Baada ya uamuzi wa Mahakama ya Kenya,Zitto asema Katiba Mpya ni lazima lazima lazima

Tatizo la watanzania ni kuamini kwamba katiba mpya unapewa na mtesi wako. CCM hayuko tayari kukupa katiba mpya. Unapigania katiba mpya.

Uhuru tulipewa maana nchi ikikuwa under the mandate of Great Britain. Sasa tunadhani hata katiba tutapewa bure.
 
Katiba mpya haitakua na maana Tanzania endapo wagombea urais wa Tanzania ni walewale akina Lowasa na wapiga deal wenzie..!
 
Hakuna kipya ...kwani hatujui hilo? Tunawataka waje na mikakati si porojo za umuhimu wa katiba mpya ambazo tunazijua .....
Hivi kweli kabisa mtu unasema katiba mpya ni porojo!!! Ama kweli Tanzania tuna safari ndefu sana kama watu wenyewe ndio kama hawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna kipya ...kwani hatujui hilo? Tunawataka waje na mikakati si porojo za umuhimu wa katiba mpya ambazo tunazijua .....

..hivi kwanini SERIKALI isipeleke Bungeni muswada wa kufanyia marekebisho sheria mbalimbali?

..Kwa hali ilivyo sasa hivi suala hili likianzia upinzani litakwama kwasababu ya wingi wa wabunge wa ccm ktk bunge la jamhuri.

..Kwa uchache, na kwa kuanzia SERIKALI inaweza kupeleka mswada utakaoleta mambo yafuatayo.

1. Tume Huru ya Uchaguzi.

2. Vyama kuruhusiwa kuungana bila kulazimika kujifuta na kuanza sifuri.

3.Matokeo ya udiwani, ubunge, uraisi, kuhojiwa mahakamani.

4.Kuna na Mahakama huru. Jaji Mkuu na Jaji Kiongozi wathibitishwe na bunge.


..Nadhani Prof.Kabudi ni mhubiri wa hayo niliyoyaorodhesha hapo juu. Sielewi kwanini hapeleki mswada wenye mabadiliko hayo bungeni.
 
Hivi zito hakutoka nje wakati wakujadiliana kupata katiba eeh
 
Katiba sio kipaumbele cha serikali ya awamu hii, tuiache serikali ijenge viwanda kwanza.

mafisadi hayana rangi
 
Nyinyi viongozi wa vyama ndio wa kusindikiza hayo mambo mkiwa ndani ya bunge na nje ya bunge muhamasishe wananchi kufanya migomo na maandamano ili watawala wajuwe kwamba wananchi wamechoka kutawaliwa wanataka kuongozwa kisheria na kufuata katiba co kila ck tundu lissu .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…