Baada ya matokeo ya kura bungeni, UKAWA waendelea kuhaha

Baada ya matokeo ya kura bungeni, UKAWA waendelea kuhaha

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2013
Posts
5,536
Reaction score
2,266
unnamed-8-564x272.jpg


Wakati wakisusia Bunge Maalum la Katiba, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alikaririwa akisema, “Ukawa hatuwezi kuendelea kushiriki dhuluma dhidi ya wananchi kwa kupitisha Katiba ambayo ni kinyume cha matakwa yao.”

Madai hayo hayakuishia kwa Prof. Lipumba pekee. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe naye pia alikaririwa akisema,“Hoja ya msingi ni kwamba, vikao vinavyoendela Dodoma ni batili. Viko kinyume cha mchakato ulioasisiwa kwa misingi ya shirikishi na vinaakisi ubabe, dharau na kejeli za viongozi kwa Watanzania,”.

Aliendelea kusema, Vikao hivyo ni kama michezo ya kitoto ya kujitekenya na kucheka wenyewe, Mbowe alisema ikifanikiwa kupata Rasimu ya Katiba itakayopendekezwa kuwa Katiba na hata ikipitishwa kwa kura ya maoni kuwa katiba mpya, wao wataendelea kudai katiba bora.

Habari zaidi inapatikana hapa,
Kama hiyo haitoshi, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe (pichani), alitangaza maandamano na migomo isiyokoma nchi nzima kushinikiza kuvunjwa Bunge Maalumu la Katiba, kwa madai kwamba limekuwa likitafuna fedha za umma huku wakijua kwamba Katiba haiwezi kupatikana.

Habari zaidi iko hapa,
Mantiki ya hoja inatueleza kuwa, viongozi wakuu wa vyama vya CUF na CHADEMA au UKAWA kwa ujumla wao walishafuta yale yote yaliyokuwa au yanayoendelea kufanywa ndani ya Bunge Maalum na matokeo yake yote. Kwa lugha rahisi, UKAWA hawalitambui Bunge Maalum na maamuzi yake pamoja na kwamba sheria ya nchi inalitambua, hii ni pamoja na maamuzi yake linayofanya bila uwepo wa kikundi kinachojiita UKAWA.

Kinachoshangaza ni kuanza kuwasikia viongozi wa UKAWA wakilalamikia upigaji wa kura na matokeo ya kura za kupitisha Rasimu ya Katiba ndani ya bunge ambalo wao wameishasema hawalitambui. Kwa lugha nyingine, UKAWA wanalalamikia matokeo wakati hata chanzo cha matokeo hawakitambui.

Kwa habari zaidi unaweza kusoma hapa,
Kama UKAWA walidhani kuna umuhimu wa kupiga kura na kusimamia zoezi la upigaji kura, kwa nini walisusa na wakaondoka bungeni?.

Ni hawa hawa UKAWA walikuwa kila siku wanasema wabunge wote waliobaki bungeni ni wanaCCM wanaotaka kuendeleza muundo wa Serikali mbili lakini cha kushangaza ni hawa hawa UKAWA kwa sasa eti wanalalamika matokeo ya kura za wajumbe waliokuwa wanawaita wanaCCM na pia wasaliti. Are they serious?

Hoja za UKAWA nazifananisha na mwanamme anayepinga hamtambui mwanamke fulani halafu huyo mwanamke anapojifungua mtoto, anaanza kuomba wafanye DNA ili afahamu kama mtoto ni wake. Hiki ni kichekesho!

Kuhoji matokeo ya kura wakati hawawatambui hata wapiga kura(wabunge) achilia mbali taratibu zilizotumika kupiga kura nakupatikana matokeo ni kichekesho kwa watu wenye fikra pevu.

Kama wao wameishajitoa kwenye Mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya chini ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83, basi inabidi wakae kimya au waanze kudai Mchakato mwingine nje ya huu wa sasa kwa sababu wamedai wajumbe walioko bungeni wanachofanya kwa sasa ni kama wanajitekenya na kucheka wenyewe.

Tuliposema UKAWA hawafahamu wanachokisimamia baada ya kususia Bunge Maalum, kuna baadhi ya watu hawakutuelewa.

