Watu wanahoji timing na kundi lilikuwa limemzunguka kaka?ndo mana nimetoa hili kama angalizo soma text vizuri?Mwanajeshi anapokuwa vitani kuna tofauti ya Uhuru ambao anakuwa nao tofauti na kipindi anapokuwa Uraiani?Unafanya nini Bar na kundi la wafanyabiashara na wanachama wa CCM meza moja mda huu wa kazi?na mimi angalizo langu ni kwa CHADEMA NA CCM kwa pamoja..Nimezungumzia watu wawili mwenyekiti wa CCM na wa MGOMBEA..Namwamini sana Lema...ila ajirekebishe
Tatizo chadema mna mawazo mengi ya kilofa...
Katika hali isiyotarajiwa na inayotia shaka Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chadema Ndugu Godbless Lema amekutwa Bar akiwa amekaa na viongozi wa andamizi wa Chama Cha Mapinduzi katika Bar ya Family Pub mjini Arusha kuanzia saa tatu usiku na kuendelea huku wakiwa wenye furaha.Ikiwa haiujulikani ni kwa vipi jambo hili limetokea wakati Mgombea wa CCM Jakaya Kikwete akiwa mjini Arusha kwa ziara rasmi ya kampeni.
- Maswali ya kujiuliza ni kwa vipi mwenyekiti wa CCM Ndugu Jublate Kileo awepo Bar na Mgombea wa Chadema wakati ambao mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho akiwa bado mjini hapa?ina maana hawana mazungumzo ya mikakati ya kulitwaa jimbo au ndo mkakati ni kumchakachua GODLESS LEMA
- Je kwanini wawepo mda huo mahali hapo au ndo kuthibitisha kuwa Jublate hamuungi mkono Dr Batilda Buriani kwani alikuwa kundi la Felix Mrema?
- Ndo kusema sasa CCM wanataka kumchakachua Godless Lema arudishe kadi na kujitoa kugombea Ubunge hapa Arusha mjini?ni muda tu utakaosema.Nategemea sana wahusika wote watatoa ufafanuzi wa kina au kama walikuwa wana mazungumzo ya kawaida nani ajuaye
starehe haina siasa...ndio maana Jakaya ...pamoja na upinzani na mbowe majukwaani ....walikuwa wakikutana pamoja kwenye starehe.....na huko nyuma ...Jakaya alikuwa ni mmoja wa wahudhuriaji wazuri kwenye Club ya billicanas.....
Ni muhimu ikaeleweka kuwa siasa haiwezi kutuzuia kukaa baa pamoja naa kuzungushiana raundi za bia kama ilivyo utamaduni wetu watanzanania .....mkifuatilia mtagundua kuwa kuna wagombea wengi tu wa CCM wanakunywa na wapinzani ie CHADEMA....na hata wale wavutaji wa sigara wanaendelea kugongeana ....na wale wakware wanaendelea kutongozana ...maisha yanaendelea.......
Sioni ajabu kwenye hili.....ningeshangaa kama walikuwa wananywea pombe chumbani.....maana ingemaanisha walikuwa wana ongea siri.....lakini BAR is a public place....na watu wa Arusha kukesha bar ni kawaida yao.....
Mwenye macho haambiwi tazama kaka...ni bora kupata mbunge makini tuWakuu kama kuna mwanjamvi aliwahi kupitia andiko langu "Ubunge Arusha ni kati ya Batilda,Lyimo na Lema" hawezi kushangaa hata kidogo Lema anajulikana ni mwanasiasa mfanyabiashara bahati mbaya CCM wanajua bei yake siku nyingi.Lema aligombea ubunge TLP mwaka 2005 akashinda lakini CCM wakamuonga kitu kidogo akaondoa kesi mahakamani.Lema alimwondoa aliyekuwa diwani wa Sombetini Bwana Mawazo na kumpeleka CCM.Hakuishia hapo alipanda jukwaani kumnadi Bwana Mawazo hadi akashinda udiwani wa Sombeti kwa tiketi ya CCM !,wanaoshanga Godbless Lema watakuwa ni wageni na pengine hawajui jamaa yuko kwenye siasa kimaslahi zaidi.
