jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 36,197
- 29,717
Baada ya Oktoba 25 wanachama wa chadema asili wanajipanga kukirudisha chama chao kutoka mikono ya familia ya Mtei na kukifanya kuwa taasisi ya umma kwa kuwa inatumia ruzuku za serikali.
Ni wazi Mbowe anaonekana kujutia uamuzi wake wa kubadili gear angani,uamuzi ambao umeigharimu chadema kwa kumpoteza shujaa wa ujenzi wa upinzani wa kweli Tanzania ndugu Dr Slaa.
Ni ukweli usiojificha kwa wanachama wa chadema asili wametaharuki na kushangaa chama chao kutekwa na wahuni au makapi yaliyoisumbua ccm hadi Kikatio cha Mangula kilipotumika.
Wanachama wa chadema asilia wamelazimika kuirudisha ccm madarakani kwa kosa kubwa la kiitifaki lililoamuliwa na familia moja tu ndani ya chama.
Wanachama wa chadema asilia ni wazi wanatafakari hasa baada ya ushindi wa kishindo wa Magufuli ni kwa vipi wanaweza kukinusuru chama chao kisiporomoke kama NCCR,CUF na TLP.
Wanachadema asilia wanatafuta mwenyekiti kwani haiwezekani Wangwe,Arfi,Zitto,Kitila,Mwigamba na Slaa wakawa na matatizo...tatizo ni mwenyekiti na akiendelea kuchekewa chama kitafutika kwenye ramani ya kisiasa.
Wanachadema asilia wanatambua wanayo haki ya kisheria ya kukiondoa chama mikononi mwa familia ya mtei.
Wanachadema asilia wanataka kuona mfumo wa uteuzi wa wagombea ndani ya chama unakuwa wazi na kufuata taratibu za chama.
Wanachadema asilia wanataka kuona mgao wa ruzuku unakuwa fairly distributed na sio kuwafikia baadhi ya wanaojidai makamanda kutoka kaskazini.
Ni katibu aliyeondolewa na Mbowe ndio aliyetuelekeza kwenda mitaani na vijijini ili kukikuza chama na aliahidi kutupima kwa hilo.leo hii Mbowe amemfanya katibu ni mvivu.
Wanachadema asilia hawajapewa fursa rasmi ya kumpitisha lowassa kuwa mgombea urais kupitia chadema.hili limefanyika kiujanjaujanja kwa kuwa Mwenyekiti anajua wanachama wangelipinga kwani mgombea huyu hana sifa za kikamanda wala hajui misingi ya kuwa kamanda wa wananchi wanyonge.
Wanachadema asilia hawakupewa fursa ya kuamua au kujua jinsi gani mchakato wa kuachiana majimbo utakavyokuwa.sana sana mchakato ulisikika kwenye vyombo vya habari tu.
Wanachadema asilia walijitoa kwa hali,mali na uhai wao kwa kutarajia Tanzania mpya inazaliwa ikiwa haina ufisadi,uongo,udini,ukanda,ufamilia,ukabaila na usaliti badala yake Mwenyekiti na timu ya wachache imetuletea mamluki wanaokichafua chama na kukiacha kikiwa vipande vipande.
Kwa heshima ya Wangwe,Zitto,Slaa,Arfi,Kitila,Kafulila na wengine ni lazima Mwenyekiti uondolewe kwani wewe ndio tatizo.Mwenyekiti umebebwa sana na think tanks ndani ya Chadema na malipo yao yamekuwa ni kuwafukuza tu.
Mwisho wa Mbowe kuwa mwenyekiti Chadema ni oktoba 25.
SENT AS RECEIVED!
Ni wazi Mbowe anaonekana kujutia uamuzi wake wa kubadili gear angani,uamuzi ambao umeigharimu chadema kwa kumpoteza shujaa wa ujenzi wa upinzani wa kweli Tanzania ndugu Dr Slaa.
Ni ukweli usiojificha kwa wanachama wa chadema asili wametaharuki na kushangaa chama chao kutekwa na wahuni au makapi yaliyoisumbua ccm hadi Kikatio cha Mangula kilipotumika.
Wanachama wa chadema asilia wamelazimika kuirudisha ccm madarakani kwa kosa kubwa la kiitifaki lililoamuliwa na familia moja tu ndani ya chama.
Wanachama wa chadema asilia ni wazi wanatafakari hasa baada ya ushindi wa kishindo wa Magufuli ni kwa vipi wanaweza kukinusuru chama chao kisiporomoke kama NCCR,CUF na TLP.
Wanachadema asilia wanatafuta mwenyekiti kwani haiwezekani Wangwe,Arfi,Zitto,Kitila,Mwigamba na Slaa wakawa na matatizo...tatizo ni mwenyekiti na akiendelea kuchekewa chama kitafutika kwenye ramani ya kisiasa.
Wanachadema asilia wanatambua wanayo haki ya kisheria ya kukiondoa chama mikononi mwa familia ya mtei.
Wanachadema asilia wanataka kuona mfumo wa uteuzi wa wagombea ndani ya chama unakuwa wazi na kufuata taratibu za chama.
Wanachadema asilia wanataka kuona mgao wa ruzuku unakuwa fairly distributed na sio kuwafikia baadhi ya wanaojidai makamanda kutoka kaskazini.
Ni katibu aliyeondolewa na Mbowe ndio aliyetuelekeza kwenda mitaani na vijijini ili kukikuza chama na aliahidi kutupima kwa hilo.leo hii Mbowe amemfanya katibu ni mvivu.
Wanachadema asilia hawajapewa fursa rasmi ya kumpitisha lowassa kuwa mgombea urais kupitia chadema.hili limefanyika kiujanjaujanja kwa kuwa Mwenyekiti anajua wanachama wangelipinga kwani mgombea huyu hana sifa za kikamanda wala hajui misingi ya kuwa kamanda wa wananchi wanyonge.
Wanachadema asilia hawakupewa fursa ya kuamua au kujua jinsi gani mchakato wa kuachiana majimbo utakavyokuwa.sana sana mchakato ulisikika kwenye vyombo vya habari tu.
Wanachadema asilia walijitoa kwa hali,mali na uhai wao kwa kutarajia Tanzania mpya inazaliwa ikiwa haina ufisadi,uongo,udini,ukanda,ufamilia,ukabaila na usaliti badala yake Mwenyekiti na timu ya wachache imetuletea mamluki wanaokichafua chama na kukiacha kikiwa vipande vipande.
Kwa heshima ya Wangwe,Zitto,Slaa,Arfi,Kitila,Kafulila na wengine ni lazima Mwenyekiti uondolewe kwani wewe ndio tatizo.Mwenyekiti umebebwa sana na think tanks ndani ya Chadema na malipo yao yamekuwa ni kuwafukuza tu.
Mwisho wa Mbowe kuwa mwenyekiti Chadema ni oktoba 25.
SENT AS RECEIVED!