa na kuiacha timu ikikabiliwa na khali ngumu ya kifedha madeni kwa wachezaji na ikikabiliwa na mchezo muhimu dhidiya Yanga. Ni hawa hawa kina HP ndo walikuwa wanasimamia kambi ya timu, kulipa madeni ya wachezaji na hatimae 2nafurahia ushindi wote pamoja dhidi ya mtani wetu au anafurukuta anapata sare.

Kama kuna mtu alikuwepo Taifa siku ile game ya 3-3 na Yanga, kabla ya game Manji alisimama alikuwa na Sanga akawanyanyua wana Yanga akawa anaonyesha vidole vi3 na Yanga wakalipuka sana sie tukanywea kabisa hadi alipoibuka HP nae akatuinua wanasimba akaonyesha vidole vi5 tukalipuka mara mbili yao, mnakumbuka? Rage alikuwa wapi siku ile?

Watu wanaweza kuwa wanafanya vitu kwa good faith but changamoto ni nyingi mno katika soka la sasa, kila timu inawezeshwa hivyo zinajiandaa kikamilifu.

Kaburu nasikia hana mawe siku hizi, hivyo hatoi hela pale SSC.

Tayari kocha kamtaja Kaburu kuwa ndiye anayempigiaga simu kumwambia wachezaji wa kuwapanga, kocha alitishia kuacha kazi au kumtukana kiongozi yeyote atakayefanya hivyo. Source: Bin Zubeiry(naiamini souce)
 
Kipindi cha uongozi wa Rage ni mara ngapi alikuwa anazikimbia mechi za Simba 2napotaka kucheza na Yanga? Tena wakati mwingine anaenda nje ya nchi kabisa na kuiacha timu ikikabiliwa na khali ngumu ya kifedha madeni kwa wachezaji na ikikabiliwa na mchezo muhimu dhidiya Yanga. Ni hawa hawa kina HP ndo walikuwa wanasimamia kambi ya timu, kulipa madeni ya wachezaji na hatimae 2nafurahia ushindi wote pamoja dhidi ya mtani wetu au anafurukuta anapata sare.

Kama kuna mtu alikuwepo Taifa siku ile game ya 3-3 na Yanga, kabla ya game Manji alisimama alikuwa na Sanga akawanyanyua wana Yanga akawa anaonyesha vidole vi3 na Yanga wakalipuka sana sie tukanywea kabisa hadi alipoibuka HP nae akatuinua wanasimba akaonyesha vidole vi5 tukalipuka mara mbili yao, mnakumbuka? Rage alikuwa wapi siku ile?

Watu wanaweza kuwa wanafanya vitu kwa good faith but changamoto ni nyingi mno katika soka la sasa, kila timu inawezeshwa hivyo zinajiandaa kikamilifu.

Kaburu nasikia hana mawe siku hizi, hivyo hatoi hela pale SSC.

Tayari kocha kamtaja Kaburu kuwa ndiye anayempigiaga simu kumwambia wachezaji wa kuwapanga, kocha alitishia kuacha kazi au kumtukana kiongozi yeyote atakayefanya hivyo. Source: Bin Zubeiry(naiamini souce)

Mkuu;

Mimi Excuse ya kusema timu ya Simba haina pesa siielewi kabisa;

Na wala haiingii akilini.

Kuna mikataba mingi pale simba;


  1. Mkataba wa Kilimanjaro wenye zaidi ya Sh Bilioni moja kwa mwaka
  2. Mkataba wa Vodacom ambao ndio sponsors wa ligi ni mamilioni ya shillingi kwa kila klabu
  3. Mkataba wa Azam TV
  4. Viingilio Vya uwanjani
  5. Kodi ya Majeno ya Timu
  6. Uuzaji wa jezi za timu

Kiurahisi tu ukiangalia hayo...timu haiwezi kufulia;

Kwa mfano tufanye estimation za haraka;


  1. Mishahara ya wachezaji na benchi la ufundi Milioni 30 kwa mwezi,Kwa mwaka milioni 360
  2. Kambi ya Timu kwa mwaka milioni 500
  3. Usajili Milioni 200 kwa mwaka
  4. Mengine Milioni 100

Jumla hapo Bilioni 1.15

Hio Bilioni 1.15 inaweza kuwa covered na mkataba mmoja tu wa TBL Kilimanjaro.

Ndio maana nasema tatizo la simba sio pesa...pesa iko nyingi na inapatikana sana...isipokuwa kuna watu wanakula pale
 
Back
Top Bottom