Pre GE2025 Baada ya Mbowe kutetea uenyekiti wake, masikini Tundu Lissu, kwishney! Je, atabaki ama atatimka? Lissu Cool down, usiitishe Press kumjibu Mbowe!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kama hizi ndio hoja zako, basi sasa nimeamini umezeeka.
 
Pascal hjatimiza wajibu wako professionally, hujatoa sababu gani Mbowe atashinda, na lisu kushindwa......

all in all. Lisu anaropoka sana....HAFAI
 
Pascal hjatimiza wajibu wako professionally, hujatoa sababu gani Mbowe atashinda, na lisu kushindwa......

all in all. Lisu anaropoka sana....HAFAI
Namba hazidanganyi, Lisu anaungwa mkono na wanaharakati wenzake wa mitandaoni, wakati Mbowe anaungwa mkono na wanasiasa wenzake na wajumbe wengi wa mkutano mkuu ( wapiga kura).

Hesabu hizi hazihitaji kufaulu somo la Mathematics kujuwa kwamba Mbowe tsyari ameshamaliza uchaguzi tena Lisu atapigwa kwa kura nyingi tu, wrong timing and wrong strategy for team Lisu.
 
Kwani alitaka kupita bila kupingwa au alisema anagombea, si anajua watakuwepo wengine wa kupigiwa kura? Kwa nini iwe kwishney kwa kuongezeka wagombea learned brother? Na si ndio demokrasia yenyewe? I am confused😱
Huyu mleta mada naye kichwa andazi tu. Bumunda la ccm Lazima kuna kitu nyuma ya pazia kwanini wanaogopa lissu kugombea na kushinda..
 
Ili chama kiendelee kuwa na mvuto inatakiwa mbowe apumzike. Tofauti na hapo CHADEMA itaridi hatua mia mbili nyuma.

Ushauri wangu ni huu endapo mbowe atashinda basi lisu apumzike ajikalie kimya amuachie mbowe chama na huo ndio utakuwa mwisho wa chadema.
 
Huyu mleta mada naye kichwa andazi tu. Bumunda la ccm Lazima kuna kitu nyuma ya pazia kwanini wanaogopa lissu kugombea na kushinda..
Wewe ndio Bumunda namba moja, kwa nini wanaharakati wanamuogopa Mbowe kugombea?

Si ana haki ya kugombea na kikatiba? Nendeni sasa mkamuamgushe kwenye uchaguzi ili mtuaminishe amechokwa, ila akiwagaragaza mtuloe msianze kelele.
 
Wasira ndio mtabiro wa kwanza wa mwisho wa Chadema matokeo yake tunauona mwisho wake na Chadema ipo na itaendelea kuwepo.
 
Lissu can't be kwishney and shall never be kwishney. Spare your words coz the future is unknown but we just put a plan. Not everything planned can come true. Najua wengi tunaishi kwa upepo. Lakini mambo hubadilika na unaweza ukabadili sentence za kuongea hapa. It's not over until it's over. Kesho imeficha Siri kubwa mno.
 
Mie naona hao drama 🤣🤣🤣🤣tu wameweka wapate attention ya wananchi then.............. Walete walichopanga iwe mshituko tena ati wanatoa 🤣🤣🤣🤣

Iweje Mwenyekiti (na wenye Chama) wasimsishushe cheo Makamu wake hadi leo au kufanya lolote aache kupiga mdomo wake tangu aanze.

Sijui katiba yao kutoana kukoje ila Mkiti angesukuma iwe hivyo tanguuuuuu kwa njia yoyote.

CHADRAMA

Nawaonea huruma mnaojipiga wa navyotaka kuwa jadili asubuhi hadi asubuhi.. hadi mmoja humu jana eti maisha sijui nini kisa chama hiki..

Mie 🍿🍿🍿
 
Sio kwamba tunataka TAL awe mwenyekiti.

Tunataka mwana chama yeyote mwenye sifa za kugombea agombee then wananchi waamue.

Na hiyo ndo democrasia walio kua wanaihubiri.
 
Sote tunauona uhuni huu, ila ukimya umekuwa ndiyo chaguo la wengi. Hata wanachama wenyewe wa Chadema wako kimya. Ukimya mzito, kama pazia jeusi lililoshushwa katikati ya jukwaa lenye kelele.

Hayupo anayeongea. Hakuna hata anayethubutu kunong’ona. Ni kama vile walikubaliana kimyakimya kuwa hakuna lolote la kusema. Mtu mmoja, Pascal Mayalla akiwa nje ya Chadema, anaweza kufanya nini?

Unajua kimya cha huko Chadema kimetokana na nini? Umasikini. Adui wa kwanza wa Tanzania ni umasikini.
Umasikini huu si wa kawaida. Ni mwizi wa matumaini, mkandamizaji wa ndoto, na silaha mikononi mwa wenye nacho.

Wenye nazo hawahitaji silaha nyingine – wanatumia umasikini wa watoto wa masikini kuwajenga wao wenyewe. Wanatoa ahadi nzuri kwa masikini, ahadi ambazo hazitafika popote. Wanajenga ngome zao juu ya jasho na machozi ya wasio nacho.

Wanaomuunga mkono Tundu Lissu wanaongea kwa sauti ya kimya. Ukimya wao unazua maswali zaidi ya majibu. Ni hofu? Ni unyonge? Au ni hesabu za kisiasa za watu waliokwama njia panda?

Lakini, kwenye upande mwingine, wanaomuunga mkono Mbowe hawana muda wa ukimya. Wanakesha wakihubiri sifa zake, wakitengeneza headline za magazeti na mitandao ya habari. Mikocheni imegeuka kiwanda cha propaganda. Na hapa ndipo mchezo wa wenye nguvu unafikia kilele chake.

Unajiuliza, hii ni demokrasia au mapambano ya kiitikadi yaliyojaa hila? Labda suluhisho ni moja tu, kuongeza matajiri kwenye siasa.

Wenye nazo wakishindana wao kwa wao, labda masikini wataachwa wapumue. Lakini kwa sasa, matumaini ya wanyonge yamekwama kwenye mifumo inayowalalia.

Swali linabaki, Tanzania itaamka lini? Tutapambana lini na adui huyu ambaye kila siku anazidi kutufanya watumwa wa wenye nguvu? Labda ni ndoto tu – ndoto inayongoja shujaa wa kuifanikisha.

Swali ni; shujaa huyo ni nani? Na atafika lini?

Ova
 
This is deep, umeandika kwa machungu na uzalendo uliotopea.
Nimeumia, kama nchi tumepotea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…