Tetesi: Baada ya Serikali kuanza mahojiano na Nyalandu kuhusu kashfa katika Wizara ya Maliasili na Utalii, atimkia CHADEMA

Tetesi: Baada ya Serikali kuanza mahojiano na Nyalandu kuhusu kashfa katika Wizara ya Maliasili na Utalii, atimkia CHADEMA

Wiki iliyopita Waziri wa Maliasili na Utalii, Dr. Hamisi Kigwangalla, akizungumza na wadau wa Wizara yake alisema kuwa baadhi ya mawaziri na wabunge wa awamu ya nne wangepaswa kuwa jela kwa ufisadi na ushiriki wao kwenye ujangili. Leo Nyalandu amekimbia. Ifuatayo ni historia ya kashfa moja ya Nyalandu.

Kampuni ya Kimarekani ya Friedkin Conservation Fund (FCF) ambayo inamiliki kampuni tanzu za uwindaji wa kitalii za Mwiba Holdings Ltd, Tanzania Game Trackers Safaris (TGTS) ni miongoni mwa watuhumiwa wa ujangili
Uchunguzi unaonesha kumekuwapo matukio kadhaa ya wafanyakazi wa Mwiba kukamatwa wakiwa wameua wanyamapori na kukutwa na nyara za Serikali.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii vimesema mara zote kesi zinazoihusu kampuni hizo zimekwama kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni urafiki wao wa karibu na aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Nyalandu.

Urafiki wa Nyalandu na wamiliki wa kampuni hizo ulikuwa mkubwa kiasi cha kumpatia moja ya helikopta zake aitumie kwenye mbio za kuwania urais, kabla ya kushindwa na kujielekeza kwenye ubunge.

Helikopta ya kampuni hiyo ndiyo aliyoitumia wakati wote wa kampeni zake za ubunge
Nyalandu alimwamuru Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori wa wakati huo, Paul Sarakikya, kutoa Leseni ya Rais kwa familia ya Tom Friedkin (mmiliki wa kampuni hizi) kuwinda wanyamapori 700 katika vitalu vinane na eneo la wazi la Makao. Leseni hizo zilitolewa bure bila kulipiwa hata senti.

Miongoni mwa wanyamapori waliokuwa kwenye orodha ya kuuawa ni tembo walio katika hatari ya kutoweka.

Pia Nyalandu alikiuka sheria kwa kupuuza ukomo wa idadi ya vitalu vitano kwa kampuni moja. TGTS imemilikishwa vitalu vinane pamoja na eneo la wazi; hali ambayo ni ukiukwaji wa kifungu cha 38(7) cha Sheria ya Wanyamapori.

Kampuni hiyo pia ilipewa vitalu na Nyalandu kinyemela, ilhali sheria ikiagiza kuwa kitalu kinapobaki wazi sharti kitangazwe kwanza na waombaji washindanishwe katika mfumo na utaratibu ulio wa haki na uwazi [Kanuni ya Uwindaji wa Kitalii 18(1).

Pamoja na kutoa Leseni ya Rais, Wamarekani hao walileta watoto wadogo, chini ya umri wa miaka 18 kuwinda; jambo ambalo ni kinyume cha kifungu cha 43(3) cha Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009.

FCF na kampuni tanzu imekuwa ikiendesha shughuli za utalii kwenye eneo la Makao WMA tangu 2011 baada ya Mwiba Holdings Ltd kumilikishwa eneo jirani na WMA ya Makao kwa ajili ya shamba la mifugo na wanyama (Makao Ranch).

Kampuni ya Mwiba Holdings Ltd chini ya TGTS Ltd ambazo zinamilikiwa na Friedkin Conservation Fund (FCF) imekuwa ikiendesha shughuli za utalii kwenye eneo la Makao WMA tangu 2011 baada ya Mwiba Holdings Ltd kumilikishwa eneo jirani na WMA ya Makao kwa ajili ya shamba la mifugo na wanyama.

Hata baada ya kumalizika Mkataba wake na JUHIWAPOMA, kampuni ya Mwiba Holdings Ltd iling’ang’ania na kuendelea kukalia eneo la Makao WMA kwa mabavu na kinyume cha sheria.

Tutawaletea moja baada ya nyingine.