Huhitaji kuwa political analyst kuelewa kuwa UKAWA is all over the place. Kwa sasa hata ukiwauliza suala la maandamano na migomo limefikia wapi, huwezi hata kupata jibu.

Tumeanza kuona hata jina la UKAWA limeanza kufutika!.
 
Hebu tulia wewe acha umbulula,nenda kapige mswaki sisi wananchi ndio tutaamua
 
Kama ulikuwa karibu na mwizi, ukajitenga nae baada ya kuona kila ukimshauri harekebiki haina maana akiendelea kuiba ukiwa mbali nae basi utabariki wizi. Bado utapambana kuutokomeza wizi, wakati huo utakuwa umekwepa nawe kuitwa mwizi ungeonekana kuwa karibu nae wakati wote (ingekuwa kama ile kauli ya birds of same feathers fly together).

UKAWA, we chose not to fly together with the rest of criminals but that doesn't imply we should be in agreement with their proceedings.
For sure, I can realize logical thinking is a grave problem in this Taifa la Tanzania as it is evidenced in your post.
 
Kuanzia jana hakuna ukawa tena itabidi waunde umoja mwingine sijui utaitwa umoja wa vyama vya viongozi wasiojitambua?
 
Watu kama mbatia wanavichwa vikubwa halafu hawana akili kazi kweli.
 
mtu mjinga tu ama mchumia tumbo ndiye anaweza kusapoti rasimu ya CHENGE na SITTA basi ule mle ni ujinga mtupu
hata hili la UWAZI
UZALENDO
UWAJIBIKAJI kwako wewe si chochote?
 
Kama ulikuwa karibu na mwizi, ukajitenga nae baada ya kuona kila ukimshauri harekebiki haina maana akiendelea kuiba ukiwa mbali nae basi utabariki wizi. Bado utapambana kuutokomeza wizi, wakati huo utakuwa umekwepa nawe kuitwa mwizi ungeonekana kuwa karibu nae wakati wote (ingekuwa kama ile kauli ya birds of same feathers fly together).

UKAWA, we chose not to fly together with the rest of criminals but that doesn't imply we should be in agreement with their proceedings.
For sure, I can realize logical thinking is a grave problem in this Taifa la Tanzania as it is evidenced in your post.
Ndugu,
Nadhani hujaelewa mantiki ya hoja yangu!.

Jaribu kusoma tena ili uelewe vizuri!
 
mtu mjinga tu ama mchumia tumbo ndiye anaweza kusapoti rasimu ya CHENGE na SITTA basi ule mle ni ujinga mtupu
hata hili la UWAZI
UZALENDO
UWAJIBIKAJI kwako wewe si chochote?

Kaka unaongelea kuhusu UWAJIBIKAJI wakati tumeamua kuifilisi TANZANIA
 
Kuanzia jana hakuna ukawa tena itabidi waunde umoja mwingine sijui utaitwa umoja wa vyama vya viongozi wasiojitambua?
Kwa sasa CHADEMA imeanza kutofautishwa na UKAWA kwenye masuala ya Katiba.

Kwa sasa tovuti za CHADEMA zinaandika CHADEMA-UKAWA kama ilivyo hapa,
Wataalam wa maandishi watakuambia hii ni njia ya kuitoa CHADEMA ndani ya mwanvuli wa UKAWA.
 
Hoja hapo siyo nani amesema, hoja ni kura za maruhani zilikuwepo au hazikuwepo?
Mmechakachua, hamkuchakachua?
 
Ukweli utabaki rasimu hii imeoutishwa kwa vitisho na ghilba tupu ni aibu .
Tangia mwanzo ccm haikua na nia ya katiba.
Walitukana bungeni mnakumbuka kina asha.
Walopiga kura ya wazi wote karibu wameikataa.
Walopiga kura ya siri mnajua wenyewe
 
Hoja hapo siyo nani amesema, hoja ni kura za maruhani zilikuwepo au hazikuwepo?
Mmechakachua, hamkuchakachua?
UKAWA walipotoka bungeni wakaanza kuwaita majina mbali mbali waliobaki bungeni.

