Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 20,654
- 35,887
Heshima sana wanajamvi,
Katibu Mkuu wa chama chochote ukiondoa vile vyama vya msimo wa uchaguzi ndiye mtendaji mkuu wa shughuli na utendaji wa chama za kila siku.Chama tawala CCM kimewabadili makatibu wakuu kwasababu mbali mbali lakini nyingi kati ya hizo sababu ni kushindwa kwenda na wakati au kushindwa kutimiza majukumu ya chama.
Tumewashuhudia makatibu wakuu wengi wakiondoka na wengine wakiingia katika nafasi hiyo nyeti ya kiutendaji.Tuliona kina Hayati Kawawa,Kolimba,Makamba na mwisho Mh Kinana wakiondolewa wengine kwa fedhea na wengine wakistaafu kwa heshima kubwa.
Dr Bashiru ni msomi mkubwa,kabla hajaibuliwa chamani alikuwa Mhadhiri UDSM tena mbobezi mkubwa katika fani ya siasa.Nilitegemea kuona mabadiliko makubwa ndani ya chama kupitia Mbobezi huyu wa siasa lakini katika hali ya mshangao mkubwa chini ya utendaji wake tulishuhudia CCM ikitegemea zaidi nguvu ya vyombo vya dola kuliko WANANCHI au WANACHAMA.Chini ya uongozi wake zilizaliwa siasa za kuunga mkono juhudi
Sasa tunaweza kusema pasipo shaka kwamba wasomi wetu wabobezi hawana kitu cha ziada ukiwalinganisha na Wazee wetu kama Mzee Kawawa.Wasomi wetu wa leo wanafanya mambo ya hovyo hovyo kuliko yaliyofanywa na wazee wetu wengi waliomaliza darasa la nane au kumi kipindi cha ukoloni.Elimu yetu ya leo imejaa wingi wa vyeti na mbwe mbwe nyingi pasipo maarifa.Kati ya mabo ya hovyo kuwahi kufanywa na CCM ni suala la kununua wapinzani halafu kuandaa chaguzi za kiini macho ambazo wananchi walinyimwa fursa ya kuchagua.
Ni matarajio ya wengi baada ya uchaguzi huu Dr Bashiru ataondolewa mara moja kwasababu ya kushindwa kumshauri vizuri Mwenyekiti wake.Hata baada ya kukaa katika nafasi ya Katibu Mkuu kwa muda wa kutosha bado anaonekana hakijui chama.
Wasalam Ngongo safarini Katavi Mpanda Mjini kwasasa.
Katibu Mkuu wa chama chochote ukiondoa vile vyama vya msimo wa uchaguzi ndiye mtendaji mkuu wa shughuli na utendaji wa chama za kila siku.Chama tawala CCM kimewabadili makatibu wakuu kwasababu mbali mbali lakini nyingi kati ya hizo sababu ni kushindwa kwenda na wakati au kushindwa kutimiza majukumu ya chama.
Tumewashuhudia makatibu wakuu wengi wakiondoka na wengine wakiingia katika nafasi hiyo nyeti ya kiutendaji.Tuliona kina Hayati Kawawa,Kolimba,Makamba na mwisho Mh Kinana wakiondolewa wengine kwa fedhea na wengine wakistaafu kwa heshima kubwa.
Dr Bashiru ni msomi mkubwa,kabla hajaibuliwa chamani alikuwa Mhadhiri UDSM tena mbobezi mkubwa katika fani ya siasa.Nilitegemea kuona mabadiliko makubwa ndani ya chama kupitia Mbobezi huyu wa siasa lakini katika hali ya mshangao mkubwa chini ya utendaji wake tulishuhudia CCM ikitegemea zaidi nguvu ya vyombo vya dola kuliko WANANCHI au WANACHAMA.Chini ya uongozi wake zilizaliwa siasa za kuunga mkono juhudi
Sasa tunaweza kusema pasipo shaka kwamba wasomi wetu wabobezi hawana kitu cha ziada ukiwalinganisha na Wazee wetu kama Mzee Kawawa.Wasomi wetu wa leo wanafanya mambo ya hovyo hovyo kuliko yaliyofanywa na wazee wetu wengi waliomaliza darasa la nane au kumi kipindi cha ukoloni.Elimu yetu ya leo imejaa wingi wa vyeti na mbwe mbwe nyingi pasipo maarifa.Kati ya mabo ya hovyo kuwahi kufanywa na CCM ni suala la kununua wapinzani halafu kuandaa chaguzi za kiini macho ambazo wananchi walinyimwa fursa ya kuchagua.
Ni matarajio ya wengi baada ya uchaguzi huu Dr Bashiru ataondolewa mara moja kwasababu ya kushindwa kumshauri vizuri Mwenyekiti wake.Hata baada ya kukaa katika nafasi ya Katibu Mkuu kwa muda wa kutosha bado anaonekana hakijui chama.
Wasalam Ngongo safarini Katavi Mpanda Mjini kwasasa.