Baada ya vurugu kubwa, ofisi na madarasa kuchomwa moto ndipo mabadiliko yakaja!

Baada ya vurugu kubwa, ofisi na madarasa kuchomwa moto ndipo mabadiliko yakaja!

Lavit

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2011
Posts
14,834
Reaction score
32,522
Wakuu leo nimekumbuka takribani miaka 20 iliyopita nilikuwa kidato cha nne shule ya serikali huko Mbeya.
Sasa pale shule toka tunafika form 1 kulikuwa na malalamiko makubwa sana kuhusu chakula kibovu, malalamiko yalikuwa mengi sana ila yalipuuzwa hasa na second master aliyekuwa amekaa pale kwa zaidi ya miaka 20.

Sasa 2005 miezi kama hii vuguvugu likawa kubwa sana kwa wanafunzi kuchoshwa kula dona (sisi tulikuwa tunaita shudu), na yalikuwa mashudu kweli maana yale mahindi yalikuwa yanasagwa yakiwa machafu na muda mwingine yakiwa yameoza kabisa.

Nakumbuka tetesi za mgomo zilianza kama utani zikihusisha viongozi wote wa mabweni, second master alivyopata taarifa aliitisha kikao ambacho aliishia kututisha kwamba hata kama watabadilisha chakula sio kwa ajiri ya kale kamgomo ketu.
Muda ulienda na ikawa bahati walimu walikuwa na sherehe yao, wakiwa wamepika pilau na bia za kutosha huku sisi wakiwa wametuachia "shudu"

Sasa kilichotokea, ile sherehe haikufanyika maana staff ilivamiwa na vioo vilivunjwa, baadaye ofisi ya nidhamu na madarasa mawili yalichomwa moto. Nakumbuka FFU walikuja usiku ule ule, huku wakikuta watu wengi hatupo pale shuleni!

Kulipokucha wengi tulirudi, cha ajabu na kushangaza siku ile tulikula ugali wa sembe na kwa mara ya kwanza tukagaiwa matunda.

Matokeo yake wengi walifukuzwa shule, na tuliobaki tulipigwa fine. Ila toka hapo mambo yalibadilika, yule second master kiburi aliomba uhamisho maana alidai hawezi tena kubaki ile shule labda kuwe hamna shule nyingine hii nchi.

Nb; nilichojifunza ni kwamba ni ngumu sana kuleta mabadiliko kwa kuongea tu, maongezi yetu ya miaka nenda rudi yalikuja kuhitimishwa na vurugu ya siku moja. Wale walimu wasingeweza kufanya mabadiliko hivi hivi wakati walikuwa wanufaika wa kutulisha chakula kibovu.
 
Nb; nilichojifunza ni kwamba ni ngumu sana kuleta mabadiliko kwa kuongea tu, maongezi yetu ya miaka nenda rudi yalikuja kuhitimishwa na vurugu ya siku moja. Wale walimu wasingeweza kufanya mabadiliko hivi hivi wakati walikuwa wanufaika wa kutulisha chakula kibovu.
Kwa hio CDM na wao watafute Bunduki kupambana na Polisi waiba kura za uchaguzi?
 
Wakuu leo nimekumbuka takribani miaka 20 iliyopita nilikuwa kidato cha nne shule ya serikali huko Mbeya.
Sasa pale shule toka tunafika form 1 kulikuwa na malalamiko makubwa sana kuhusu chakula kibovu, malalamiko yalikuwa mengi sana ila yalipuuzwa hasa na second master aliyekuwa amekaa pale kwa zaidi ya miaka 20.

Sasa 2005 miezi kama hii vuguvugu likawa kubwa sana kwa wanafunzi kuchoshwa kula dona (sisi tulikuwa tunaita shudu), na yalikuwa mashudu kweli maana yale mahindi yalikuwa yanasagwa yakiwa machafu na muda mwingine yakiwa yameoza kabisa.

Nakumbuka tetesi za mgomo zilianza kama utani zikihusisha viongozi wote wa mabweni, second master alivyopata taarifa aliitisha kikao ambacho aliishia kututisha kwamba hata kama watabadilisha chakula sio kwa ajiri ya kale kamgomo ketu.
Muda ulienda na ikawa bahati walimu walikuwa na sherehe yao, wakiwa wamepika pilau na bia za kutosha huku sisi wakiwa wametuachia "shudu"

Sasa kilichotokea, ile sherehe haikufanyika maana staff ilivamiwa na vioo vilivunjwa, baadaye ofisi ya nidhamu na madarasa mawili yalichomwa moto. Nakumbuka FFU walikuja usiku ule ule, huku wakikuta watu wengi hatupo pale shuleni!

Kulipokucha wengi tulirudi, cha ajabu na kushangaza siku ile tulikula ugali wa sembe na kwa mara ya kwanza tukagaiwa matunda.

Matokeo yake wengi walifukuzwa shule, na tuliobaki tulipigwa fine. Ila toka hapo mambo yalibadilika, yule second master kiburi aliomba uhamisho maana alidai hawezi tena kubaki ile shule labda kuwe hamna shule nyingine hii nchi.