Tuliwasikia wakisema waliobaki bungeni ni wasaliti na pia wanaCCM, kama hiyo ndiyo ilikuwa hoja yao, kwa hiyo walitegemea nini kutoka kwa watu waliokuwa wanawaita wasaliti na wanaCCM.

Kwa hiyo UKAWA walitaka wasaliti wapige kura za hapana au wasaliti hao hao wazilinde kura za wasaliti.

Hiki ni kichekesho!

Kama UKAWA walifahamu kuna umuhimu wa kulinda kura ili zisichakachuliwe, kwa nini walisusia bunge.

Kwa nini walishindwa kurudi na kupiga kura kama alivyofanya Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.
 
Eti MwanaDiwani , huku mtaani watu wanasema kuna kura kama 7 hivi waliozipiga hawajulikani, unasemaje kuhusu hili maana limewatia umma wasiwasi mkubwa
 
Last edited by a moderator:
Ukweli utabaki rasimu hii imeoutishwa kwa vitisho na ghilba tupu ni aibu .
Tangia mwanzo ccm haikua na nia ya katiba.
Walitukana bungeni mnakumbuka kina asha.
Walopiga kura ya wazi wote karibu wameikataa.
Walopiga kura ya siri mnajua wenyewe
Ndugu,
Nadhani hukupata kuangalia zoezi la upigaji wa kura bungeni.

Jaribu kutafuta hata video ili uone na kuelewa vizuri idadi ya wajumbe waliopiga kura ya wazi ili ujidhihirishe kama wengi waliikataa Katiba inayopendekezwa.
 
Eti MwanaDiwani , huku mtaani watu wanasema kuna kura kama 7 hivi waliozipiga hawajulikani, unasemaje kuhusu hili maana limewatia umma wasiwasi mkubwa
Ndugu,
Mimi sikuwa msimamizi wa kura na kwa maana hiyo, sifahamu lolote zaidi ya official results kama zilivyotolewa bungeni.

Ingefaa uwaulize zaidi hao wanaotoa hayo madai labda wana majibu yatakayo waondoa wasiwasi.
 
Wakati wakisusia Bunge Maalum la Katiba, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alikaririwa akisema, “Ukawa hatuwezi kuendelea kushiriki dhuluma dhidi ya wananchi kwa kupitisha Katiba ambayo ni kinyume cha matakwa yao.”

Madai hayo hayakuishia kwa Prof. Lipumba pekee. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe naye pia alikaririwa akisema,“Hoja ya msingi ni kwamba, vikao vinavyoendela Dodoma ni batili. Viko kinyume cha mchakato ulioasisiwa kwa misingi ya shirikishi na vinaakisi ubabe, dharau na kejeli za viongozi kwa Watanzania,”.

Aliendelea kusema, Vikao hivyo ni kama michezo ya kitoto ya kujitekenya na kucheka wenyewe, Mbowe alisema ikifanikiwa kupata Rasimu ya Katiba itakayopendekezwa kuwa Katiba na hata ikipitishwa kwa kura ya maoni kuwa katiba mpya, wao wataendelea kudai katiba bora.

Habari zaidi inapatikana hapa,

Kama hiyo haitoshi, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe (pichani), alitangaza maandamano na migomo isiyokoma nchi nzima kushinikiza kuvunjwa Bunge Maalumu la Katiba, kwa madai kwamba limekuwa likitafuna fedha za umma huku wakijua kwamba Katiba haiwezi kupatikana.

Habari zaidi iko hapa,

Mantiki ya hoja inatueleza kuwa, viongozi wakuu wa vyama vya CUF na CHADEMA au UKAWA kwa ujumla wao walishafuta yale yote yaliyokuwa au yanayoendelea kufanywa ndani ya Bunge Maalum na matokeo yake yote. Kwa lugha rahisi, UKAWA hawalitambui Bunge Maalum na maamuzi yake pamoja na kwamba sheria ya nchi inalitambua, hii ni pamoja na maamuzi yake linayofanya bila uwepo wa kikundi kinachojiita UKAWA.