Mkuu Bria
Namfahamu Godbless Lema, mimi nimesoma na David Kileo mtoto wa huyo mwenyekiti Jubilate Kileo ambaye ni mjomba wa Godbless.Nimetembelea nyumbani kwa huyo Mzee Kileo kule Kaloleni,ninachokifahamu mimi Mwenyekiti yuko upande wa Felix Mrema.Fikra zangu zinanituma kuwa wangependa kuona mgombea wa CCM ashindwe kushikisha adabu hilo kundi lingine.Nakubaliana kabisa na mawazo ya Keil uhuru wa kujumuika tuuheshimu.
Godbless Lema ajiangalie manake sisi wananchi wa Arusha ( Chadema followers) hasira yetu itakuwa mbaya sana kwake na atajuta maisha yake yote kama atataka tamaa yake ituondelee uwakilishi kwenye uchaguzi asome alama za nyakati
Mkuu Bria
Namfahamu Godbless Lema, mimi nimesoma na David Kileo mtoto wa huyo mwenyekiti Jubilate Kileo ambaye ni mjomba wa Godbless.Nimetembelea nyumbani kwa huyo Mzee Kileo kule Kaloleni,ninachokifahamu mimi Mwenyekiti yuko upande wa Felix Mrema.Fikra zangu zinanituma kuwa wangependa kuona mgombea wa CCM ashindwe kushikisha adabu hilo kundi lingine.Nakubaliana kabisa na mawazo ya Keil uhuru wa kujumuika tuuheshimu.
Uhuru anao mpaka mwisho kaka hapa ndipo swala la kuwa "Public figure"pata picha kipindi hiki cha Uchaguzi Batilda aonekane na viongozi wa CHADEMA Bar Usiku unadhani jamii itamuelewa vipi?Ukihitaji kuwa kiongozi bora ni lazima ukubali kukosolewa na kutokaa katika mazingira hatarishi.Kikubwa nia ni kuonyana wakati ambao wenzetu siasa wao si urafiki bali ni kulinda maslahi ya watu WACHACHE..Nikukumbushe hawakukaaa kama ndugu bali viongozi wa CCM walifika na magari yao na bendera..zipo mbinu nyingi za kufanya lobbying kaka..Iweje uongozi wa juu wa CHAMA UMTELEKEZE MGOMBEA URAIS NA KUKAA NA MGOMBEA WA CHADEMA..hapa ndo swali la msingi?
au ndo kusema kuna makundi?na kama kuna makundi si ndo ulikuwa mdau wa kuyatatua?NGASTUKA HAPA MACHALE KUNDESA
Ni kweli kambi ya Felix wengi wao wanamuunga mkono Lema...Nitamuomba Lema alitolee ufafanunuzi hapo kwenye rangi nyekundu kwani inaonekana anakubalika sana hapa Arusha huo ndiyo ukweli na utaona tarehe 31-10-2010...kwa hiyo naamini hata wewe utakuwa na imani nae pale atakapo tolea ufafanuzi..
Wakuu kama kuna mwanjamvi aliwahi kupitia andiko langu "Ubunge Arusha ni kati ya Batilda,Lyimo na Lema" hawezi kushangaa hata kidogo Lema anajulikana ni mwanasiasa mfanyabiashara bahati mbaya CCM wanajua bei yake siku nyingi.Lema aligombea ubunge TLP mwaka 2005 akashinda lakini CCM wakamuonga kitu kidogo akaondoa kesi mahakamani.Lema alimwondoa aliyekuwa diwani wa Sombetini Bwana Mawazo na kumpeleka CCM.Hakuishia hapo alipanda jukwaani kumnadi Bwana Mawazo hadi akashinda udiwani wa Sombeti kwa tiketi ya CCM !,wanaoshanga Godbless Lema watakuwa ni wageni na pengine hawajui jamaa yuko kwenye siasa kimaslahi zaidi.