Nb; nilichojifunza ni kwamba ni ngumu sana kuleta mabadiliko kwa kuongea tu, maongezi yetu ya miaka nenda rudi yalikuja kuhitimishwa na vurugu ya siku moja. Wale walimu wasingeweza kufanya mabadiliko hivi hivi wakati walikuwa hiywanufaika wa kutulisha chakula kibovu.
Hiyo shule nahisi naifahamu .safi sana ccm kuna la kujifunza
 
Hiyo inaitwa kufactory reset. Huwa inakuja na gharama kubwa sana.

Ukiona mataifa makubwa wanavyoishi unaweza fikiri imetokea tu kumbe walishafumuana sana miaka hiyo.
Geita huko madogo wamepiga Walimu na Walinzi wa Shule kisa mwenzao kasimamishwa Shule kwa kukutwa na Simu, wakalianzisha tifu piga Walimu piiga Walinzi mpaka Polisi wakaja
 
Geita huko madogo wamepiga Walimu na Walinzi wa Shule kisa mwenzao kasimamishwa Shule kwa kukutwa na Simu, wakalianzisha tifu piga Walimu piiga Walinzi mpaka Polisi wakaja
Hao washamba tu. Kipindi wanajiunga na hiyo shule si walisomewa sheria?
 
Hiyo inaitwa kufactory reset. Huwa inakuja na gharama kubwa sana.

Ukiona mataifa makubwa wanavyoishi unaweza fikiri imetokea tu kumbe walishafumuana sana miaka hiyo.
Mabadiliko hayajaja hivi hivi...sisi tunasubiri changes kwa kuchekeana
 
Kuna ka mgomo tulifanya tosamaganga miaka hiyo 😀😀😀, rafiki yangu Amon.... kama upo humu utaelewa hii code
 
Hahaha ume nikumbusha nili mwambia kaka wa marehemu mzee wangu, kuwa ana tamaa za kijenge Sana 😂 😂

Wakuu leo nimekumbuka takribani miaka 20 iliyopita nilikuwa kidato cha nne shule ya serikali huko Mbeya.
Sasa pale shule toka tunafika form 1 kulikuwa na malalamiko makubwa sana kuhusu chakula kibovu, malalamiko yalikuwa mengi sana ila yalipuuzwa hasa na second master aliyekuwa amekaa pale kwa zaidi ya miaka 20.

Sasa 2005 miezi kama hii vuguvugu likawa kubwa sana kwa wanafunzi kuchoshwa kula dona (sisi tulikuwa tunaita shudu), na yalikuwa mashudu kweli maana yale mahindi yalikuwa yanasagwa yakiwa machafu na muda mwingine yakiwa yameoza kabisa.

Nakumbuka tetesi za mgomo zilianza kama utani zikihusisha viongozi wote wa mabweni, second master alivyopata taarifa aliitisha kikao ambacho aliishia kututisha kwamba hata kama watabadilisha chakula sio kwa ajiri ya kale kamgomo ketu.
Muda ulienda na ikawa bahati walimu walikuwa na sherehe yao, wakiwa wamepika pilau na bia za kutosha huku sisi wakiwa wametuachia "shudu"

Sasa kilichotokea, ile sherehe haikufanyika maana staff ilivamiwa na vioo vilivunjwa, baadaye ofisi ya nidhamu na madarasa mawili yalichomwa moto. Nakumbuka FFU walikuja usiku ule ule, huku wakikuta watu wengi hatupo pale shuleni!

Kulipokucha wengi tulirudi, cha ajabu na kushangaza siku ile tulikula ugali wa sembe na kwa mara ya kwanza tukagaiwa matunda.

Matokeo yake wengi walifukuzwa shule, na tuliobaki tulipigwa fine. Ila toka hapo mambo yalibadilika, yule second master kiburi aliomba uhamisho maana alidai hawezi tena kubaki ile shule labda kuwe hamna shule nyingine hii nchi.

Nb; nilichojifunza ni kwamba ni ngumu sana kuleta mabadiliko kwa kuongea tu, maongezi yetu ya miaka nenda rudi yalikuja kuhitimishwa na vurugu ya siku moja. Wale walimu wasingeweza kufanya mabadiliko hivi hivi wakati walikuwa wanufaika wa kutulisha chakula kibovu.
Mbona ni kama fumbo hili!
 
Mabadiliko hayajaja hivi hivi...sisi tunasubiri changes kwa kuchekeana
Mambo yale hayapangwi yanatokea tu.

Watanzania bado wana uhakika wa kula milo mitatu kwa siku. Itapofika siku mtu akifungua biashara inakufa ndani ya mwezi, hata mia ya kununua chakula hana, watoto wamefukuzwa shule ada zipo juu. Sio Mbowe sio Lissu sio Zitto atayeshawishi watu waandamane kudai mabadiliko ya uongozi.

Watanzania bado tupo kwenye uhakika lakini nakukuhakikisha CCM taratibu wanaanza kuvuruga hata mahitaji muhimu ya kibinadamu kuyapata inakua shida. Ndio tunakoelekea.
 
Miaka ile vyakula vilikuwa vya hovyo san mashuleni. Ila pale Mkwawa High School tulikuwa tunakula kama cha nyumbani tu. Na wakati wa kula tunakaa mezani na kula kistaarabu. Ile ilikuwa kama mini-university
 
Back
Top Bottom