Jana aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe alitangaza rasmi kujiunga na chama cha ACT Wazalendo
Mchakato wa Membe ulianza zaidi ya miezi minne iliyopita huku serikali ikifuatilia kwa karibu
Baada ya hivi karibuni kujiridhisha kwamba atajiunga na kuna uwezekano vyama pinzani vikamsimamisha kuwa mgombea wao,serikali kupitia ofisi ya msajili ikaibuka na kituko cha mwaka kwa kuwaandikia ACT barua ya kuwajulisha nia ya kuwaadhibu
Miongoni mwa sababu zilizotajwa kwamba ni za kutoa adhabu ni pamoja na chama hicho kuwahimiza wananchi kusimamia haki yao,kuitaka tume ya uchaguzi na vyombo vya dola kutenda haki ili uchaguzi uishe kwa amani na salama
Tayari Mutungi na timu yake kwa sasa wako katika hatua ya mwisho ya kutangaza adhabu hiyo kwa lengo la kuhakikisha CCM haipati upinzani unaostahili