Kinachoshangaza ni kuanza kuwasikia viongozi wa UKAWA wakilalamikia upigaji wa kura na matokeo ya kura za kupitisha Rasimu ya Katiba ndani ya bunge ambalo wao wameishasema hawalitambui. Kwa lugha nyingine, UKAWA wanalalamikia matokeo wakati hata chanzo cha matokeo hawakitambui.

Kwa habari zaidi unaweza kusoma hapa,

Kama UKAWA walidhani kuna umuhimu wa kupiga kura na kusimamia zoezi la upigaji kura, kwa nini walisusa na wakaondoka bungeni?.

Ni hawa hawa UKAWA walikuwa kila siku wanasema wabunge wote waliobaki bungeni ni wanaCCM wanaotaka kuendeleza muundo wa Serikali mbili lakini cha kushangaza ni hawa hawa UKAWA kwa sasa eti wanalalamika matokeo ya kura za wajumbe waliokuwa wanawaita wanaCCM na pia wasaliti. Are they serious?

Hoja za UKAWA nazifananisha na mwanamme anayepinga hamtambui mwanamke fulani halafu huyo mwanamke anapojifungua mtoto, anaanza kuomba wafanye DNA ili afahamu kama mtoto ni wake. Hiki ni kichekesho!

Kuhoji matokeo ya kura wakati hawawatambui hata wapiga kura(wabunge) achilia mbali taratibu zilizotumika kupiga kura nakupatikana matokeo ni kichekesho kwa watu wenye fikra pevu.

Kama wao wameishajitoa kwenye Mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya chini ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83, basi inabidi wakae kimya au waanze kudai Mchakato mwingine nje ya huu wa sasa kwa sababu wamedai wajumbe walioko bungeni wanachofanya kwa sasa ni kama wanajitekenya na kucheka wenyewe.

Tuliposema UKAWA hawafahamu wanachokisimamia baada ya kususia Bunge Maalum, kuna baadhi ya watu hawakutuelewa.

Huhitaji kuwa political analyst kuelewa kuwa UKAWA is all over the place. Kwa sasa hata ukiwauliza suala la maandamano na migomo limefikia wapi, huwezi hata kupata jibu.

Tumeanza kuona hata jina la UKAWA limeanza kufutika!.
MwanaDiwani,
Bado nakupongeza na kukutakia sherehe njema.Mmenifanikisha mlichodhamiria na mna haki ya kusheherekea,kukejeli na kila aina ya style ya kusherehekea mnayotaka.
Naamini vijembe,mipasho na kejeli ni hapo next week.
Hongereeeni sana!!!!!!!!!!!!!!!
 
Ndugu,
Mimi sikuwa msimamizi wa kura na kwa maana hiyo, sifahamu lolote zaidi ya official results kama zilivyotolewa bungeni.

Ingefaa uwaulize zaidi hao wanaotoa hayo madai labda wana majibu yatakayo waondoa wasiwasi.

Mkuu, Mimi binafsi najua we ni kada wa chama pendwa chama cha Mapinduzi, watu wanaulizana hili na inaonekana ni kweli hizo kura hazikupigwa bali tu ziliongezwa...

Je hichi kitu cha kujaziliza kura ambazo hazikutosha kimefanyika kwa faida ya nani, kwann tusingeacha demokrasia ikachukua fursa yake
 
MwanaDiwani,
Bado nakupongeza na kukutakia sherehe njema.Mmenifanikisha mlichodhamiria na mna haki ya kusheherekea,kukejeli na kila aina ya style ya kusherehekea mnayotaka.
Naamini vijembe,mipasho na kejeli ni hapo next week.
Hongereeeni sana!!!!!!!!!!!!!!!
Ndugu MIGNON
Ninaendelea vile vile kuzikubali pongezi zako.

Safari ya kupata katiba mpya bado ni ndefu na yenye vikwazo vingi sana.

Hatua inayofuata ambayo niya mwisho ni ngumu sana!

Mawimbi ya bahari ya kisiasa ndani ya Bunge Maalum yaliwatosa UKAWA nje ya bunge lakini cha kushangaza eti kwa sasa wanaomba msaada kwa waliobaki bungeni wawasaidie kuwaokoa katika safari ya mchakato wa Katiba mpya.
 
Back
Top Bottom