Uchaguzi 2020 Baada ya Nyalandu kuongoza kura za awali kwa 100%, Je ni dalili za Nyalandu kupeperusha bendera ya CHADEMA? Je, Lissu atarudi kweli J3?


Haya ndio matamanio yako.
 
Kwani kinachoamua nani agombee urais ni wapiga kura (wajumbe) au wanachama?

Hizi shobo ndizo zitakazowaponza.

Vyovyote iwavyo, sisi wapiga kura wengi wa upinzani tunamtaka Lissu, hiyo ni bila kujali hao wajumbe watampitisha nani.
 
Mlishindwa kumtoa roho na sasa mmesikia anarudi sasa mmeanza kujijambia kwa uoga wa kuumbuliwa.

Mmawia wewe hufai kwa ushabiki maandazi wako, Lissu lazima alitakari kwa hili, CCM wanamtaka sana , ndio maana shuguli zake za kesi pale Kisutu wameahirisha kumpa nafasi ya kugombea kupeperusha bendera ya CHADEMA. Swali tangu lini CCM wakawa watu wema kwa upinzani. Panya hukarimiwa nyama lakini kwenye mtego ili umnase..
 
Itakuwa kituko kama watampitisha Nyalandu kuwa mgombea!
Maana watu watajiuliza wameshindwaje kukubali kuungana kutengeza UKAWA 20 ili mgombea awe Membe ambayo ingeweza kuimarisha afya ya upinzani kwa mapana zaidi kuliko huyo Nyalandu?

Kweli itashangaza sana!
 

Punguza moto, wanacham na wapenzi unatuita kondoo, inakuwa kama hujui mikwala dume vyombo vya dola vinaipiga wakati wowote Mkulu akiwa anapelekwa Jehanam? Kuzidiwa mikwala dume.
 
Sasa kama munajua ni hivyo kwa nini munapoteza mda na rasilimali pesa.
 
Mkuu ni ngumu kukuweka kwenye kundi la watu wenye akili ngumu kwa sababu hoja zako nyingi zina mantiki, zinasomeka na kujisimamia ipasavyo. Tatizo lako ni ama unafanya makusudi ya kutoutambua na kuukubali baadhi ya ukweli au mapenzi yako ya kupitiliza kwa chama unachoamini yameshakuathiri na kwa hivyo siyo rahisi ukafanya analysis nyingine yoyote huru nje ya imani yako ya asili. Eti unajipofua kwamba Lowasa hakuleta kura yoyote mpy CDM, eti umeendelea kung'ang'ana, hajafungua matawi, nk., nk. Kumbuka wakati fulani TL akitetea kwanini walimfyekelea mbali Dr. Slaa na kumweka Lowasa. Alichoeleza ni kwa sababu walifuata ushauri wa watafiti toka nje ya nchi waliokuwa wamepewa kazi hiyo na CDM ili kushauri ni mgombea yupi angeweza kupata kura nyingi kwa kutumia influence yake pekee. Lowasa alikuwa nambari 1 kwa maelezo ya TL ambaye wewe ndo unamwona A -Z. Watu wanapokuambia subiria matokeo ya mwaka huu yatakuonesha kama cdm ilikuwa na watu ama Lowasa ndo alikuwa na watu usilete utetezi mara hoooo, Magufuli hana demokrasia, hooo wala rushwa watatangazwa. Kama unayajua yote hayo kauli za mwisho wa Magufuli ni baada ya uchaguzi zinatoka wapi? Kwanini tumchoshe TL kuingia kwenye uchaguzi ambao tunajua cdm kupata angalau jimbo moja ni kwa kudra za Mwenyezi Mungu pekee?
 

Nashukuru kwa kiwango cha waledi wa kujibu hoja, keep it up. uko vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…