Watz nimeamini kwa majungu tunaoongoza.Mtu akiishatangaza kuhama kambi fulani tayari kuna kundi kubwa humu ndani kazi yao ni kutengenza threads za kuchafuana lkn akiwa na madaraka ndani ya vyama hivyo hakuna anayesema mabaya yao.kwa kweli si ustaarabu na si hulka yetu watz.hali hii naiona jinsi tunavyosonga mbele inazidi kupata kasi ya ajabu.kwa nini tunapenda kuwadhalilisha watu wengine wanapoamua kufanya maamuzi wanayotaka?
Inasikitisha sana humu ndani wanajf jinsi wanavyomshambulia nyarandu wengine wameenda mbali zaidi kiasi cha kumualia nini afanye.tuachane na hizo negativity na tuwe realistic tunapojadili mambo.tuwajadili watu kwa uzuri na tuachane na tabia ya kuchafuana ktk mitandao hii haina afya kwetu kabisa.tujifunze siasa kutoka kwa majirani zetu ndo maana watu tumechoka hata kusoma magazeti ya tz sababu hata uandishi wake hauna afya na maslahi kwa nchi bali ni wa chuki tu.
 
Moja ya kitu kibaya zaidi kwa maisha ya mwanadamu ni woga, woga humfanya mwanadamu aishi maisha ya kinyonge mpaka anaingia kaburini
 
Why now, bado keshawapiga goli ccm nijuavyo Mimi akiguswa lazima na Kikwete aguswe. Katiba mbovu huzaa majanga
 
ni upumbavu usio na kifani mtu akiwa ccm msafi akitoka mwizi
 
Mlikuwa wapi kumchafua wakati mko naye, leo amekataa kula sahani moja ndo mnatuletea tupicha picha tu, siku hizi picha zinapikwa hivyo katafute ushahidi mwingine utuletee wa tofauti na hako kapicha, kwani hiyo picha imekosa nini wakati kaipiga public mbele za watu au unaona yuko na huyo chumbani?
 
Mkuu ukisema nyalandu kamkimbia kigwangala.
Utakuwa unakosea.

KWANI NYALANDU AMEKIMBIA NCHI?
SI YUPO HAPA HAPA?

Sasa kamkimbia vipi?
Naomba ufafanuzi tafadhali.
Ufafanuzi ni kwamba alikokimbilia kuna watetezi wa UFISADI.
 
Wiki iliyopita Waziri wa Maliasili na Utalii, Dr. Hamisi Kigwangalla, akizungumza na wadau wa Wizara yake alisema kuwa baadhi ya mawaziri na wabunge wa awamu ya nne wangepaswa kuwa jela kwa ufisadi na ushiriki wao kwenye ujangili. Leo Nyalandu amekimbia. Ifuatayo ni historia ya kashfa moja ya Nyalandu.

Kampuni ya Kimarekani ya Friedkin Conservation Fund (FCF) ambayo inamiliki kampuni tanzu za uwindaji wa kitalii za Mwiba Holdings Ltd, Tanzania Game Trackers Safaris (TGTS) ni miongoni mwa watuhumiwa wa ujangili
Uchunguzi unaonesha kumekuwapo matukio kadhaa ya wafanyakazi wa Mwiba kukamatwa wakiwa wameua wanyamapori na kukutwa na nyara za Serikali.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii vimesema mara zote kesi zinazoihusu kampuni hizo zimekwama kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni urafiki wao wa karibu na aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Nyalandu.

Urafiki wa Nyalandu na wamiliki wa kampuni hizo ulikuwa mkubwa kiasi cha kumpatia moja ya helikopta zake aitumie kwenye mbio za kuwania urais, kabla ya kushindwa na kujielekeza kwenye ubunge.

Helikopta ya kampuni hiyo ndiyo aliyoitumia wakati wote wa kampeni zake za ubunge
Nyalandu alimwamuru Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori wa wakati huo, Paul Sarakikya, kutoa Leseni ya Rais kwa familia ya Tom Friedkin (mmiliki wa kampuni hizi) kuwinda wanyamapori 700 katika vitalu vinane na eneo la wazi la Makao. Leseni hizo zilitolewa bure bila kulipiwa hata senti.

Miongoni mwa wanyamapori waliokuwa kwenye orodha ya kuuawa ni tembo walio katika hatari ya kutoweka.

Pia Nyalandu alikiuka sheria kwa kupuuza ukomo wa idadi ya vitalu vitano kwa kampuni moja. TGTS imemilikishwa vitalu vinane pamoja na eneo la wazi; hali ambayo ni ukiukwaji wa kifungu cha 38(7) cha Sheria ya Wanyamapori.

