Uchaguzi 2020 Baada ya matokeo ya kura za maoni, Je kuna uwezekano wa CCM kupata mpasuko?

Uchaguzi 2020 Baada ya matokeo ya kura za maoni, Je kuna uwezekano wa CCM kupata mpasuko?

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Nauliza hili swali kama raia wa kawaida ambae nimepigwa butwaa na nini kimetokea kwenye matokeo ya kura za maoni za chama tawala nchini Tanzania.

Kila mtu haamimi nini kilitokea Kawe, Kigamboni na Kyela. Yaani jimbo la Kawe Gwajima, Paschal Mayalla, kipi na vigogo kibao waligaragazwa na Kijana asiyekuwa na jina. Kigamboni kila mtu amejionea kwa macho.

Huko Kyela, Dkt. Harrison na uwezo wake wote wa kuongea kwa kujiamini nae amekula mzinga! Na hawa ambao walitoka upinzani na kujiunga na CCM nao wamelamba mchanga!

Lakini tuachane na hayo kuna hii minog'ono inayoibuka kuwa huenda CCM ikagawanyika kama mwaka 2010. Maana kuwakata walioshika namba moja bila sababu za msingi kutaleta mpasuko mkubwa. Mfano ni mwaka 2010 David Mwakalebela alishinda kura za maoni Iringa mjini,jina likakatwa na Monica akapewa nafasi,kilichofuata Chadema ikachukua jimbo.

Sasa hata mwaka huu huenda yakajirudia yaleyale ya 2010. Maana kuwakata walioshinda kutaleta mpasuko na hasira kwa waliompitisha aliyekatwa. Labda tu advantage kwa CCM ni kuwa kwa sasa tofauti na 2010 upinzani upo hoi maututi.
 
  • Thanks
Reactions: rr4
Upinzani ungekuwa hoi mngetumia Polisi kuudhibiti?

Mnafiki tu wawe!
Kama upo hai utaonekana tu wala usiwe na hasira. Polisi wanaudhibiti vipi? CCM inapasuka mnashinda maana watalazisha kupitisha walioshindwa.
 
Endelea kujidanganya kuwa upunzani uko hoi, jiulize ni kwa nn upinzani uliodhaifu unafanyiwa figisu kila kukicha? Wee andika tu kusha kachukue b7 zako maisha yasonge
 
Endelea kujidanganya kuwa upunzani uko hoi..jiulize ni kwa nn upinzani uliodhaifu unafanyiwa figisu kila kukicha?? wee andika tu kusha kachukue b7 zako maisha yasonge
Buku saba unalipa wewe? Huoni CCM wana hali ngumu kuchuja. Acha upuuzi, kila kitu buku7.
 
Jana hili swala nililizungumzia nilileta uzi hapa hap unaosema kama wako mods wakaunganisha uzi na mwingine
 
Back
Top Bottom