Ni kweli kambi ya Felix wengi wao wanamuunga mkono Lema...Nitamuomba Lema alitolee ufafanunuzi hapo kwenye rangi nyekundu kwani inaonekana anakubalika sana hapa Arusha huo ndiyo ukweli na utaona tarehe 31-10-2010...kwa hiyo naamini hata wewe utakuwa na imani nae pale atakapo tolea ufafanuzi..
heshima kwako phillemon mikael,
mkuu nadhani unashindwa kujua kwamba godbless lema hakuwa chagua la chadema wilaya ya arusha kwasababu wanamjua alivyokigeugeu na tapeli la kisiasa.lema kapachikwa na uongozi wa chadema taifa,demokrasia haikufuatwa hata kidogo.
Godbless lema na mawazo walijitoa tlp kwa ahadi wataachiwa nafasi za kugombea ubunge na udiwani respectively.nafasi ya udiwani iliwezekana kwasababu bwana mawazo alikuwaakishikilia nafasi hiyo lakini nafasi ya ubunge ikawa ngumu ndiyo maana godbless akatimkia chadema.inakupasa kujua godbless ana mafungamano makubwa na ccm nadhani kinachosubiriwa ni fungu kubwa litolewe jamaa amwage manyanga chini.najua watu hawapendi kusikia hizi habari hapa jamvini lakini ukweli ni huo huwezi kumwamini lema ukiitazama historia yake kwenye siasa za upinzani.
heshima kwako bria,
unashindwa kujua jambo moja muhimu hapa jamvini ukileta story mbaya kuhusu chama fulani lazima itapingwa sana lakini ingekuwa story ya cuf,ccm,tlp au nccr mageuzi nakwambia itachangamkiwa mpaka utashangaa.ukweli ni kwamba lema siku ya j4 alikuwa miami beach bar ya mjomba wake mzee j kileo na viongozi wa ccm mkoa wa arusha kwaajili ya maandalizi ya kurejesha kadi ya chadema kwenye mkutano wa ccm jana kilichoshindikana ni fuba na cheo alichoahidiwa hakikumridhisha.ngoma ilikuwa iwe godbless na nakaaya wajiunga na ccm, bado viongozi wa ccm wanashughulika mawindo yao muda si mrefu mtasikia na kushangaa jinsi ccm wanavyoendesha siasa za maji taka.kuwa mpinzani kunataka moyo wa ujasiri mkubwa bwana lema si miongoni mwa wapinzania wenye mioyo ya simba.
Nimekusoma Mkuu, ila usisahau Elerai pia anakubalika sana...Kiboko ya mafisadi ndaya ya A-Town kesho....Saa tano mbauda....
Heshima kwako Crashwise,
Mkuu soma MwanaHalisi kasema alimkampenia Mawazo kwasababu ni rafiki yake !!!!!!!!!!!!!!!!!.siwezi kumpatia kura mtu ambaye najua hawakilishi maslahi yangu na jamii kwa ujumla eti kwasababu ni mpinzani ?.Niliwahi kuingia kwenye mtego wa kumshabikia mtu kwasababu ni chama fulani.Nadhani unawakumbuka kina Masumbuko Lamwai,Nswanzigwako,Makongoro Nyerere,na wengine wengi.Godbless Lema anatumia CHADEMA kufanikisha malengo yake kitu ambacho tumekishuhudia kikifanyika enzi za NCCR Mageuzi.Godbless Lema anatamba mjini hasa maeneo ya Kijenge na kaloleni mwambie aende Sombeti au sokoni1 kwenye wapiga kura wengi hawezi hata siku moja hakuna mwenye habari nae kwasababu wanakumbuka alivyomnadi Mawazo kwenye kampeni za udiwani.