Kampuni hiyo pia ilipewa vitalu na Nyalandu kinyemela, ilhali sheria ikiagiza kuwa kitalu kinapobaki wazi sharti kitangazwe kwanza na waombaji washindanishwe katika mfumo na utaratibu ulio wa haki na uwazi [Kanuni ya Uwindaji wa Kitalii 18(1).

Pamoja na kutoa Leseni ya Rais, Wamarekani hao walileta watoto wadogo, chini ya umri wa miaka 18 kuwinda; jambo ambalo ni kinyume cha kifungu cha 43(3) cha Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009.

FCF na kampuni tanzu imekuwa ikiendesha shughuli za utalii kwenye eneo la Makao WMA tangu 2011 baada ya Mwiba Holdings Ltd kumilikishwa eneo jirani na WMA ya Makao kwa ajili ya shamba la mifugo na wanyama (Makao Ranch).

Kampuni ya Mwiba Holdings Ltd chini ya TGTS Ltd ambazo zinamilikiwa na Friedkin Conservation Fund (FCF) imekuwa ikiendesha shughuli za utalii kwenye eneo la Makao WMA tangu 2011 baada ya Mwiba Holdings Ltd kumilikishwa eneo jirani na WMA ya Makao kwa ajili ya shamba la mifugo na wanyama.

Hata baada ya kumalizika Mkataba wake na JUHIWAPOMA, kampuni ya Mwiba Holdings Ltd iling’ang’ania na kuendelea kukalia eneo la Makao WMA kwa mabavu na kinyume cha sheria.

Tutawaletea moja baada ya nyingine.
Yaani mkae na mbunge jangili kwa miaka miwili hamumshitaki, halafu leo kaondoka mnaanza? Hapo mmekosea timing, lolote mtakalofanya ni uonevu tu.
Ndio maana tunasema CCM haiwezi kupambana na ufisadi. Leo Ngeleja amerudisha mabilioni yake ya Escrow lakini amesamehewa, siku akihama chama kesi zinafufuliwa.
 
Mimi ni mkazi wa Arusha mjini na nilishawahi nunua kiwanja kule Sanawari ya Juu Arusha jirani na alikojenga Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu jumba kubwa na nafikiri anaishi humo kwa sasa na amebase Arusha badala ya Singida au Arusha na Dar kama walivyo wabunge wengi wa CCM na upinzani.

Tusishangae 2020 Nyalandu akigombea ubunge Arusha Magharibi kama atashindwa Urais kupitia CDM.

Nashauri tu tunapojadili siasa na wanasiasa tusizame sana kuwatetea maana hatuwajui wala hatutawajua unless wewe nawe ni mwanasiasa au mnufaika wa siasa chafu za TZ
 
Mimi ni mkazi wa Arusha mjini na nilishawahi nunua kiwanja kule Sanawari ya Juu Arusha jirani na alikojenga Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu jumba kubwa na nafikiri anaishi humo kwa sasa na amebase Arusha badala ya Singida au Arusha na Dar kama walivyo wabunge wengi wa CCM na upinzani.

Tusishangae 2020 Nyalandu akigombea ubunge Arusha Magharibi kama atashindwa Urais kupitia CDM.

Nashauri tu tunapojadili siasa na wanasiasa tusizame sana kuwatetea maana hatuwajui wala hatutawajua unless wewe nawe ni mwanasiasa au mnufaika wa siasa chafu za TZ

AnayoHAKI kujenga Tanzania popote apendapo ila hana haki ya kufanya ubadhirifu,kama kuna kesi ya UFISADI au UBADHIRIFU rukhsa kumshataki
 
tangu jana mh lazaro nyarandu alaipo tangaza kujiuzulu ccm na kuhamia cdm yamezuka mambo ambayo tusiyofaham kuhusu uongozi wake kwenye wizara hiyo ya maliasili hizi ni baadhi tuu ya picha pindi akiwa Waziri katika wizara ya maliasili [HASHTAG]#source[/HASHTAG] tanzamwanga /facebook page
View attachment 621161
Facebook ndiyo source ya hizo taarabu zako alfu mbona avatar yako upo kama jike au sio riziki mkuu?
 
Amekimbia kesi zake huyu anataka kujificha nyuma ya chadema ili wananchi waseme anaonewa kwa kua kahama chama
 
Back
Top Bottom